DP World ni mwanzo tu, mengi yatafuata

DP World ni mwanzo tu, mengi yatafuata

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Tanzania hii si ile. Watanzania hawa si wale. Wakati wetu (tukiwa kwenye kutumikia Serikali na chama), ilikuwa rahisi kama kula bisi kuwaaminisha watanzania juu ya jambo fulani.

Ilikuwa rahisi kuwaambia Tanzania kuwa jezi za Simba ni za njano na za Yanga ni nyekundu. Na waliamini. Propaganda zilitamalaki.

Kulikuwa na sababu. Wengi wetu hawakuwa na elimu na utambuzi. Elimu ya darasani na hata ile ya mtaani iliwafikia watu wachache sana.

Wengi walikuwa mbumbumbu wa kielimu na kiutambuzi. Walikuwa na macho lakini hawakuwa wanaona. Walikuwa na masikio lakini hawakuwa wanasikia. Watanzania wa sasa, wanaona na wanasikia.

Kitendo cha watanzania wa kila aina kujitokeza na kupinga kwa namna mbalimbali Mkataba wa DP World wa kukodishwa Bandari zetu za Tanzania Bara si cha bahati mbaya.

Ni kwakuwa muda umefika. Watanzania wamefikia kwenye ukomavu wa kifikra; kimbinu na kiutendaji. Watanzania hawa hawayumbishwi na hawatishwi.

Watanzania wa aina hiyo wapo kila mahali: kwenye Serikali; chamani; kwenye wasomi; kwenye vyombo vya ulinzi na usalama; mitaani; mitandaoni; mijini na vijijini.

Amini nawaambia, hakutafichwa chochote chenye ukakasi na viongozi wetu kisiwekwe hadharani na watanzania hawa. Hata mikataba itakayofuata kuihusu Bandari yetu au popote pale, itaanikwa kama itapangwa kufichwa.

DP World imeonesha sura halisi ya watanzania wa sasa. Imeonesha jinsi watanzania wanavyoweza kupinga, kukosoa, kuongea, kujiamini, na kutobabaishwa na vitisho au propaganda.

Viongozi wetu wa Serikali na CCM wanapaswa kutishwa kuliko kawaida. Watishwe zaidi na jinsi watanzania wanavyopuuza mikutano ya viongozi wa CCM wanaozunguka nchini kuaminisha wananchi kuwa Mkataba wa Bandari ni mzuri.

DP World ni mwanzo tu, mengi yatafuata. Wa kujifunza na ajifunze sasa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mbeya)
 
Kwa mara ya kwanza maishani mwangu, ndio nimeona serikali ikibanwa kwenye jambo na wananchi wake mpaka inakosa majibu, serikali imebaki uchi haina la kusema, kwasababu kila aina ya jibu la uongo walilojaribu kuja nalo, limekataliwa na watanganyika.

Serikali ya aina hii ni dhalimu, haina mamlaka tena ya kutawala, kwasababu haiaminiki, kwa kushindwa kwake kutoa majibu yanayoeleweka kwenye jambo nyeti kama la bandari, itoshe tu kusema tunaongozwa na serikali dhaifu, isiyo na muelekeo, iliyo chini ya mtawala msaliti.
 
Sisi watu wa maombi tuzidishe Tu maombi yetu najua MUNGU aonae sirini atafunua yote
 
itendo cha watanzania wa kila aina kujitokeza na kupinga kwa namna mbalimbali Mkataba wa DP World wa kukodishwa Bandari zetu za Tanzania Bara si cha bahati mbaya.
ccm inajua kucheza na akili za Wa Tz hasa hawa wenye elimu duni na wafuasi wa ccm.
Hawana mbele wala nyuma, lkn hawataki kuamka ktk usingizi wa pono!
Wanaibiwa lkn hata habari hawana!
Ni maombamba lkn hawataki kujua umaskini wao ni shauri ya ccm!
 
Tanzania hii si ile. Watanzania hawa si wale. Wakati wetu (tukiwa kwenye kutumikia Serikali na chama), ilikuwa rahisi kama kula bisi kuwaaminisha watanzania juu ya jambo fulani.

Ilikuwa rahisi kuwaambia Tanzania kuwa jezi za Simba ni za njano na za Yanga ni nyekundu. Na waliamini. Propaganda zilitamalaki.

Kulikuwa na sababu. Wengi wetu hawakuwa na elimu na utambuzi. Elimu ya darasani na hata ile ya mtaani iliwafikia watu wachache sana.

