Donald Trump: I Will Lock Mugabe, Museveni in Prison

Status
Not open for further replies.
Ninamkubali sana Trump kwasababu hana muda wa kudanganya umma na nafsi yake. Obama hakuwahi kutoa ahadi ya kumwangusha Muammar Qaddafi na kuipeleka Libya katika mchafuko lakini alifanya hivyo na hali ya Libya sote tunashuhudia.
Siungi mkono kukiukwa kwa uhuru wa taifa moja kiasi cha kuingiliwa mambo yake ya ndani lakini kwa namna dunia inavyoendeshwa sasa suala hili haliepukiki. Hii ni kwasababu kuna njia nyingi za kufanya infiltration kwa mataifa ya Afrika hususani Uganda na Zimbazwe ambako demokrasia imepewa kisogo kwa muda mrefu.
 
Daah napenda sanaa maneno ya huyu mtu yaani yamejaa ukweli na ujasiri sanaa. Mtu wa aina hii ni wako wachache sanaa Duniani..Mungu bless Donald Trump to ascend the throne.
 






Mkubwa jaribu kuilinda kama "mboni" heshima yako kidogo isiyoweza kujaa hata kisoda uliyobaki nayo hapa jukwaani.Hivi ni kweli kwa Elimu ya MEMKWA uliyonayo umeshindwa hata kujuwa muundo wa serikali za kifalme? Hapana!!!!,nahisi hapa umetania tu wala hujamaanisha ulichokiandika.
 
Huyu bwana akishirikiana na papa watatimiza maneno ya unabii yaliyonenwa ktk biblia ikiwemo kushurutisha wakazi wote wa dunia kufanya kazi kwa siku zote 7 za wiki isipokuwa jumapili
 
.Hivi ni kweli kwa Elimu ya MEMKWA uliyonayo umeshindwa hata kujuwa muundo wa serikali za kifalme? .

Hapa ndipo wasomi koko kama wewe wanapoonyesha kuwa waabudu wazungu.Kama uingereza wana muundo wao wa Malkia kutawala milele na muundo huo unaheshimiwa na Marekani,Kwa nini Uganda au Zimbabwe wasiwe na muundo wao ambao Marekani inabidi iuheshimu kama wanavyoheshimu muundo wa uingereza?

Tukiwa na waswahili waimba nyimbo za wazungu kama wewe hatuji kuendelea waafrika.Wao wana muundo wao hadi wa mashoga wanataka waheshimiwe lakini hawako tayari kuheshimu miindo yetu.LAZIMA UJITAMBUE.

Hawa ni watu wa ajabu mfano Tanzania walitushinikiza kuanzisha mfumo wa vyama vingi wakisema ndio wa kidemokrasia.Wakatishia kuvunja hata mahusiano kama hatutaruhusu huo mfumo.Lakini China haina vyama vingi ina chama kimoja tu lakini mmarekani kaufyata hathubutu hata kunyanyua mdomo kumwambia China weka vyama vingi kwa sababu wachina wanajitambua.Tanzania tuna tatizo la watu kama wewe wasiojitambua.Mtoto wa Kikwete akishika uongozi utasikia ona wanarithishana.Lakini Bush akimrithisha mwanae Bush uongozi mnakenua meno tu hamlaani wala kusema chochote.

Mke wa KIkwete akishika uongozi nongwa.Na wazungu watapiga kelele.Lakini Raisi Clinton akimrithisa mkewe CHEO na kumfanyia kampeni mnakenua meno tu.

Watu kama wewe ni mzigo kwa bara la Afrika.
 
Wewe huwa unaandika makala ndefu zisizo na
akili na ndo unae tegemewa kuongoza jahazi la lumumba humu.... ufalme wa malkia ni tofauti hata na wa king Mswati maana mswati anaongoza serikali.... malikia ni simble au ceremonial leader... haongozi serikali mkubwa....
 
Anawajua wazungu au unawasikia? utawewaza kwa kipi hasa au ni maneno ya Kahawani
 
. malikia ni simble au ceremonial leader... haongozi serikali mkubwa....

Kazi unayo aliyekwambia ni ceremonial ni nani huyo?

QUEEN ndiye kiongozi wa nchi (HEAD OF STATE)

Miswada yote ya sheria ndiye huwa anasaini kama ambavyo Raisi wetu anafanya BILA KUSAINI YEYE HAUWI SHERIA Angalia kazi zake kwenye website ya ufalme wa uingereza.Wasomi wa UKAWA mnatuangusha.Ndio maana si rahisi kumkuta Profesa mwanachama wa UKAWA labda awe ana matatizo ya akili.

http://www.royal.gov.uk/MonarchUK/HowtheMonarchyworks/theroleofthesovereign.aspx
 
this is a serious mental case! I hope America will not dare vote him in.
 
Mkuu nani anaunda serikali? Nani anateua mawaziri? Kama huna shida na ki english utanielewa ukisoma kipande hiki.....

As 'Head of Nation', The Queen's role is less
formal, but no less important for the social and cultural functions it fulfils.

" neno less formal" linaeleza nnacho kueleza....
 
Huyu bwana akishirikiana na papa watatimiza maneno ya unabii yaliyonenwa ktk biblia ikiwemo kushurutisha wakazi wote wa dunia kufanya kazi kwa siku zote 7 za wiki isipokuwa jumapili
hapo sijaelewa kidogo,siku zote 7 za wiki isipokuwa jumapili,fafanua vizuri tafadhali
 
hapo sijaelewa kidogo,siku zote 7 za wiki isipokuwa jumapili,fafanua vizuri tafadhali
Ktk masomo ya unabii kuna jambo linaongelewa kuwa itafika wakati watu wote watalazimishwa kuwa na siku 1 ya ibada ambayo Itakuwa j pili ktk kupambana na Kile wanachokiita uvivu uliofichika ktk muda mwingi wa kuabudu, search ktk mtandao Sunday law (Sheria ya jumapili)
 
Babu Mugabe alikwisha wadharau hawa marekani siku nyingi; siku hizi hata hela yao ameidharau kwani Zimbabwe wanatumia YUAN fedha za kiChina!!!

😀 still anatumia dola, lkn haina thamani! dola moja=shilingi 6 yahuku, dola 50=shilingi 302 yahuku
 



Naweza pata link la hicho alichosema from reliable source kama , web ya gazet au TV au video clip ikibidi. Maana imefika wakati kila mtu anatunga stori kuhusu Trump tunapotezeana tu muda wa kusoma
 
Naweza pata link la hicho alichosema from reliable source kama , web ya gazet au TV au video clip ikibidi. Maana imefika wakati kila mtu anatunga stori kuhusu Trump tunapotezeana tu muda wa kusoma
 
Halafu mangi hiyo mbege unanywea wapi aisee!dunia inabadilika kazi hakuna ni mashine na marobot ndio zinafanya kazi, kweli mangi haujui hilo sasa itakuaje
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…