Down memory lane...

Hizo picha ungezitolea Maelezo
 
Kuna watu wakiona umepandisha uzi, basi matumbo yanawakata utafikiri wamewekewa nyembe tumboni!!
 
Mwana,
Hapana sijaandika uongo.

Hapo ninapozungumzia FM Stations ni mwaka wa 1991 nikieleza kifo cha
Mohamed Abdulwahab.
Nashangaa huyo anayesema 1985 hatukuwa na FM stations nchini, sijui alikuwa pande ipi ya nchi!
 
Msimamo wangu Kuhusu wazee wetu wapigania uhuru wote walifanya kazi kubwa
Wewe una weakness moja ya kudhani wazee wakiislam waliplay role kubwa Kuliko wale ambao hawakuwa waislam Hii si kweli kabisa

Ahsante mkuu
Mikocheni,,,
Tatizo lako ni kuwa wewe huijui historia ya TANU.

Sikulaumu hauko peke yako wewe ni moja wa kundi kubwa sana wa wasiojua.

Mimi ''sidhanii'' katika historia hii nimefanya utafiti na nimeandika kwanza kitabu
na nina ''paper,'' nyingi nimeandika kuhusu somo hili kiasi nimeshirikishwa katika
miradi miwili ya kuhifadhi historia hii.

Nimeshiriki katika mradi wa Oxford University Press, Nairobi na wamechapa kitabu
nilichoandika, ''The Torch on Kilimanjaro,'' (2007).



Nimeshiriki katika mradi wa Dictionary of African Dictionary (DAB) uliokuwa chini
ya Havard na Oxford University Press, New York (2011).

Kitabu cha Sykes kimepitiwa na wanahistoria maarufu wanaoijua historia ya Tanzania
kama John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan.

Ukimtoa Iliffe hao wawili waliobakia tunafahamiana kwa miaka na kilichotukutanisha
ni historia hii.

Ningeweza kuendelea zaidi.

Lakini kubwa katika waasisi wa African Association (1929) aliyeandika historia hiyo ni
Kleist Sykes na walikuwa watu 9 hakuna aliyeandika historia hiii na moja ya sababu
ni kuwa michango yao haikuwa mikubwa sana na haikudumu kwa muda mrefu hivyo
hawakuwa na mengi ya kuandika.

Katika waasisi 17 wa TANU (1954) hakuna aliyeweza kuandika historia yake ukimtoa
Abdul Sykes na yeye aliweza kufanya hili kwa kuwa alikuwa anaijua historia yote na
alikuwa na nyaraka.

Jambo la kusikitisha ni kuwa historia hii Abdul hakumaliza kuindika kwa sababu
palizuka sintofahamu kama hizi tunazojadili hapa hivi sasa.

Wewe huijui historia hii lakini hutaki kuwasikiliza wenye kuijua.

Hivi tunavyojadili, kutokana na kitabu cha Sykes Prof. Shivji na wenzake wanaandika
kitabu cha maisha ya Mwalimu Nyerere nia ikiwa pamoja na mengine, kujua nini
ulikuwa mchango wake katika kuunda TANU.

Naamini unauona mnyororo huo wa TANU kuanzia kwa Kleist Sykes hadi kwa
wanae Abdul na Ally katika historia hii.

Ikiwa ipo historia ya TANU isiyo kuwa hii hadi hivi sasa kitabu kipo mwaka wa 20
bado hakijaandikwa.
 
Mwafrika anaamini kuna mzungu huko uzunguni anaijua historia yake yeye mwafrika kuliko yeye mwenyewe


Sisi tuna matatizo wacha iendelee kubaki mzungu ndio aligundua Mlima Kilimanjaro, ziwa Victoria nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…