Dr Hosea, Feleshi targeted



Zalendohalisi, nimekupata mkuu. Ila tu kwa kifupi don Hosea ile taasisi siyo right kwake. Aondoke. Yeye anaitumikia state na si jamii. Tunahitaji mtu mwenye kujali maslahi ya wananchi na si vimemo.
 

Tatizo ni SOURCE: IPP media mmmh
 
Zalendohalisi, nimekupata mkuu. Ila tu kwa kifupi don Hosea ile taasisi siyo right kwake. Aondoke. Yeye anaitumikia state na si jamii. Tunahitaji mtu mwenye kujali maslahi ya wananchi na si vimemo.

Mkuu Maane samahani kwanza ndugu yangu; Hivi una maana gani unaposema kuwa "Yeye anaitumikia state na si jamii.". Una maana kuwa PCCB ni chombo cha wananchi? PCCB siyo chombo cha jamii.

La pili linalonikera ni pale watanzania tunapoweka matumaini ya ufanisi wa institutions zetu sambamba na yule anayeiongoza hiyo institution, na wala siyo kwenye misingi iliyoiweka hizo institutions. Pia viongozi wa hizo istitutions wamapochaguliwa linalopewa kipaumbele ni "uwenzetu" au "umwana matandao" na siyo uwezo na integrity inayoambatana na hiyo nafasi. Ndiyo maana JK anachemsha kila kukicha e.g hili la kumweka Mataka aliyeshindwa kuiendesha ATC sasa ndiyo "brain" wa kui-restructure NIC, utadhani nchi hii haina intellectuals apart from those around JK.

Let's say Hosea anondoka leo, je vita vya dhidi ya rushwa vitabadilika just because you have another face who takes orders from the same source? - I don't think so. What might change is the perception towards the head of the institution leadership lakini siyo tabia za ulaji rushwa na ufisadi uliojikita kwenye jamii ya kitanzania.

PCCB siyo chombo cha wananchi and I repeat PCCB siyo chombo cha wananchi ama sivyo kingekuwa chini ya wananchi (Parliament). PCCB ni chombo cha excutive branch chini ya CEO wake JK! Na nikujidanganya bure kuwa PCCB ni chombo cha wananchi. Tatitizo ni kuwa watanzania tumefika mahali hata ukweli ulio wazi hatuuoni wala kuuelewa in its real terms. Hosea of PCCB reports to the president period; Othman wa TISS reports to the president and those two instituions will ALWAYS play by the rules laid down not by consitution but as intepreted by the excutive branch. That's the truth and its hard to swallow BUT it's the reality.

Wewe unadhani Hosea ana ubavu wa kumpeleleka Yona au Mramba Kisutu? Subutu! lazima JK aliulizwa kwanza na hata hayo mafaili mengine yanayozungumziwa kukaliwa na Hosea I bet yanasubiri approval za JK. Hosea ataondoka tukidhani huyo mwingine atakuwa na ubavu, lakini ni staili na approach labda itakuwa tofauti ILA ukweli utabakia palepale kuwa the head of state ndiye mwenye duka lenye nembo PCCB.

ZalendoHalisi
 

Umemaliza Mkuu Zalendohalisi. Sidhani kama kuna ulichokiacha hapo.

Matatizo ya nchi yetu ni Katiba yetu. Period.

Katiba inatoa mamlaka makubwa kwa Rais. Nae akiwa kichwa ngumu, anaua nchi. Mifano michache uliyoitoa hapo juu Mkuu Zalendohalisi inatukumbusha ukweli huo vya kutosha kabisa.

Mimi nalilia Katiba yetu. Katiba yetu imetutoa katika utawala wa mkoloni (nadhani wenye nguvu walikuwa wengi zaidi kuliko sasa) na kutupeleka kwenye mikono ya mtu mmoja (ambae si lazima awe mwenzetu kwa kila kitu). Tanzania huru bado haijapatikana. Huo ndio ukweli. Nadhani kama tunaitakia mema nchi hii, ni lazima kuwe na Katiba yenye uwiano mzuri zaidi. Haiwezekani kumpa mtu madaraka yote kupitia taasisi mbalimbali anazoziongoza. Tena nyingi ya Taasisi hizo zina nguvu kubwa katika uhuru wetu na ustawi wetu wote.

