Dowans wanatunyonga hivi

Dah tutakoma mwaka huu wanakaba mpk senti ya mwisho:shetani:
 
Dowans kosa lao ni nini?

Wanaokunyonga ni wale walioshinikiza mkataba na Dowans uvunjwe. Jee, ni kina nani?

Dowans wametimiza masharti ya Mkataba na ndio maana Mahakama yakimataifa ikaona kuwa wanastahiki kulipwa. Ingekuwa ni mahakama ya Tanzania, tungesema hakimu kahongwa.

Unajuwa kuwa Dowans waliileta ile mitambo tena kwa midege mikubwa ajabu ambayo kwa mara ya kwanza ilituwa Tanzania kuleta ile mitamabo? Na unajuwa kuwa ile mitambo waliyoleta ilijaribiwa hapo Ubungo na ikafanya kazi vizuri kabisa?

Sasa kama Dowans waliyafanya yote hayo, tena unajuwa kuwa dowans waliyafanya yote hayo bila kulipwa chochote? Ni ahadi tu zilitolewa!

Kama wafanya biashara walifanya yote hayo, kwanini leo Tanesco uamuwe kuvunja mkataba? Si kujitafutia matatizo.

Na hawa dowans mlitaka wakae kimya baada ya wao kuingia gharama zote hizo na kucunjiwa mkataba? Hizo gharama za kununuwa au kukodisha au kukopa hiyo mitambo, kuisafirisha, kuifunga, kuijaribu, zooote hizo ni waziachie?

Nadhani wengi wenu humu mnafata mkumbo bila ya kupima na kupitia kwa kina kujuwa tatizo limeanza vipi.
 

u r absolutely right, walioshinikiza mkataba uvunjwe walijua kuwa lazima tanesco/serikali ikishitakiwa itashindwa, cha kushanhgaza zaidi wote ni wanasheria waliobobea: mh sita na mwakyembe. Naikumbuka kauli ya mwakyembe bungeni juu mkataba wa dowans: kuliko kununua mitambo ya dowans bora nchi iwe gizani. Sasa nchi iko gizani na walalahoi wanakamuliwa kulipa deni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…