Elections 2010 Dr Slaa aitikisa Karatu

Regia Mtema

R I P
Joined
Nov 21, 2009
Posts
2,970
Reaction score
866
Mgombea Urais kipitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kesho ataunguruma Nyumbani kwake Karatu. Dr Slaa anakwenda kukutana na wanakaratu aliowatumikia kwa kipindi cha miaka kumi tano(15) akiwa Mbunge. Kabla Dr Slaa hajaenda tayari kuna timu moja toka Makao Makuu imeshakwenda jana kwaajili ya kufanya maandalizi kwa kushirikiana na Watu wa Karatu.

Timu nyingine ikiongozwa na Kamanda Freeman Mbowe inaondoka leo kuelekea huko.Viongozi wa ngazi ya juu wa chama pamoja na Prof Baregu ndio timu inayomsindikiza Dr Slaa. Baada ya kuzungumza na Wanakaratu Dr Slaa atacchukua fomu na kuzunguka nchi nzima kwaajili ya kupata wadhamani. Safari ya kuzunguka nchi nzima Dr Slaa atasindikizwa na Kamanda mwenzake Freeman Mbowe.

Wengine tumebaki Makao Makuu tukiendeleza mapambano.Leo tutakuwa na wawakilishi/mashujaa wa wanazuoni walisaini kutaka Dr Slaa agombee Urais kwaajili ya kupanga mikakati ya namna ya kumuunga mkono Dr Slaa kwa staili mpya kabisa. Mkutano huo unatarajiwa kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 7 mchana Makao Makuu Kinondoni Manyanya Mtaa wa Ufipa.Mnakaribishwa sana kwa wale mnaopenda kushiriki harakati hizi muhimu.

Find attachment hotuba ya Ufunguzi ya Mwenyekiti wa Kamati ya BAVICHA-Bw John Mnyika.

Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke.

Angalia picha chini:


Dr. Slaa akikabidhi fomu kwa Mwenyekiti Mbowe



Karatu wakiridhia Dr. Slaa awe mgombea Urais.
 

Attachments

Akienda huko karatu asisahau kum-endorse na kuwatambulisha wana karatu mgombea mpya wao wa ubunge kwa tiketi ya chadema..


nawatakia kila la kheri wana chadema wote.
 
CCM yajulikana kwa fitina na mizengwe ndani na nje ya chama! Kikubwa chenye matamanio yangu ni kwamba - Dr. Slaa anapewa ulinzi madhubuti na afya yake inatiliwa maanani na kulindwa. Pilikapilika ni nyingi, na katika vikumbo vya hapa na pale katika hizi kampeni, ulinzi na afya vyaweza kuwa overlooked. Usalama kwanza! Haitopendeza kuanza kusikia story kama za akina Yushchenko wa Ukraine...

Nawatakia kampeni njema.
 
Namuamini sana Dr lakini kwahili naona kama anaenda kuliweka jimbo la karatu rehani
 
Namuamini sana Dr lakini kwahili naona kama anaenda kuliweka jimbo la karatu rehani
acha woga!!! jimbo litabaki na mengine yataongezeka. ukombozi wa Tanzania ni sasa!! tuna imani sana na Dr. Slaa
 
Heri aiweke karatu rehani ila aiokoe Tanzania kuliko sasa hivi nchi iko rehani hewani kabisa
 
Kama kweli Lipumba ni mpenda mabadiliko, angemuunga Mkono Dr. Slaa. Ingekuwa vizuri kama viongozi wa CUF na CHADEMA wakawa kwenye maongezi katika ngazi ya juu kabisa. Bila muungano wa namna moja au nyingine hatuwezi kuwashinda mafisadi.
 
Kwa vyombo vya habari vinavyoelezea rushwa za CCM katika kura za maoni sasa hivi, kweli njia ni nyeupe kwa CHADEMA!...Tuko nyuma yenu GS.
 
Binafisi niko tayari kwa HALI na MALI katika kuunga mkono harakati hizi za ukombozi. Naamini huku Morogoro tutakuwa na kazi kubwa ya kufanya katika kusaidia haya mambo...
 
Kila lakheri Dr Slaa, kila lakheri waTanzania. Mapambazuko yamewadia na tusipoteze fursa hii adimu ya kubadilisha mwelekeo wa nchi.
 

Tumejipanga vya kutosha.Hatuwapi nafasi maadui ng'o..Tupo kamili gado.
 
Saa tano kamili atapokelewa na maelfu uwanja wa ndege wa Arusha na kusindikizwa mpaka Karatu ambapo leo atawasha moto huko.

Stay tuned..
 
Kila la kheri Dr. tupo nyuma yako tunakuunga mkono.
 
Na msikitikia sana dokta Maslaa, Ndio mwisho wake huu ametolewa kafara na Chadema!
 
Habari nitazileta.Atapokelewa saa tano mchana uwanja wa ndege wa Arusha na mamia ya wakazi wa Arusha na Moshi na kusindikizwa na magari mpaka Karatu.


all the best GS...usisahau kutupatia nakala ya yatakajojiri leo kwenye mkutano!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…