Habari zenu wadau...?
Nina rafiki anatatizo la warts sehemy za siri..mwanaume, na anaomba msaada kwa anaejua Dokta mzuri wa kutibu hili tatizo, yeye anaishi Dar. Mungu awabariki
Warts inatibika kirahisi tu hospitali nyingi.Ila kama atapenda pia anaweza kujitibu mwenyewe nyumbani taratibu kwa njia za asili.
Kwanza kwa yeye kupata tatizo hilo pia ni ishara kubwa kwamba kinga yake iko chini na anaweza kuwa na ukosefu wa madini kama vile zinc.Hivyo mambo haya ni muhimu kuyatilia maana kwa kuwa hata kama atapona inaweza kumrudia baadaye kutokana na mapungufu haya.
1.Ale mlo kamili unaohusisha mboga za majani na dona,anywe juisi mbichi ya mboga za majani kama vile spinachi,celery na matembele,anywe juisi ya tango,parachichi,ndizi,chungwa,apende kutumia bizari mbichi kuweka kwenye juisi tajwa hapo juu.Anaweza pia kunywa uji wa dona uliochanganywa na uga wa mlonge angalau kijiko kimoja.Awe na utaratibu huu ili kujenga kinga yake na kurudisha madini muhimu mwilini.
2.Tiba ya tatizo;Vitu vifuatavyo vinaweza kutumika kutibu tatizo/dalili(warts):
Kitunguu maji,kitunguu saumu,apple cider vinegar.Vyote hivi hutumika kwa kupaka na kufunga aidha kwa bandage kwenye eneo lililoathirika.
-Chukua kitunguu maji kimoja katakata na uweke chumvi ya mawe kijiko 1,acha mchanganyiko utulie muda masaa angalau 12,kisha saga mchanganyiko na ukamue maji yake ambayo ndio utatumia kupaka eneo lililoathirika na kukaa masaa 5.
-Kuhusu kitunguu saumu;unaweza kutumia mafuta yake kuepuka usumbufu wa kusaga.Paka mafuta ya kitunguu saumu eneo lililoathirika na ufunge kwa bandage kwa masaa angalau 5.
-Tumia apple cider vinegar pia kwa kupaka eneo lililoathirika kwa utaratibu kama wa hapo juu.Kama utaona kero ya harufu ya kitunguu saumu unaweza kukiacha na utumie kitunguu maji na apple cider vinegar pekee.
Tumia tiba hizi kila siku mpaka utakapoona dalili zimepotea kabisa.
Wakati unatumia tiba hizi hakikisha unakula mlo kamili unaojumuisha vyakula nilivyotaja hapo juu au zaidi ili kujenga kinga yako na kurudisha madini yaliyopotea ambalo ndilo msingi wa tatizo.Ukifanya hivyo vimelea vya magonjwa kama hayo havitakuathiri kwa urahisi.