Dr. Issack Maro wa njia panda aongelea fine ya kipindi chake

Dr. Issack Maro wa njia panda aongelea fine ya kipindi chake

Nukta5

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2014
Posts
1,182
Reaction score
1,288
Leo katika kipindi cha njia panda dr. Issack ameelezea fine waliyotozwa na TCRA kwamba kipindi kilitozwa fine kutokana na kwamba kilipotosha wasikilizaji kuhusu nguvu za kishirikina wakati wanamhoji Mussa kipindi kilichorushwa tarehe 15.

Pia Dr. alielezea kuhusu nia ya kipindi ni kufundisha, kuelimisha na kusaidia jamii yote kwa ujumla kuhusu matatizo wanayopitia watu kwa kuwahoji wahusika live.

Katika kuelezea kipindi cha njia panda ni kipindi cha kuelimisha na kusaidia watu Dr. Issack alisema hakuna kipindi kilichowahi kuwasaidia watu kama kipindi cha njia panda kwani kimeshawasomesha watu takribani 100 na pia kuwasaidia watu kwenye kesi zao hadi walipopata haki zao na akaendelea kusema kama mtu anabisha yupo tayari kumwandikia check alete ushahidi.
 
Yule jamaa nina shaka na udaktari wake mambo yanayoongelewa katika kipindi mengi ni ya kufikirika ila yeye huwaga anayasapoti kweli kama mwehu vile
 
Kwani kile kipindi kina tofauti gani na sinema? Kama wanaacha sinema ziendelee kutuburudisha basi ni ujinga kupiga faini sinema za redioni!
 
Hata mie nilijua, maana watu wanasema kuwa wanaiba na kupotea hivi mtu anaweza kupotea kabisa
 
TCRA nao wazushi tu.....ile faini ya uonevu ....issue zilizozungumziwa ndio mambo yaliyoko mtaani ......wanawaacha akina Kibonde na Hando kwa uchochezi kwavile hawaigusi CCM lakini wanajitutumua kwenye ujinga ....
 
Nakikubali sana hicho kipindi kwan toka enzi za Sebastian Ndege wamesaidia sana watu na kuelimisha kuhusu afya na masuala ya kijamii
 
teheee... mimi nilijua fine imetokana na bangi za XXL..
Kumbe ni huyoo??
 
tCRA ni watu wa ajabu sana kipindi kimesaidia jamii sana kile
 
Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni hakika mim ni moja yawatu walioanza kufuatilia njia panda tangu enzi za sebastian Hakika kipindi hki kimeifanyia makubwa sana watanzania wenye shida namatatzo mbalimbal kadri yauwezo wao hakika wengi hawaipendi clouds ila kuna ukwel ulio waz kuwa weng wamepta msaada..naomba tusiwe warahsi wakuhukumu ila tuangalie je mema yamezidi mabaya? kila b'damu ana mapungufu yake ila pale mtu anapojitahidi tumpongeza pia tukubali kuwa mwenzetu amefanya jambo kubwa. si ajabu wanaoping kuwa hakuna ushrikina ndo washrikina wakubwa stay in true clouds kwa kipindi cha njia panda hawana mpnzani wamefanikiwa mno...mungu mbariki dk issack maro.
 
Leo katika kipindi cha njia panda dr. Isack ameelezea fain waliyotozwa na TCRA kwamba kipindi kilitozwa fain kutokana na kwamba kilipotosha wasikilizaji kuhusu nguvu za kishirikina wakati wanamhoji Mussa kipindi kilichorushwa tareh 15

Pia Dr. alielezea kuhusu nia ya kipindi ni kufundisha, kuelimisha na kusaidia jamii yote kwa ujumla kuhusu matatizo wanayopitia watu kwa kuwahoji wahusika live .

Katika kuelezea kipindi cha njia panda ni kipindi cha kuelimisha na kusaidia watu Dr. Isack alisema hakuna kipindi kilichowahi kuwasaidia watu kama kipindi cha njia panda kwani kimeshawasomesha watu takribani 100 na pia kuwasaidia watu kwenye kesi zao hadi walipopata haki zao na akaendelea kusema kama mtu anabisha yupo tayari kumwandikia check alete ushahidi.

ID yako ni kiboko mkuu
 
Hao watu wa TCRA waliowatoza njia panda Fine itakua ni wachawi wa kuluka na ungo, imewauma siri zao kutoka nje wakaona wawakomee clouds kulipiza kisasi, sikuona ubaya wa kile kipindi ..dr isack kaza buti endelea kutuelimisha husikaktishwe tamaa na hao wachawi
 
Back
Top Bottom