Dr. A.Meru(EPZA):Kubadilisha Majina ya kampuni hakuambatani na ukwepaji kodi

Dr. A.Meru(EPZA):Kubadilisha Majina ya kampuni hakuambatani na ukwepaji kodi

TUJITEGEMEE

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2010
Posts
25,225
Reaction score
25,488
Dr. A. Meru, Mkurugenzi mkuu wa Export Processing Zone Authority (EPZA), amesema utaratibu unaotumiwa na makampuni kubadilisha majina: mfano Sheraton kuwa MovenPick, Airtel kuwa Zain, Mobitel kuwa Tigo, n.k., hauambatani na ukwepaji wa kulipa kodi. Amesema ukwepaji huo wa kodi haupo kwani mkataba unausisha mradi (project) wala sio jina la kampuni. Pia alisema utaratibu wa kubadilisha majina ni wa kawaida kwa makampuni mengi duniani wala hili halifanyiki Tanzania tu. Aliongeza kuwa EPZA inatoa likizo ya kutolipa kodi (tax holiday) ya miaka kumi. Muda huo ukiisha lazima kampuni ilipe kodi bila kujali ilibadilisha jina ama la.

Dr. Meru aliyasema haya wakati wa Mhadhara wa wazi kwa Umma (Public Lecture) uliondaliwa na Engineers Registration Board (ERB) na kufanyika Luther House (Dar-es-Salaam) jana huku yeye akiwa mzungumzaji mkuu.

Source: ERB


WanaJF mnasemaji kuhusu maelezo haya ya Mkurugenzi mkuu wa EPZA?
 
Kama amesoma MBA mwambieni aka review upya topic inayoitwa TRANSFER PRICING! aone huo ujinga anao utetea wa TAX HOLIDAY ya miaka 10! labda watu wanaiogopa hiyo PHD yake! Unaweza kuwa PHD holder bado ukawa kiazi wa kutoa mawazo kama Dr Benson Bana wa UDSM!!!!:shut-mouth:
 
Kama amesoma MBA mwambieni aka review upya topic inayoitwa TRANSFER PRICING! aone huo ujinga anao utetea wa TAX HOLIDAY ya miaka 10! labda watu wanaiogopa hiyo PHD yake! Unaweza kuwa PHD holder bado ukawa kiazi wa kutoa mawazo kama Dr Benson Bana wa UDSM!!!!:shut-mouth:

Professionally ni Mechanical Engineer.
 
viongozi wa namna hii
ni mzigo kwa walipakodi
ni vema tukatoa mawazo kwenye katiba
mpya bunge lipewe meno
baada ya kiongozi wa shirika la uma pamoja na Mkuu wa jeshi la polisi, magereza na uhamiaji

majina yao yapelekwe bungeni, yajadiliwa na ikionekana aanafaa ndio aidhinishwe kuwa MD

hii itasaidia saana kuwawajibisha hawa ma MB mbumbumbu

angekuwa china angepewa zawadi ya kunyongwa
 
Akitetea uwamuzi wa EPZA kutoa tax holiday ya miaka kumi kwa kampuni zinazotaka kuwekeza katika SEZ(special economic zone) na EPZ(expert Processing zone) alisema miaka 10 wanaanza kuihesabu pale tu kampuni inapopewa leseni wakati kampuni hiyo kabla hajaijapata eneo la kufanyia kazi, kujenga kiwanda n.k.

Alongeza kuwa ni vigumu kwa kampuni kuanza kupata faida (Break Even) ndani ya muda huo kwa maeneo hayo ya SEZ na EPZ.

Kwa maelezo zaidi namna scheme za EPZ na SEZ zinavyofanya kazi soma hapa>>>http://www.epza.co.tz/About-EPZ-Program.html
 
Kama amesoma MBA mwambieni aka review upya topic inayoitwa TRANSFER PRICING! aone huo ujinga anao utetea wa TAX HOLIDAY ya miaka 10! labda watu wanaiogopa hiyo PHD yake! Unaweza kuwa PHD holder bado ukawa kiazi wa kutoa mawazo kama Dr Benson Bana wa UDSM!!!!:shut-mouth:

Asante mkuu na mm ngoja niitafute hiyo topic TRANSFER PRICING je itakuwa kwenye Accounting or Corporate Finance ?
 
Kama amesoma MBA mwambieni aka review upya topic inayoitwa TRANSFER PRICING! aone huo ujinga anao utetea wa TAX HOLIDAY ya miaka 10! labda watu wanaiogopa hiyo PHD yake! Unaweza kuwa PHD holder bado ukawa kiazi wa kutoa mawazo kama Dr Benson Bana wa UDSM!!!!:shut-mouth:

Mkuu tayari nimejaribu kupitia TRANSFER PRICING naona kama inahusika Product Transfer Pricing Policy/methodology In Multinational Corporation among branches na sio Ownership Transfering Labda utusaidie kuelewa mahusino yake na tax in transfering ownership ? kwa nia nzuri na sisi tuelewe
 
Back
Top Bottom