Dr. Mwakyembe ataja viwanja vitatu AFCON 2019 kwa vijana chini ya miaka 17

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe ametaja viwanja vitakavyotumika katika mashindano ya vijana chini ya miaka 17 katika fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) mwakani.

Waziri Mwakyembe alisema Uwanja wa Taifa utatumika kwaajili ya ufunguzi na kufungukia mashindano hayo, huku viwanja vingine vya Uhuru na Azam Complex Chamazi vikitumika katika mechi za mashindano hayo.

"Tunataka tufanye mabadiliko katika hizi nyasi bandia za uhuru tuweke mpya, lakini uwanja wa Gymkhana utatumika kwa mazoezi, bado kuna viwanja vingine tunaendelea kuvichagua ili timu zipate sehemu ya kufanyia mazoezi kwa urahisi," alisema Mwakyembe.

Waziri Mwakyembe alisema wanajua wingi wa timu nane zinazokuja zitakuwa na viongozi, wachezaji na mashabiki hivyo wanajiandaa kuhakikisha wageni hao wanapata mahitaji yao mapema.

"Magari yanahitajika kwaajili ya kuwabeba wageni wetu hivyo inabidi yapatikane na kuandaliwa mapema, lakini pia tunajupanga juu ya suala la foleni wasiweze kukutana nalo,'' alisema.

Mwakyembe aliongeza kwamba wanaendelea na maandalizi, wapo katika hatua nzuri kwa ajili ya mashindano hayo.

Chanzo: Mwananchi
 
Viwanaja vingine ni kututia aibu tu
 
Huyu waziri mbona hana mvuto kabisa ?
 
Kiwanja kingine cha mazoezi wawa peleka pale Jangwani(Kaunda)
 
Mwakyembe toka awekwe kwenye hii wizara amekuwa mtu wa porojo mwanzo mwisho
 
Miaka 50 ya Uhuru nchi bado Ina uwanja mmoja tu mikoa yote ya tz ni dar tu ndio wawe na haki ya kupata mechi za kimataifa,tatizo la mwakyembe analeta siasa kwenye soka letu. Tanzania tutasubili sana.na sisi wa mikoani mkituonyesha kupitia luninga ,tutawashangilia wageni,msitulazimishe uzalendo kwa unafiki.
 
Ingekua hivi
Dsm
1. Taifa
2. Shmba la bibi
Mazoezi chamazi &Gymkana
Zanzibar
1. Amani
Mazoez amani
Mwanza
1. Kirumba
Mazoezi Nyamagana
.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…