Drywall na ujenzi wa kisasa

Nyumba nyingi za drywall zinatumia kuta za nje zinazoitwa siding. Zinatengenezwa kwa aina fulani ya plastic ngumu iitwayo vinyl. Inapendeza na kusafishika kirahisi lakini wajenzi hawafichi haina uimara wa tofali. Inakatika kwa msumeno.

Faida kubwa ya kutumia siding ni kuwa gharama yake ni ndogo kuliko tofali. Cha kushangaza ni kuwa nyumba zinazotumia siding ni nyingi mno ukilinganisha na tofali. Sasa kama wamarekani wanabana matumizi kwa kutumia hizi siding sisi ni vipi hapo?

Ila si kila cha wenzetu ni chema zaidi kwetu. Kama tofali ni rahisi kwetu kuliko siding hiyo ni heri kwetu. Lakini hatuwezi kulinganisha bei kwa sababu sisi hatuzijui hizi kuta za siding.



 
Kwa Tanzania no ghali mno hiyo kitu
Vipi kuhusu uwezo wa huo ukuta dhidi ya wezi?
 
Mkuu mars nyingi ulaya hasa amerka ndo ujenzi wao,very cheep,,,bora utumie tofali za Moro au msata ni cheep zaidi ,,kuhusu wezi no ksms bsnda LA kuku
 
Ni kweli lakini utaitumiaje kwa ujenzi wa kwetu bongo? Maana inahitaji wall framing kwa mbao au metal studs, Mbao zetu sio well treated zinaliwa na mchwa faster na metal stud kwetu bado hazijaanza kutumika, kwahiyo kwetu zitatumika kwa celing kwa sasa aise. Pia hakuna waterproof ni only moisture resistance, uzito inategemea unatumia size gani maana zipo tofauti thickness na urefu. Yapo mengi ya kuelezea ngoja niishie hapo.
 
Ukiona wanajenga magorofa kwa zege nyembamba hivyo ni kwa sababu hawana mpango wa kutumia tofali kwenye kuta za ndani. Watatumia drywall au glass.
Most gorofa wanatumia dirtt wall kugawa vyumba, dry wall inatumika sehemu ndogo sana ie storage na vyooni around elevators pia.
 
Kwa nyumba ya kawaida ya nyumba vitatu Na senile nahitaji material kiasi Gani Na itanigharimu shilingi ngapi?
Sikushauri utumie kwa tanzania sababu framing structure yako itakuwa ya mbao tu. Gharama itakuwa ndogo compare tofali.
 
Hapa ndiyo na mimi ninapomsubiri. Atupatie hizo gharama na life span yake huo ukuta
Life span yake ni kubwa. Ila kwa nyumba za kawida bongo nasema NO unless unatumia metal framing.
 
Most gorofa wanatumia dirtt wall kugawa vyumba, dry wall inatumika sehemu ndogo sana ie storage na vyooni around elevators pia.

Uko vizuri mkuu lakini hii mara nyingi ni kwenye maofisi. High rise apartments au condominium wanakata vyumba kwa drywall.
 
Uko vizuri mkuu lakini hii mara nyingi ni kwenye maofisi. High rise apartments au condominium wanakata vyumba kwa drywall.
Any residential ni drywall. Commercial high rise office dirtt. Mall maduka drywall
 
Mkuu mars nyingi ulaya hasa amerka ndo ujenzi wao,very cheep,,,bora utumie tofali za Moro au msata ni cheep zaidi ,,kuhusu wezi no ksms bsnda LA kuku

Kwanza nizungumzie suala la wizi. Wanapozungumzia uimara wanazungumzia umri wa hizi kuta. Tofali zinadumu miaka mingi zaidi na haziliwi na mchwa. Hawazungumzii uimara wa kukata ukuta na kisu.

Ili kibaka avunje huu ukuta atahitaji vifaa vya umeme kama drills na misumeno ya umeme. Kibaka wa mtaani hana hivyo vitu. Labda atumie nyundo. Kama ni nyundo si bora avunje mlango. Na nyundo ikiwa hevi anaweza hata kuvunja tofali.

Huu ukuta shughuli yake inaweza kuwa ngumu kuliko tofali. Kwanza inabidi kukata siding za plastic ngumu. Halafu ukate gypsum (drywall). Ufukue au ukate manyavunyavu na masopongi ya ndani ya ukuta. Baada ya hapo unakutana na mbao za nguvu. Kazi haijaisha unakutana tena na gypsum (drywall) ya upande wa pili.

Amini usiamini kuna apartments fulani magorofa kama 15 ya matofali ya kuchoma yaliyojengwa zamani. Wapangaji walipewa notisi wakahama wote. Jamaa wakaleta bulldozers wakavunja yale magorofa yote wakafunga haya maboksi yao wakaanza kupangisha upya.
 
Any residential ni drywall. Commercial high rise office dirtt. Mall maduka drywall
Nchi kama marekani all town homes na apartment wanatumia wood (timber) na dry wall size ya residential ni 1/2 inch thickness, kwahiyo wanapunguza weight kubwa sana kutumia drywal.
 
Any residential ni drywall. Commercial high rise office dirtt. Mall maduka drywall

Inasikitisha sana kuona sisi bado tunabebesha watu tofali wapande nazo juu ya gorofa kujengea vyumba. Ila si haba Dar hii minara ya kisasa inachomoza mmoja mmoja kama uyoga.
 
Inasikitisha sana kuona sisi bado tunabebesha watu tofali wapande nazo juu ya gorofa kujengea vyumba. Ila si haba Dar hii minara ya kisasa inachomoza mmoja mmoja kama uyoga.
Yaap good things. Im teaming up na architecture mmoja kutaka kufanya metal framing bongo tuone km people will like. Si unajuwa nchi zetu hizi. But ni kitu nzuri sana na ina last hata 300 years wewe unafanya touch up ya drywall tu.
 
Yaap good things. Im teaming up na architecture mmoja kutaka kufanya metal framing bongo tuone km people will like. Si unajuwa nchi zetu hizi. But ni kitu nzuri sana na ina last hata 300 years wewe unafanya touch up ya drywall tu.

Elimu ni ufunguo. Watu wakielemishwa siku hizi dunia ni kijiji. Teknoloji mpya zitafika. Watu waelimishwe pia kutumia mitandao kwa manufaa.
 
Huu ujenzi bila shaka utakuwa na ghalama sana



Tizama izo mbao ziliwekwa kwenye ukuta Huu ujenzi kibongo bongo utakuwa unaglama Kwasababu bei ya tofali ipo chini na mbao zipo juu


Labda kwenye maofice ndio unafaa huu ujenzi wa Drywall

Alfa kwenye uimala wa nyumba tofali is the best for me.
 
Disadvantage ndio nyingi kushinda Advantage
 

Mbao nyingi ziko kwenye dari. Wewe kama unataka kujenga nyumba yako ya vyumba sita upangishe juu uweke bati huhitaji mbao nyingi hivyo.

Halafu hilo nalo neno. Nyumba za Marekani zina shimoni (basement) na juu zina levo moja au mbili. Na hazitumii zege kwenye dari. Ni mwendo huo huo wa drywall.

Nyumba za Bongo zinatumia vyuma kwenye zege. Hizi nyumba zege iko kwenye msingi tu. Sasa chuma na mbao ipi bei kubwa.


Tizama kwenye hii picha kama utaona chuma cha zege.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…