Mdakuzi
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,294
- 6,872
Jumanne, Januari 14, 1958
United iliichapa Red Star Belgrade mabao 2-1 katika mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Ulaya kwenye uwanja wa Old Trafford.
Jumatatu, Februari 3, 1958
Kikosi cha Manchester United kilikwea ndege ya kukodi kutoka Manchester kwenda Belgrade, Yugoslavia. Safari hiyo ilipangwa kupitia Munich kwa safari zote kwa ajili ya kujaza mafuta, baada ya ndege hiyo kukosa ruti ya moja kwa moja.
Saa chache baadaye wakiwa angani, wakakumbana na hali ya hewa mbaya, mawingu mazito, kushindwa kuona na barafu. Hali iko chini ya kiwango kinachoruhusiwa na shirika la British European Airways (waliowakodisha ndege hiyo) kuruhusu marubani kutua.
Hali inazidi kuwa mbaya kiasi kwamba mhandisi wa uwanja wa ndege wa Munich alishtukia tu ndege imetua wakati alipoiona ikiegeshwa.
Jumatano, Februari 5, 1958
United ilitoka sare ya mabao 3-3 naushindi wa mabao 4-0 wa Red Star Belgrade na kufanikiwa kusonga mbele kwenye nusu fainali ya Kombe la Ulaya kwa msimu wa pili mfululizo.
Baada ya mechi, pati ya nguvu ikaandaliwa kwa ajili ya wachezaji ambayo ilifanyika kwenye Ubalozi wa Uingereza.
Alhamisi, Februari 6, 1958
Msafara huo, pamoja na abiria wengine watano walioongezeka - akiwemo mke na binti wa ofisa wa jeshi la anga katika Ubalozi wa Yugoslavia jijini London – uliondoka jijini Belgrade
wakati wa mawio kuelekea Manchester.
Safari ilichelewa kwa saa moja baada ya winga Johnny Berry kupoteza paspoti yake. Baadaye, ndege hiyo ikaondoka na kutua Munich kwa ajili ya kujaza mafuta, ambapo uwanja wa ndege umezingirwa na mawingu, mvua na barafu.
Kutua kwenye uwanja huo wa Munich kulimlazimu rubani, Kapteni James Thain, kutumia vifaa maalum vya kukabiliana na barafu, kwenye mabawa.
Baada ya kutua, msafara wa Manchester ulitoka kwenye ndege na kuingia kwenye jengo la uwanja huo, huku baadhi ya wachezaji wakitaniana na wafanyakazi waliokuwa wakijaza mafuta kwenye ndege.
Baada ya kukamilisha taratibu za kuondoka, abiria wote walirejea kwenye ndege, huku wafanyakazi wa ndege hiyo wakiikagua hasa kwenye mabawa.
Kwa tahadhari, mafuta ya kuzuia barafu yangeweza kupakwa kwenye mabawa ama barafu kutolewa, lakini wakaamua kuacha kutokana na mazingira yalivyokuwa.
Majira ya saa 8.20 mchana (GMT), takriban zaidi ya saa baada ya kuwasili, ndege hiyo ikawa tayari kwa kupaa. Hata hivyo, sauti isiyo ya kawaida kutoka kwenye injini ikamshtua rubani Kapteni Thain na msaidizi wake, Kapteni Kenneth Rayment.
Inaendelea...
Ova
United iliichapa Red Star Belgrade mabao 2-1 katika mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Ulaya kwenye uwanja wa Old Trafford.
Jumatatu, Februari 3, 1958
Kikosi cha Manchester United kilikwea ndege ya kukodi kutoka Manchester kwenda Belgrade, Yugoslavia. Safari hiyo ilipangwa kupitia Munich kwa safari zote kwa ajili ya kujaza mafuta, baada ya ndege hiyo kukosa ruti ya moja kwa moja.
Saa chache baadaye wakiwa angani, wakakumbana na hali ya hewa mbaya, mawingu mazito, kushindwa kuona na barafu. Hali iko chini ya kiwango kinachoruhusiwa na shirika la British European Airways (waliowakodisha ndege hiyo) kuruhusu marubani kutua.
Hali inazidi kuwa mbaya kiasi kwamba mhandisi wa uwanja wa ndege wa Munich alishtukia tu ndege imetua wakati alipoiona ikiegeshwa.
Jumatano, Februari 5, 1958
United ilitoka sare ya mabao 3-3 naushindi wa mabao 4-0 wa Red Star Belgrade na kufanikiwa kusonga mbele kwenye nusu fainali ya Kombe la Ulaya kwa msimu wa pili mfululizo.
Baada ya mechi, pati ya nguvu ikaandaliwa kwa ajili ya wachezaji ambayo ilifanyika kwenye Ubalozi wa Uingereza.
Alhamisi, Februari 6, 1958
Msafara huo, pamoja na abiria wengine watano walioongezeka - akiwemo mke na binti wa ofisa wa jeshi la anga katika Ubalozi wa Yugoslavia jijini London – uliondoka jijini Belgrade
wakati wa mawio kuelekea Manchester.
Safari ilichelewa kwa saa moja baada ya winga Johnny Berry kupoteza paspoti yake. Baadaye, ndege hiyo ikaondoka na kutua Munich kwa ajili ya kujaza mafuta, ambapo uwanja wa ndege umezingirwa na mawingu, mvua na barafu.
Kutua kwenye uwanja huo wa Munich kulimlazimu rubani, Kapteni James Thain, kutumia vifaa maalum vya kukabiliana na barafu, kwenye mabawa.
Baada ya kutua, msafara wa Manchester ulitoka kwenye ndege na kuingia kwenye jengo la uwanja huo, huku baadhi ya wachezaji wakitaniana na wafanyakazi waliokuwa wakijaza mafuta kwenye ndege.
Baada ya kukamilisha taratibu za kuondoka, abiria wote walirejea kwenye ndege, huku wafanyakazi wa ndege hiyo wakiikagua hasa kwenye mabawa.
Kwa tahadhari, mafuta ya kuzuia barafu yangeweza kupakwa kwenye mabawa ama barafu kutolewa, lakini wakaamua kuacha kutokana na mazingira yalivyokuwa.
Majira ya saa 8.20 mchana (GMT), takriban zaidi ya saa baada ya kuwasili, ndege hiyo ikawa tayari kwa kupaa. Hata hivyo, sauti isiyo ya kawaida kutoka kwenye injini ikamshtua rubani Kapteni Thain na msaidizi wake, Kapteni Kenneth Rayment.
Inaendelea...
Ova