Duh! bora hili la kuwaita Warundi waje kuilima Tanzania

Kwenye karatasi tu ila wabishi wanapeleka kama kawa na kwa sasa hivyo vikwazo vilishatolewa
Itakuwa unaishi vijijini kule maeneo ya Mkuranga au Kolomije. Tuulize sisi ambao tupo mipakani. Hata viwanda vya kutengeneza vyakula vya kuku na mifugo, ambavyo vipo kwenye barabara ya Nairobi-Namanga vinapata supply yao ya mahindi kutoka U.G. Yimekula kwenu nyinyi wakulima wa jasho jingi na majembe.
 
Imekula wapi wewe wakati huku wafugaji ndo wanakula maisha vyakula vya mifugo vinakua vya kumwaga na we unaweza ukawa mpakani ila kipofu sio lazima uletewe mahindi uambiwe haya yametoka tz watu wanapeleka ila usitake kujua zaidi wanapelekaje.........sehem za michezo mitamu ni sirari na tarakea we kaa namanga kula vumbi tu
 
Kuna tofauti kubwa kati ya ukulima na kilimo biashara. Mkulima anayejielewa huwa anapeleka mazao yake kwenye soko ambalo litamletea faida kubwa iwezekanavyo. Sirari, Tarakea kote nakufahamu vizuri wewe endelea kukariri ukiwa huko Mkuranga. Sasa hivi mbao ndizo zinavunwa na wakenya kutoka shamba la bibi. Hii ni baada ya marufuku ya kukata miti kutekelezwa Kenya.
 
Agizo lilishakuwa reversed na prime minister bungeni, mwezi unakata sasa
Huyu yupo kwenye fulusuti lake anatupigia kelele tu inawezekana huko kote anapoongelea anapaona tu kwenye ramani ya infinix yake
 
Serikali yaondoa zuio kuuza mazao nje ya Nchi
 
Tusifurahie, kwa jinsi tulivyo mazuzu, Hawa Leo wanakuja kama vibarua Na baada ya muda mfupi wao ndio watakuwa wamiliki wa ardhi
Mkuu mbona hili halijaanza leo?sma tu serikali imeamua kulitangaza rasmi!!tena sehemu kama wilaya ya ngara hawa jamaa wanafanya kazi kama mashine tena kwa ujira kidogo sana na matajiri wengi sana wanafaidika kupitia hawa jamaa kwani utakuta mtu ana ng'ombe 1000!! Warundi ndio wachungaji ,na we mtu analima ekali moja kwa 50,000!!! Daa hao jama ni ma bulldozer ,ukienda huko katavi ,tabora ndio walimaji wakubwa wa tumbaku kwnye mashamba!!
 
Huyu yupo kwenye fulusuti lake anatupigia kelele tu inawezekana huko kote anapoongelea anapaona tu kwenye ramani ya infinix yake
Hahaha infinix sio? Kwetu tunavaa shuka sio suti. Eroo tumeelewana long'ui?
 
Agizo lilishakuwa reversed na prime minister bungeni, mwezi unakata sasa
Basi itakuwa wanaingiza vikwazo vingine. Biashara kwenye mipaka na Tz imedorora kweli kweli. Sijaelewa shida ipo wapi lakini upande wa Kenya kila kitu kipo shwari.
 
Haijalishi, mwisho wa siku wao watalima hata kwa kujificha kwa kutumia mgongo wa neno vibarua, hiyo ni lugha ya kuficha aibu.
Sasa atakuja na shamba kutoka Burundi ?
 
Hawa wanakuja kufanya vibarua, na si ufikirivyo ww,yaelekea akili zako unatumia kuvukia barabara tu.....?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…