and 300
JF-Expert Member
- Jun 27, 2012
- 26,398
- 36,406
Dr. Aldin Mutembei alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Taaluma ya Kiswahili (TATAKI), University of Dar es Salaam, amevuliwa madaraka ya Ukurugenzi wa TATAKi kufuatiwa tuhuma za Ubadhirifu wa Pesa za Taasisi na pia kuleta dharau kwa wafanyakazi wa TATAKI hususani wale wastaafu wanaofanya kazi kwa Mikataba. Kwa hili la Uongozi wa UDSM kumnyang'anya madaraka Dr. Mutembei mnastahili pongezi hususan Prof. Mukandala, maana usingechukua hatua watu wangesema unamlinda Mhaya mwenzio (Dr. Mutembei) na iwe somo kwa Mutembei kuwa kwa kuwa na Boss wa kabila lako sio ndo ufanye lolote unalotaka. Kaa benchi kwa kwanza ujifunze jinsi ya kuwa mwadilifu na kuishi na watu vizuri.