DPP hana nia ya kumshitaki: Naomba kujuzwa kuhusu DPP na majukumu yake inaelekea ni mtu mwema sana

DPP hana nia ya kumshitaki: Naomba kujuzwa kuhusu DPP na majukumu yake inaelekea ni mtu mwema sana

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Waungwana na wajuvi habari zenu:
Naomba kufahamishwa nijue;
  1. Je; DPP anaweza kufuta/ au kuondoa kesi hata pale baada ya mashahidi wake wote kutoa ushadi na ikathibitika kuna kesi ya kujibu?
  2. Anaposema hana nia ya kumshitaki mhalifu huwa ni maoni yake mwenyewe au ni sheria?
  3. DPP anakuwa kaendesha kesi na baadae kufuta au kuiondoa huwa kuna fidia yoyote kwa mtuhumiwa aliyekuwa ameshikiliwa kwa mashitaka?
  4. DPP anatumia chombo gani kuchunguza hadi anapofikia hatua ya kutokuwa na nia ya kushtaki wakati tayali polisi huwa wameshakusanya vielelezo na kukamta?
  5. Je; Serikali haioni kwamba ni wakati sasa iweke ukomo wa mda kwa DPP kufuta kesi iliyonguliwa, (mfano, siku 60 baada ya kusomwa kesi, DPP asiruhusiwe kufuta kesi hadi ikamilike, vinginevyo itafsirike jamhuli Imeshindwa?
Nashawishika kujua zaidi kuhusu DPP inaelekea ni mtu mwema sana anaweza kufuta kesi zote!

Hata kumwachia mtu yoyote na asihojiwe wakati wowote hata kama iwe ni kesi ya Mauaji, Uamsho au Escrow!!!
 
Tatizo anakuwa na roho ya huruma ndani yake iliyoambatana na harufu 10% ndio maana huwa anakosa nia yabkushtaki
 
= mhalifu

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?

Niliwahi kutomwelewa mwalimu wangu enzi hizo pale alipoingia darasani na kudai kuwa darasa lote tulikuwa ni wajinga na vichaa, siku hizi ndio naanza kumwelewa!
 
ni mtu mmoja au jopo la mahakimu? taaluma yake ni nini
DPP ni mtu mmoja, Mkurugenzi wa mashitaka na Ofisi yake ni moja Idara nyeti za Serikali. Cheo chake ni cha Kikatiba. Ofisi yake ina matawi mikoa yote na ana waendesha mashitaka (PP) wengi tu.

Kwa kiasi kikubwa anasaidiwa na polisi hasa upande wa upelelezi na uchunguzi. Maafisa wake wengi ni wanasheria, hivyo uhusika zaidi kuandaa mashitaka na kusimamia kesi.

Sheria umempa DPP mamlaka makubwa sana. Anatakiwa kuwa mtu mwenye integrity na weledi wa kiwango cha juu.

Kesi hata za rushwa nyingi haziwezi kwenda mahakamani bila idhini yake na anayo Mamlaka kisheria kuondoa shitaka lolote mahakamani km halijamalizika kusikilizwa hata km si yeye amelipeleka mahakamani.

Kidogo wanasheria wataweka vizuri zaidi kwa vifungu na sheria zaidi ya Katiba zinazompa mamlaka DPP.
 
DPP ni mtu mmoja, Mkurugenzi wa mashitaka na Ofisi yake ni moja Idara nyeti za Serikali. Cheo chake ni cha Kikatiba. Ofisi yake ina matawi mikoa yote na ana waendesha mashitaka (PP) wengi tu.

Kwa kiasi kikubwa anasaidiwa na polisi hasa upande wa upelelezi na uchunguzi. Maafisa wake wengi ni wanasheria, hivyo uhusika zaidi kuandaa mashitaka na kusimamia kesi.

Sheria umempa DPP mamlaka makubwa sana. Anatakiwa kuwa mtu mwenye integrity na weledi wa kiwango cha juu.

Kesi hata za rushwa nyingi haziwezi kwenda mahakamani bila idhini yake na anayo Mamlaka kisheria kuondoa shitaka lolote mahakamani km halijamalizika kusikilizwa hata km si yeye amelipeleka mahakamani.

Kidogo wanasheria wataweka vizuri zaidi kwa vifungu na sheria zaidi ya Katiba zinazompa mamlaka DPP.
Anaposema hana nia ya kumshitaki mhalifu huwa anatumia sheria au busara?
 
Hii loophole huwa siielewi.

Eti hana nia ya kuendelea na kesi.

Wala hana haja ya kujustify maamuzi yake. Na anakuwa appointed na rais.
 
Niliwahi kutomwelewa mwalimu wangu enzi hizo pale alipoingia darasani na kudai kuwa darasa lote tulikuwa ni wajinga na vichaa, siku hizi ndio naanza kumwelewa!
🙄 😳
 
Hii loophole huwa siielewi.

Eti hana nia ya kuendelea na kesi.

Wala hana haja ya kujustify maamuzi yake. Na anakuwa appointed na rais.
ndiyo maana nataka mtu atuçhambulie lakini watu ndo vile mambo kama haya wengi hawayajui
 
Hii loophole huwa siielewi.

Eti hana nia ya kuendelea na kesi.

Wala hana haja ya kujustify maamuzi yake. Na anakuwa appointed na rais.
Ndo hata mm sielewi je maumivu ya mshitakiwa hufidiwaje?
 
