Sheria kwa Kiswahili
Senior Member
- Mar 30, 2018
- 116
- 106
Kifungu hiki hakiwezi kitumika katika nchi zetu ambazo zinaua kirejereja...Wakati mwingine tumechanganya makosa yanayoshitakika ICC tukidhani ICC inashughulikia makosa yote. tumetengeneza tafsiri hii kwa ajili ya raia wa kawaida kabisa, ili watu tukisome na kujiepusha na yale yanayoweza kutufanya tuishie ICC au kusumbuliwa nayo.
sijakuelewa, unauliza swali au unakosoa kipengele hicho?Kifungu hiki hakiwezi kitumika katika nchi zetu ambazo zinaua kirejereja...
Mfano ni Rais wa zamani wa Sudan, Rais Al Bashir alituhumiwa kutenda makosa nchini kwake Sudani, na Sudani sio mwanachama wa Mahakama ya ICC; hakuna nchi yeyote iliyokuwa na uwezo kisheria kulipeleka suala hilo ICC, wala Mwendesha mashitaka kisheria hakuruhusiwa kuanzisha mchakato yeye mwenyewe, hadi pale Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipotoa Azimio la kupeleka maombi ICC ndipo mchakato wa kutoa hati ya kumkamata ulianza. Kama Balaza la Usalama lisingefanya hivyo hakuna chombo kingine kisheria ambacho kingeisukuma ICC kuanzisha mchakato dhidi ya Rais Omar Al Bashir.
Nauliza, maana huku say Tz wanasema kama nchi siyo mwanachama hawezi kushitakiwa, hivyo bado kuna mwanya wa kumshitaki rais anayefanya mauaji.....sijakuelewa, unauliza swali au unakosoa kipengele hicho?
Dah, kaka kitabu hiki ni kizuri. huo ukurasa wa 32 na 33 kuna madini fulani hapo ya kuteka watu na kunyanyasa watu na kufunga watu bila sababu, safi sana mwandishi. nilishawahi kukuona mahakama ya Tunduma kumbe umesoma kufika mbali hivyo...safi sana!Wakati mwingine tumechanganya makosa yanayoshitakika ICC tukidhani ICC inashughulikia makosa yote. tumetengeneza tafsiri hii kwa ajili ya raia wa kawaida kabisa, ili watu tukisome na kujiepusha na yale yanayoweza kutufanya tuishie ICC au kusumbuliwa nayo.