Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,409
- 13,262
Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Dr. Joyce Ndalichako, Dr. Hussein Mwinyi, Dr. Mohamed Shein, Dr. Michael Kadeghe, Dr. Philemon Sarungi(Prof), Dr. Mgona sipakune Tulimumu, Dr. Maji marefu("Prof"), Dr. Hamis Kigwangala nk.
Hawa wote hapo juu wanaitwa na wengine kujiita madaktari. Hapo kuna madaktari walioteseka madarasani kusomea utabibu wa binadamu na wanyama, kuna waliobobea katika fani mbali mbali za kitaaluma lakini sio kutibu, kuna waliopewa udaktari wa heshima kutokana na utendaji wao au misimamo yao lakini hawajakanyaga darasani kuteseka na kitabu na kuna wanaojitwika udaktari.
Hoja yangu ni kuwa hivi hakuna namna ya kuwatofautisha madaktari hao wakati wa kuwataja ili mtu ajue anayetajwa ni daktari wa aina gani. Hivi mtu akiwataja Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Dr. Hamis Kigwangala na Dr. Joyce Ndalichako mtu wa kawaida asiyejua historia zao kikazi au kielimu atawatofautishaje? Kuna rafiki yangu mmoja ni Dr. anayefundisha chuo kikuu alipokuja kunitembelea, na jirani yangu nilipomtambulisha kwake kama Dr. akawa anataka msaada wa ugonjwa wake unaomsumbua muda mrefu. Je hakuna namna ya kuiandika au kuitamka hii Dr. ikiwa na kitu cha kuonesha kuwa huyu kapewa, kasomea au kajipachika?? Tusaidiane maana nchi hii ina madaktari wachache na wengi feki lakini wajibebea heshima wasizostahili. Kuna vyuo vikuu pia vinapoona havivumi au ni vya kiwango cha chini huwa vinakuwa sharp kutoa udaktari wa heshima hasa kwa viongozi wakubwa ili vitambulike.
Kuna vyeo kama Mwalimu, padri, mchungani, ustaadhi, dereva, urubani, mhandisi nk mara nyingi huwa vinaelekezwa kwa watu wenye taaluma husika. Mfano mtu hawezi akaitwa dereva au rubani kwa heshima wakati hana taaluma hizo. Hivyo watu hao wakitajwa huwa hakuna tatizo kwani wanajulikana ni wataalamu wa fani hiyo. Kwenye udaktari naona kuna nipa shida! Utawatambuaje?
Hawa wote hapo juu wanaitwa na wengine kujiita madaktari. Hapo kuna madaktari walioteseka madarasani kusomea utabibu wa binadamu na wanyama, kuna waliobobea katika fani mbali mbali za kitaaluma lakini sio kutibu, kuna waliopewa udaktari wa heshima kutokana na utendaji wao au misimamo yao lakini hawajakanyaga darasani kuteseka na kitabu na kuna wanaojitwika udaktari.
Hoja yangu ni kuwa hivi hakuna namna ya kuwatofautisha madaktari hao wakati wa kuwataja ili mtu ajue anayetajwa ni daktari wa aina gani. Hivi mtu akiwataja Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Dr. Hamis Kigwangala na Dr. Joyce Ndalichako mtu wa kawaida asiyejua historia zao kikazi au kielimu atawatofautishaje? Kuna rafiki yangu mmoja ni Dr. anayefundisha chuo kikuu alipokuja kunitembelea, na jirani yangu nilipomtambulisha kwake kama Dr. akawa anataka msaada wa ugonjwa wake unaomsumbua muda mrefu. Je hakuna namna ya kuiandika au kuitamka hii Dr. ikiwa na kitu cha kuonesha kuwa huyu kapewa, kasomea au kajipachika?? Tusaidiane maana nchi hii ina madaktari wachache na wengi feki lakini wajibebea heshima wasizostahili. Kuna vyuo vikuu pia vinapoona havivumi au ni vya kiwango cha chini huwa vinakuwa sharp kutoa udaktari wa heshima hasa kwa viongozi wakubwa ili vitambulike.
Kuna vyeo kama Mwalimu, padri, mchungani, ustaadhi, dereva, urubani, mhandisi nk mara nyingi huwa vinaelekezwa kwa watu wenye taaluma husika. Mfano mtu hawezi akaitwa dereva au rubani kwa heshima wakati hana taaluma hizo. Hivyo watu hao wakitajwa huwa hakuna tatizo kwani wanajulikana ni wataalamu wa fani hiyo. Kwenye udaktari naona kuna nipa shida! Utawatambuaje?