1: DPP anaweza kuondoka kesi wakati wowote kabla ya hukumu kwa sharti kwamba endapo ataondoa kabla mtuhumiwa hajajitetea anaweza irudisha kesi tena Kwa same grounds lkn endapo Mtuhumiwa atakua kashajitetea basi hawezi tena kuturudisha kesi hiyo mahakamani

2: Anaposema hana nia ya kuendelea na kesi ni maoni yake anayoyatoa Kwa mujibu wa sheria,so yana nguvu ya ya kisheria (sect 91 CPA Cap 20 RE 2019)

3: Kuna mazingira ambayo mshtakiwa huwezi kushtaki kuomba fidia ya kushtakiwa kiuonevu (Malicious Prosecution) na kuna mengine hawezi.Hii ni endapo upande wa mashtaka ulishindwa uestablish prima facie case.Kwa kesi ya Mbowe upande wa mashtaka uliestablish kesi ya kujibu hvyo hakuna malicious prosecution.

4: DPP ndiye kiongozi wa upelelezi so Polisi wanapeleleza chini ya maelekezo ya DPP hivyo akifanya maamuzi anayafanya akizingatia uzito wa upelelezi ulofanyika katika viwango vya kuthibitisha kosa.

5: Kuna ukomo wa upelelezi ambao ukifika inabidi iombwe ruhusa kuongeza muda lkn ukomo wa DPP kuondoa kesi ni muda wowote kabla ya hukumu.
 
Waungwana na wajuvi habari zenu:
Naomba kufahamishwa nijue;
  1. Je; DPP anaweza kufuta/ au kuondoa kesi hata pale baada ya mashahidi wake wote kutoa ushadi na ikathibitika kuna kesi ya kujibu?
  2. Anaposema hana nia ya kumshitaki mhalifu huwa ni maoni yake mwenyewe au ni sheria?
  3. DPP anakuwa kaendesha kesi na baadae kufuta au kuiondoa huwa kuna fidia yoyote kwa mtuhumiwa aliyekuwa ameshikiliwa kwa mashitaka?
  4. DPP anatumia chombo gani kuchunguza hadi anapofikia hatua ya kutokuwa na nia ya kushtaki wakati tayali polisi huwa wameshakusanya vielelezo na kukamta?
  5. Je; Serikali haioni kwamba ni wakati sasa iweke ukomo wa mda kwa DPP kufuta kesi iliyonguliwa, (mfano, siku 60 baada ya kusomwa kesi, DPP asiruhusiwe kufuta kesi hadi ikamilike, vinginevyo itafsirike jamhuli Imeshindwa?
Nashawishika kujua zaidi kuhusu DPP inaelekea ni mtu mwema sana anaweza kufuta kesi zote!

Hata kumwachia mtu yoyote na asihojiwe wakati wowote hata kama iwe ni kesi ya Mauaji, Uamsho au Escrow!!!
1) Kesi inapofika mahakamani, dpp anachotoa ni ushauri tu kwa Hakimu (Judge). Judge ndie mwenye maamuzi.

2) Ni Sheria, DPP yupo pale kisheria akitimiza majukumu yake. Rudi namba moja juu hapo.

3) Inategemea na mtuhumiwa, kama atafungua kesi kudai au kutokudai fidia.

4) Anatumia chombo chake kinachompa mamlaka ya kutumia vyombo vingine vya Serikali kupata akitakacho kisheria.

5) Sheria zipo na hubadilishwa mara kwa mara na Wabunge, bungeni, serikali haiwezi kubadili sheria, inachoweza kufanya ni kuupeleka Mswada bungeni na wabunge wanaujadili kwa maslahi mapana ya taifa na kupitisha sheria stahiki.

DPP hayuko pale kutenda mema au dhambi, yupo pale kufanya kazi zake kwa kufata sheria zinazomuongoza. Akifaya mema nje ya sheria atakuwa na makosa na akifanya dhambi nje ya sheria atakuwa anafanya kosa.


Mwisho wa siku elewa tu, sheria za Kibinaadam hazitaacha kuwa na matundu (loopholes). Turudi kwennye Sharia Ya Allah (aka Qur'an), ambayo haina makosa na haibadiliki.
 
1) Kesi inapofika mahakamani, dpp anachotoa ni ushauri tu kwa Hakimu (Judge). Judge ndie mwenye maamuzi.

2) Ni Sheria, DPP yupo pale kisheria akitimiza majukumu yake. Rudi namba moja juu hapo.

3) Inategemea na mtuhumiwa kama atfungua kesi kudai au kuto kudai fidia.

4) Anatumia chombo chake kinachompa mamlaka ya kutumia vyombo vingine vya Serikali kupata akitakacho kisheria.

5) Sheria zipo na hubadilishwa mara kwa mara na Wabunge, bungeni, serikali haiwezi kubadili sheria, inachoweza kufanya ni kuupeleka Mswada bungeni na wabunge wanaujadili kwa maslahi mapana ya taifa na kupitisha sheria stahiki.

DPP hayuko pale kutenda mema au dhambi, yupo pale kufanya kazi zake kwa kufata sheria zinazomuongoza. Akifaya mema nje ya sheria atakuwa na makosa na akifanya dhambi nje ya sheria atakuwa anafanya kosa.


Mwisho wa siku elewa tu, sheria za Kibinaadam hazitaacha kuwa na matundu (loopholes). Turudi kwennye Sharia Ya Allah (aka Qur'an), ambayo haina makosa na haibadiliki.
Asante mdau
 
Back
Top Bottom