Kikwazo kikubwa cha kuleta mabadiliko ya kweli nchi hii ni wasomi na wakaazi wa maeneo ya mjini. Nimesoma kwenye threads nyingi hapa, watu wengi wenye mashaka kuwa DR Slaa hatapita ni watu ambao wanatamani mabadiliko yatokee ila hawatambui kuwa wao ni sehemu ya kufanya hayo mabadiliko yatokee.
Jana tulikuwa na wenzangu hapa Mzumbe University (Dar Campus) tunajadili kuhusu uchaguzi. Wengi wakawa wanasema watafurahi sana siku CCM ikiondoka madarakani. Lakini papo hapo wakawa wanasema Dr Slaa hataweza kuishinda maana CCM ni ''wezi'' wa kura hivyo haina haja ya kwenda kupiga kura maana upige kura usipige watashinda tu.
Nilisikitika sana maana tuliokuwa tunajadili wengi walikuwa ni wanafunzi wa shahada za uzamili. Nikajiuliza hivi wasomi wa nchi hii wana matatizo gani, maana hii si mara ya kwanza kusikia maneno kama haya kutoka kwa wasomi wa nchi hii. Nilishaona mwaka 2000, 2005 na sasa 2010.
Lakini cha ajabu mwezi wa tatu mwaka huu nilitembelea wilaya ya Newala kijiji kimoja kinaitwa Nkunya, nilikutana na wananchi wengi ambao kielimu naweza kusema sio wasomi- yaani ni darasa la saba kushuka chini, wao walikuwa wanasema kulingana na tabu wanazozipata akijitokeza mgombea yoyote wa upinzani ambaye ''anaeleweka'' wao watampigia kura na atashinda bila shida maana wamechoka na CCM. Maelezo kama haya nimeshayasikia mara nyingi sana huko vijijini kutoka kwa watu wasio wasomi.
Sasa najiuliza kwanini wasiosoma wanaona upinzani unaweza kushinda lakini waliosoma wanaona tofauti?. Zamani kidogo kuna mwalimu mmoja mstaafu aliniambia tabia ya watanzania wasomi kuwa wapole, kuburuzwa, uoga wa kuthubutu na kutokuwa tayari kujitoa mhanga ni mpango kamili ulioratibitiwa katika aina ya elimu tunayopatiwa- yeye alisema Nyerere alitengeneza mfumo wa elimu ambao unatufanya tuwe hivyo. Sikukubaliana na mawazo yake kwa vile huyo mwalimu alikuwa hampendi kabisa Nyerere.
Lakini sasa naanza kuamini watanzania ambao hawajasoma (wengi walioko vijijini) hawajalishwa sumu (indoctrinated) na elimu ya ''Nyerere'' ndo maana wanaona mageuzi yanawezekana lakini wasomi wanaona tofauti.
Anyway, unahitajika utafiti kubaini kwanini wasomi wako pessmistic upinzani kushinda tofauti na watu wasio soma?
Mkuu hapo kwenye red please note:
maelezo yako ya mwanzo unaonekana kuwa na mantiki na kuwashangaa wasomi wenzako wa digrii ya Uzamili. Huku ukiwalaumu wenzako, na wewe mwnyewe umeungana nao kwa mlango wa nyuma kwa kupinga uliyoambiwa na huyo mwalimu. ALICHOKISEMA HUYO MWALIMU NI KWELI TUPU.
Ukweli ni kuwa mfumo wa Elimu wa tanzania unawaandaa watu kutokuwa JASIRI WA KUTHUBUTU, na ndiyo sababu wasomi wa nchi hii wako tayari kuongozwa na mambumbumbu ali mradi tu mambumbumbu hao wamethubutu kujiingiza kwenye siasa na wamewaahidi vyeo vya bure-ukurugenzi, ukamishna, etc. Hata waajiri binafsi wengi si wasomi wa kutisha, wanaoendesha biashara hapa nchini, kwa mfano, wengi wao si wasomi wa ngazi za vyuo vikuu. Usomi wao ni katika kujua na kudiriki kupambana, they are realists.
Si vibaya, chukulia mfano wa Shigongo ambaye amediriki kuanzisha biashara ya magazeti na sasa anawania ubunge, je ni msomi wa chuo kikuu? Je pale Global Publishers hajaajiri wasomi?
Na pengine sababu huyo mwalimu alikuambia hivyo kwa kuzingatia hesabu hii.
Kumbuka ulioanza nao darasa la kwanza, wangapi walibahatika kupata elimu ya sekondari..................kwa nini wengine walikosa, je hawakuwa na akili?
O-level, wengine waliishia wapi, kwa nini?
A-Leve je?
Chuo kikuu undergraduate, wote uliokuwa nao darasani kuna hata mmoja uliyetoka naye kijijini kwako na au ulikuwa naye darasa la saba, form four au form six? Kwa nini iko hivyo? na wewe mwenyewe ukiwa mmoja wa waliobahatika kuelimika hivyo, uko tayari kupambana kutetea maslahi ya wanyonge hata kama ni kupotesa ajira yako na marupurupu yako? kwa nini mangumbalo wasioweza kuanalyze issues wanajiingiza kwenye siasa na wanaweza? kwa nini wasomi wanaogopa wanabaki kulaumu tu pembeni?
-tatizo ni elimu tuliyoipata na hapo ndipo penye shida.
Ukiangalia hata wasomi wanaojitokeza katika masuala ya siasa, wengi wao utakuta kwa namna moja au nyingine wamebahatika kupata elimu ya nje ya nchi hii. wenye Bachelor na Digree za uzamili za hapa bongo ni waoga mno.
Usomi wa nchi hii ni kuajiriwa na kukopa pesa benki na kununua gari, huku umepanga kwenye nyumba ya msomi aliyefeli mtihani wa darasa la saba au form four, but ana ujasiri wa kupambana na mazingira.
tuache kumshambulia Malaria Sugu, maana wasomi mmewaachia watu kama yeye kuwa viongozi wetu. Nchi hii itabadilika pale tutakapoacha kuwa waoga.
NOTE; I have nothing personal.