Nimepata sms kutoka kwa rafiki yangu aliye Mafinga kuulizia yuko wapi Dr Slaa? Kwa maana Wanamafinga wanamngoja na kuongeza kusema ana kura nyingi sana pale.
Sikuweza kujibu yuko wapi na ratiba yake iko vipi, mwenye kujua ratiba yake ya leo na kesho, na lini atakwenda Mafinga atuwekee hapa ili nimjibu swahiba wangu huyo kwa ajili ya watu wa Mafinga wanaemtaka rais wao mtarajiwa awahutubie.