Wengi walikuwa mbumbumbu wa kielimu na kiutambuzi. Walikuwa na macho lakini hawakuwa wanaona. Walikuwa na masikio lakini hawakuwa wanasikia. Watanzania wa sasa, wanaona na wanasikia.

Kitendo cha watanzania wa kila aina kujitokeza na kupinga kwa namna mbalimbali Mkataba wa DP World wa kukodishwa Bandari zetu za Tanzania Bara si cha bahati mbaya.

Ni kwakuwa muda umefika. Watanzania wamefikia kwenye ukomavu wa kifikra; kimbinu na kiutendaji. Watanzania hawa hawayumbishwi na hawatishwi.

Watanzania wa aina hiyo wapo kila mahali: kwenye Serikali; chamani; kwenye wasomi; kwenye vyombo vya ulinzi na usalama; mitaani; mitandaoni; mijini na vijijini.

Amini nawaambia, hakutafichwa chochote chenye ukakasi na viongozi wetu kisiwekwe hadharani na watanzania hawa. Hata mikataba itakayofuata kuihusu Bandari yetu au popote pale, itaanikwa kama itapangwa kufichwa.

DP World imeonesha sura halisi ya watanzania wa sasa. Imeonesha jinsi watanzania wanavyoweza kupinga, kukosoa, kuongea, kujiamini, na kutobabaishwa na vitisho au propaganda.

Viongozi wetu wa Serikali na CCM wanapaswa kutishwa kuliko kawaida. Watishwe zaidi na jinsi watanzania wanavyopuuza mikutano ya viongozi wa CCM wanaozunguka nchini kuaminisha wananchi kuwa Mkataba wa Bandari ni mzuri.

DP World ni mwanzo tu, mengi yatafuata. Wa kujifunza na ajifunze sasa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mbeya)
Magufuli naye alitoa mchango mkubwa katika kuwafanya watanzania kuwa wajuaji zaidi.
 
Tanzania hii si ile. Watanzania hawa si wale. Wakati wetu (tukiwa kwenye kutumikia Serikali na chama), ilikuwa rahisi kama kula bisi kuwaaminisha watanzania juu ya jambo fulani.

Ilikuwa rahisi kuwaambia Tanzania kuwa jezi za Simba ni za njano na za Yanga ni nyekundu. Na waliamini. Propaganda zilitamalaki.

Kulikuwa na sababu. Wengi wetu hawakuwa na elimu na utambuzi. Elimu ya darasani na hata ile ya mtaani iliwafikia watu wachache sana.

Wengi walikuwa mbumbumbu wa kielimu na kiutambuzi. Walikuwa na macho lakini hawakuwa wanaona. Walikuwa na masikio lakini hawakuwa wanasikia. Watanzania wa sasa, wanaona na wanasikia.

Kitendo cha watanzania wa kila aina kujitokeza na kupinga kwa namna mbalimbali Mkataba wa DP World wa kukodishwa Bandari zetu za Tanzania Bara si cha bahati mbaya.

Ni kwakuwa muda umefika. Watanzania wamefikia kwenye ukomavu wa kifikra; kimbinu na kiutendaji. Watanzania hawa hawayumbishwi na hawatishwi.

Watanzania wa aina hiyo wapo kila mahali: kwenye Serikali; chamani; kwenye wasomi; kwenye vyombo vya ulinzi na usalama; mitaani; mitandaoni; mijini na vijijini.

Amini nawaambia, hakutafichwa chochote chenye ukakasi na viongozi wetu kisiwekwe hadharani na watanzania hawa. Hata mikataba itakayofuata kuihusu Bandari yetu au popote pale, itaanikwa kama itapangwa kufichwa.

DP World imeonesha sura halisi ya watanzania wa sasa. Imeonesha jinsi watanzania wanavyoweza kupinga, kukosoa, kuongea, kujiamini, na kutobabaishwa na vitisho au propaganda.

Viongozi wetu wa Serikali na CCM wanapaswa kutishwa kuliko kawaida. Watishwe zaidi na jinsi watanzania wanavyopuuza mikutano ya viongozi wa CCM wanaozunguka nchini kuaminisha wananchi kuwa Mkataba wa Bandari ni mzuri.

DP World ni mwanzo tu, mengi yatafuata. Wa kujifunza na ajifunze sasa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Mbeya)
Mola ikikupendeza chukua na hawa washirika wa diipiiwelid.
 
Back
Top Bottom