Elections 2010 Dr. Slaa Jangwani katika Picha

That is very gud,go dr slaa,we are at ur back our saviour,
fulana za sihitaji kura za wafanyakazi zisambazwe kwa wingi
 

walau chonga hicho kimombo basi! Utathubutje kukosea kuanzia lugha, hoja na ukweli wa mambo!?
 
Jamani picha tu hazitoshi. Uandaliwe mkakati wa kusambaza hotuba zilizorekodiwa kwenda mikoani. Mikakati lazima iwe mipana katika kutafuta ushindi.
 

Kumbe ataupata....!!! sio ikiwa ataupata! lol :love:
mix with yours
 
walau chonga hicho kimombo basi! Utathubutje kukosea kuanzia lugha, hoja na ukweli wa mambo!?


Khaa!! Huyu naye sijui kaibukia kutoka wapi na kimombo chake! Haya, kama hicho chako ni bora zaidi hongera sana. Mimi nipo nipo sana na nitakuwepo zaidi.

Kuchemsha kwako kumenikumbusha point muhimu sana. Chadema kuna nepotism ya hali ya juu kabisa. Leo Nime-retrieve files kibao kuthibitisha. Hii karata ni moja ya mbaya kabisa kukosa kura hasa kwa sisi wa mikoani ambao tuna chama letu la nguvu linaitwa Mwandosya. Anayepinga apinge kwa hoja, siyo kwa kidhungu kama huyu hapo juu au kwa kelele kama pombe shop.
 
Of Course Mnamuogopa Slaa kwa Sababu Hamjui Hatima zenu na Baba Zenu Na Mama Zenu Wezi
 
Hiki ni nini sasa? Kwa kweli kama akili za wanaCCM wote ndo zipo kama hizi za kwako na MS, basi si ajabu kwa nchi kuwa maskini. Mtakaa mpange nini cha maendeleo ya nchi kama uwezo wenu wa kuchambua mambo ndo huu? Yale yale ya mbayuwayu..... akili za kuambiwa.....
 
Slaa's very disappointing on the podium

...Ulitaka awe na sura nzuri na anatabasamu kila wakati kama Mwafulani?? Ilimradi anahutubia mambo ya msingi inatosha, mambo ya kuuza sura tunawaachia wenyewe!!
 

Kwani wewe uko nchi ambayo ni tajiri na wewe ukiwa tajiri? Ni hiyo akili inakufanya uwe umaskini binafsi, ukisubiria Slaa akupe utajiri. Utaota sana njozi za mchana. Una hoja tuijadili hapa?!
 
Haya mkuu. Subiri mtu aje achukue pesa za mafisadi awapeni. Sina ziada.


Mkuu KN, Nani aliyekwambia kwamba una la zaidi lingine zaidi ya kupigia debe chama mufilisi cha mafisadi? Hilo la kuzichukua pesa za mafisadi lingewezekana kabisa kama tungekuwa na Kiongozi aliyeweka mbele maslahi ya nchi na pia chama kilichopo madarakani ambacho kimeweka mbele maslahi ya nchi, lakini viliyowekwa ni maslahi ya mafisadi na ndiyo sababu kubwa mafisadi wa EPA, Richmond, Meremeta na wengineo bado wanapeta uraiani pamoja na kufisadi mabilioni ya pesa za wavuja jasho.
 
''Ndugu wananchi Kikwete alikataa kura laki tatu na nusu za wafanyakazi pasipo kufanya mahesabu vizuri. hawa wafanyakazi kama ni mwanaume ana mke na kama ni mwanamke ana mume hivyo kakataa kura laki saba. Hawa nao wana watoto waliofikisha umri wa kupiga kura, wana wazazi ndug na jamaa wanawategemea kwa hali ya familia zetu za kiafrika. Tukijumlisha na kuzidisha hapo tunagundua Kikwete kakataa millioni sita na ushee. Sisi Chadema waheshimiwa wafanyakazi na wananchi kwa ujumla tunazihitaji tupate kuwapigania. Naziombeni hizo kura alizokataa Kikwete nipate kuwatumikia kwa uadilifu.''
 
Ni sawa tutampa ila chedema wanatakiwa silaha zao wasifiche mpaka kipindi cha kampeni,sasa hivi kwa kauli hiyo wenzie wameshaanza kujitetea, mi naomba chadema wawe makini kidogo kama kweli wana nia ya kweli,
 

Kabla ya urais Kikwete aligombea nini Chalinze?
 
Kanyafu nyafuuuuuuuuuu, sijui kama unachosema unakijua au ni unazi wa kisiasa tu, Slaa ni bakora ya Chama Cha Mafisadi/Majambazi, najua kura watazijambazi ili washinde Slaa ni chaguo la wafanyakazi na wategemezi wao,sasa sema ni kura ngapi atapata.Kalagabahooo kaka hata pweza mwenyewe kaona Slaa anamvuto kuliko JK, hata KANU iling'olewa na wafanyakazi na hivyo ndivyo CCM itang'oka.
 
Kama ume quote maneno uwe unasema, kwa mfano hayo kwenye red yametamkwa na nani au ni komenti yako.
 
Kwani wewe uko nchi ambayo ni tajiri na wewe ukiwa tajiri? Ni hiyo akili inakufanya uwe umaskini binafsi, ukisubiria Slaa akupe utajiri. Utaota sana njozi za mchana. Una hoja tuijadili hapa?!

Wana JF Mnajua maana ya KANYAFU NKANWA??? Maana yake Ni MWENYE KINYWA KICHAFU!!! SO haina maana kubishana na mtu aliyejitambulisha kuwa na kinywa kichafu!! Kwa kuwa kitokacho kinywani mwake ni kichafu tu!!!
 
KN achaaaaaa hizo acha kuchafuwa watu huna lolote wewe usitubabaishe na huyo msanii wako JK hamna sera na hamna jipya miaka mitano hakuna kitu cha maana tulichokiona, wiziiiiiiiii mtupuuuuuuuu...

Kama una nondo toa tuzione huna mpango, mngekuwa na mafile ya Slaa mabaya mngeisha yatoa siku nyingi mpaka waziri mkuu Lowassa kiachia ngazi siyo mchezo bwana, achana na Slaa humuwezi hata kidogo.

Huyu mtu ni mzalendo na anaipenda Tanzania siyo nyie wezi, majambazi, mafisadi, mabepari mafirauni wakubwaa, kazi na kutwaaaa kuiibia nchi, watu hawana maji safi, hakuna hospitali, shule ni majengo tuu hayo hayana hata walimu majengo yenyewe mabovuuuuu.

Angalia this time mlivyotia aibu, aibu, aibu mnaibiana kura, kadi za CCM ni feki zimetengenezwa mtu anakuja mpaka home kwako na kamera, form, na pesa juu anakupa ili tuu ujiunge na ukampigie kura wizi mtupuuuuuuuu

Aibu yenu
 
Mkuu, unaonaje ukiongea kiswahili tu ukaeleweka vizuri? Ukiandika kiingereza kibovu kama hiki watu wanaweza wakashindwa kuelewa kama uko serious
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…