Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
DUKA LA MAFUTA YA TAA LA MAMA MARIA NYERERE KARIAKOO NA MAGOMENI 1955
Duka la kwanza la Mama Maria Nyerere lilikuwa Mtaa wa Livingstone na Mchikichi kisha Mama Maria akafunga duka hili la Kariakoo kwa ajili ya umbali baada ya kuhamia Magomeni Maduka Sita kwa msaada wa Ali Msham aliyekuwa amefungua tawi la TANU nyumbani kwake Mtaa wa Jaribu, Ali Msham akamfungulia Mama Maria duka nyumbani kwake Mtaa wa Jaribu palipokuwa na tawi la TANU.
''Nikiwa mtoto nakumbuka sana vipi baba akishughulishwa na kutaka kuona kuwa Mama Maria na watoto wake hawakosi chochote kuyafanya maisha yao kuwa mepesi, ya starehe na furaha akihakikisha chakula kinapelekwa dukani kwa Mama Maria kila siku katika duka lake dogo lilikuwapo Mtaa wa Livingstone kona na Mtaa wa Mchikichi, hiki kikiwa kielelezo chake kikubwa kabisa cha huruma na ukarimu wake.''
Aisha ''Daisy'' Sykes (2018)
Duka la kwanza la Mama Maria Nyerere lilikuwa Mtaa wa Livingstone na Mchikichi kisha Mama Maria akafunga duka hili la Kariakoo kwa ajili ya umbali baada ya kuhamia Magomeni Maduka Sita kwa msaada wa Ali Msham aliyekuwa amefungua tawi la TANU nyumbani kwake Mtaa wa Jaribu, Ali Msham akamfungulia Mama Maria duka nyumbani kwake Mtaa wa Jaribu palipokuwa na tawi la TANU.
''Nikiwa mtoto nakumbuka sana vipi baba akishughulishwa na kutaka kuona kuwa Mama Maria na watoto wake hawakosi chochote kuyafanya maisha yao kuwa mepesi, ya starehe na furaha akihakikisha chakula kinapelekwa dukani kwa Mama Maria kila siku katika duka lake dogo lilikuwapo Mtaa wa Livingstone kona na Mtaa wa Mchikichi, hiki kikiwa kielelezo chake kikubwa kabisa cha huruma na ukarimu wake.''
Aisha ''Daisy'' Sykes (2018)