Governor of Bettors-GB
JF-Expert Member
- Jul 14, 2013
- 10,568
- 9,710
Uza nikupe TalakaNgoja nitafute mteja niuze azam tv.
Mstahiki Meya hii sio habari waambie na hao hapo pichani.
Kifurushi hiki kipo siku zote na mimi nilinunua ungo wao mwaka jana mwezi Agosti nilikikuta na ndio hasa natumiaga kila mwezi hata sasa. Nashanga mnaposema kinazinduliwa wakati tunatumia kila siku.
Habari ya mujini tunayoingoja toka kwao ni kuonekana kwa ITV kwenye DSTV.... hiyo ndo itakuwa habari sio hii.
Wangefanya vizuri zaidi kama wangejumuisha chanel za Super sports kwa bei hiyo.
Kuna za chini ya kapeti kuwa mkataba wa super sport na Dstv unakaribia kuisha na Azam. Tv ameshafanya mazungumzo na super sport ili kuingia mkataba
Nadhani dstv wameshaliona hilo ndo maana wanakuja na package ndogo ila is too late.
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
Wanasema ITV na Cloud tv zitaanza kuwa hewani kuanzia October.
Mkuu, hiki kifurushi kina channel za News kama BBC, CNN, Fox n.k?
Hakuna jipya hapo. Package ya Access ipo siku nyingi kwa bei hiyo ilikuwa 16.5k nadhani baada ya dola kupanda ndo inakuwa 17.5k. Nadhani hii ni kwa wanataka kujiunga n not wateja wao wa zamani.
Ndugu yangu kwani mkuu wa kaya nae si ni msomi yule tena mchumi sasa unataka viongozi gani tena wasomi? naibu waziri wa fedha ni mchumi wa first class digrii ya udsm sasa sijui huyu nae sio msomi?
Azam tv hana ubavu wa kumnyang'anya tenda Dstv ya kuonyesha chanel za super sport. Walikuja wajerumani wa g-sport miaka ya 2000+ wakachukua tenda ya kuonyesha match za primier wakachemka. Hawakumaliza hata msimu mmoja wakawa wamefilisika.
Nawashangaa wabongo kwakulalamika eti dstv anatoza bei kubwa kwenye kifurushi cha primium. Sasa ulitarajia uangalie ligi za ulaya kwa kulipa buku 10??? Teteteteee.
We unadhani watu wanakurupuka wanaenda viwanjani kufunga kamera na kuanza kurusha match live bila mikataba na vyama vya mipira? Supersport analipa hela nyingi sana kununua haki za matangazo na maonyesho ya mipira naye anakuja anamuuzia Dstv ili amrushe live na dstv anakukamua wewe mlaji wa mwisho.... dstv imesambaa karibu afrika nzima tofauti na azam inayoishia mtukula unadhani akinunua mkataba wa dstv atakukamua sh ngap we mlaji, na ndo hivo hana wateja wengi. Mwisho wa siku ataambulia hasara takatifu kwani hata akiwatoza mara 2 ya zile za dstv yan tsh.300,000 kwa mwezi bado hawezi kuiepuka hasara kwasababu ana wateja kiduchu.
Otherwise mtakua mnajifariji na maneno ya kwenye vijiwe vya kahawa.
Vipi kuhusu star TV, channel 10 na TBC , kwa package hii ya 17500 zinaonekana?