DStv punguzeni bei ya vifurushi vyenu kwa ushindani

Cha chini ni 19,000 na cha juu kwabisa 85,000
mbona Maxologist anasema cha juu ni 110,000

MIXOLOGIST Bei ni ya kawaida, inategemea unalipia kifurushi gani kwa ambayo ninailipia mimi, inacheza kati ya 110,000/- 100,000/- compact plus, it is very satisfying. 110,000/- ukigawanya kwa siku 30 ni kama 3500 kwa siku, ki-bongo bongo siyo mbaya. Siwezi kuelezea gharama za ku- connect kwa sasa, kwani nilijiunga nao zaidi ya miaka kumi iliyopita, hivyo kwa msaada zaidi tembelea ofisi zao.
 
Ninayo tayari lkn bei zilinikimbiza . compact plus unapata BBC, CNN, geographical, au? hizi ndizo bomba na mipira (ingwa sina ushabiki wa mpira)
Unapata Nat Geographic (ordinary and Wild), History, Discovery (Family and Ordinary), Super Sport 1-4 and sometimes zote, Cartoon zote mpaka, Food Tv, MTV, BET, MNET na ya kibongo na channels nyingine nyingi tu

Mkuu hii ni compact plus, ila kifurushi cha premium ni ghali zaidi na inategema una users wangapi kama ni multiple users bei itaongezeka zaidi
 
Unapata Nat Geographic (ordinary and Wild), History, Discovery (Family and Ordinary), Super Sport 1-4 and sometimes zote, Cartoon zote mpaka, Food Tv, MTV, BET, MNET na ya kibongo na channels nyingine nyingi tu
CNN, BBC unapata kwa kulipa ngapi naona hujaiweka
 
CNN, BBC unapata kwa kulipa ngapi naona hujaiweka
Hizo zipo Mkuu, kwa hiyo hiyo compact plus, mimi wananitumia sms nilipie kiasi kuanzia 110,000/-100,000/- ndiyo range yake, sometimes uwa natupia say 120,000/- definitely next month utajikuta unalipa pungufu
 
Hizo zipo Mkuu, kwa hiyo hiyo compact plus, mimi wananitumia sms nilipie kiasi kuanzia 110,000/-100,000/- ndiyo range yake, sometimes uwa natupia say 120,000/- definitely next month utajikuta unalipa pungufu
asante.
 
Ni ujinga kuanza kuwalinganisha DSTV na AZAM TV!
AZAM TV imepata wapenzai wengi(?) kwa sababu wanarusha matangazo yao kwa kiswahili ila hayana ubora wowote!
AZAM TV hawana tv Presenters, wana watangazaji wa radio tena waliochoka ndio inafanya kuwaokota mitaani!
AZAM TV hawana PROGRAM yoyote ambayo mtu unaweza kurekodi ana kuhifadhi for future use!
AZAM TV ni kwa matumizi ya wanasiasa tu haina maana kabisa.
DSTV NI MWANZO NA MWISHO WA TV PROVIDERS WOTE HAPA TANZANIA!
HATA BEI ZAO WAKIPANDISHA MARA MBILI AU TATU THEY DESERVE IT!
 
uko sahihi kabisa na kwa kuongezea EPL wameigawanya Africa katika zone 3, South Africa, Nigenia na The rest of the Africa sasa Azamtv rights anazohitaji ni za The rest of the Africa maana tz ndo inafall humo na bahati mbaya hiyo rights za the rest of the africa ndio the most competitive na ndo the most expensive so kuna kazi kidogo hapo ila kama azam wako serious kweli na EPL kwanini waligombanie rights za game moja kwa wiki ambazo anazo kwese sasa hivi kupitia tv1 na hizo rights huwa hutakiwi kuuza ni kwa ajili ya kutoa Free (EPL wanatoa game moja kwa wiki Free) Azam waanzie hapo kwanza kabla ya yote.
 
seems unaipata vizuri dstv. ebu niwekee package zake hapa tz maana kila mmoja anataja bei zake,,,,, hasa kule kwenye CNN, BBC etc (channels kali kama hizo)
 
Dstv huanzia 19,000 alafu 69,000 na 169,000. Bei zako umetoa wap?
 
Kifushi cha 100000, 80000 na 60000 kwa watanzania Wa leo ni ghali sana kwao kununua majumbani mwao. Iko siku soko la Tanzania litawawia gumu. Wengi wanaonunua dstv ni kwaajili ya EPL basi ambayo lazima wawe na kifurushi kisichopungua sh.80000+
Wangekuwa hawapati wateja wangeshashusha bei.
 
Is this true? Mixologist anasema unalipa in the range of 100,000... 110,000 or 120,000
Ipo hivi, kama unatumia kifurushi cha 110,000/= kama anachotumia yeye basi hata kikiisha watakutumia ujumbe ulipie hiyo kiasi, Mimi natumia cha 69,000/= napata BBC,CNN,SUPER SPORT 3,8,7,10.......VUZU,MNET CITY,BET na Chanel zingine kibao za Movie na Entertainment......kikiasha, wananitumia msg ya kulipia hiyo 69,000.........ila kama walivyosema wadau, ukianza kutumia DSTV hutajuta hata kama unaona bei ipo juu.
 

Safi kabisa mkuu, hapa nina swali je kifurushi hiki tutapata full cover ya World Cup?? Sitaki kukosa hata channel moja inayohusu World Cup. Maana nalipia cha juu yake ila maumivu yamekuwa makali na hii awamu sijui wanafaidika na nini sisi uchumi wetu kuyumba kiasi hiki.
 
Nishauri nilipie kipi sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…