Ndio maana huwa nasema hapa kuwa, haiwezekani mambo yote tunayoyapigia makelele yakafanyiwa kazi eti kwasababu tumepiga kelele. Haiwezekani. Yanayowezekana yote yatafanywa kwa ridhaa ya mtu mmoja tu (Rais wa Jamhuri ya Muungano).

Nchi hii ndugu zangu akitokea kiongozi mwendawazimu, anaweza kutumaliza wote kama anavyotaka (na, Katiba ikamruhusu)
 

Umemaliza Mkuu Zalendohalisi. Sidhani kama kuna ulichokiacha hapo.

Matatizo ya nchi yetu ni Katiba yetu. Period.

Katiba inatoa mamlaka makubwa kwa Rais. Nae akiwa kichwa ngumu, anaua nchi. Mifano michache uliyoitoa hapo juu Mkuu Zalendohalisi inatukumbusha ukweli huo vya kutosha kabisa.

Mimi nalilia Katiba yetu. Katiba yetu imetutoa katika utawala wa mkoloni (nadhani wenye nguvu walikuwa wengi zaidi kuliko sasa) na kutupeleka kwenye mikono ya mtu mmoja (ambae si lazima awe mwenzetu kwa kila kitu). Tanzania huru bado haijapatikana. Huo ndio ukweli. Nadhani kama tunaitakia mema nchi hii, ni lazima kuwe na Katiba yenye uwiano mzuri zaidi. Haiwezekani kumpa mtu madaraka yote kupitia taasisi mbalimbali anazoziongoza. Tena nyingi ya Taasisi hizo zina nguvu kubwa katika uhuru wetu na ustawi wetu wote.

Ndio maana huwa nasema hapa kuwa, haiwezekani mambo yote tunayoyapigia makelele yakafanyiwa kazi eti kwasababu tumepiga kelele. Haiwezekani. Yanayowezekana yote yatafanywa kwa ridhaa ya mtu mmoja tu (Rais wa Jamhuri ya Muungano).

Nchi hii ndugu zangu akitokea kiongozi mwendawazimu, anaweza kutumaliza wote kama anavyotaka (na, Katiba ikamruhusu)
 


..DG wa PCCB anaweza kuitunza familia yake Marekani bila kutumia mapato ya kifisadi?

..Gray Mgonja, retired PS wa Hazina anayeshtakiwa pamoja na Mramba, familia yake inaishi USA.

..pia kuna habari zinazagaa kwamba Dr.Benno Ndulu gavana wa BOT amenunua jumba la kifahari Marekani kwa ajili ya familia yake aliyoicha huko.

NB:

..labda hawa tuwaache wawashughulikie mafisadi wa awamu ya Mkapa.

..halafu wenyewe nao watashughulikiwa na serikali ya Membe -- atakayemrithi Kikwete.

..waliosema "kutesa kwa zamu" hawakukosea.
 
Zalendohalisi, nimekupata mkuu. Ila tu kwa kifupi don Hosea ile taasisi siyo right kwake. Aondoke. Yeye anaitumikia state na si jamii. Tunahitaji mtu mwenye kujali maslahi ya wananchi na si vimemo.

Kwani kaka hujui kwamba PCCB ni taasisi ya dola ten ipo chini ya waziri wa usalama wa taifa?

Naamini kuna haja ya kuendeleza mabadiliko ya kiasasi zaidi na zaidi ili hii taasisi iweze kutumikia jamii kama wengi tunavyopenda kuona
 
Huyu Hosea kwa nini hajiondoi? Kuwapo kwake kunaifanya vita nzima dhidi ya ufisadi kuwa kichekesho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…