Dunia hakika ina mambo. Tumekutana na mganga ambaye sharti lake uitikie 'beeee' kila akikuita!

WhoWeBe

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2022
Posts
2,299
Reaction score
4,282
Baada ya mgonjwa wetu kurudishwa hospitali kutokana na kushindwa, ikatulazimu kujaribu upande mwingine, sasa zunguka weeee bila bila, afadhali hakuna.

Jana tukatonywa juu ya uwepo wa mtaalamu mwingine kijiji fulani, tukaondoka huko tulikokuwa na leo asubuhi tumefika kwa huyo 'mtaalamu'.............dah!

Sura ya 'kitaalamu' kweli kweli, inatisha akikuangalia. Mazingira ya kitaalamu pia, zagazaga za kila aina na kila sehemu. Masharti sasa, hilo la kwanza tu sielewielewi mpaka sasa; eti yeye kwake wito wake unaitikwa kwa sauti ya 'beeeee'. Hiyo ni kwa yeyote (awe mgonjwa au muuguzi; awe me au ke) na wakati wowote utakaokuwa hapo.

Nipo hapa nje natafakari haya maisha wakati wengine wapo huko wanaendelea kusikiliza yaliyobaki!
 
Itika mkuu, Kwan unapungukiwa Nini?

Ukitaka cha uvunguni, sharti uiname.
 
Kumbe kwa mtaalam network uwazinashika!
 
Sio uitike Rabaika
 
Jaribu pia kutumia healing power Mimi nachojua sisi Binadamu tunaweza kujiponya dhidi ya changamoto yetu .


Muda Mwingine Maisha ukiyatazama yamejaa uyawani unakuta mtu Kama wewe anataka kukufanya umtii kwa kuitikia maagano yake ya Abee it is about shit sema tuishi tu
 
Huyo lazima akukule 0713
 
Naamini umeprove kwamba elimu ni kujilisha ujinga.

Madigrii na maPhD wanaitika beee kwa mwamba hapof
 
Achana na hao wapuuzi, peleka mgonjwa wako kanisani au kwa mtumishi wa Mungu akaombewe.

Bora ufie kanisani kuliko kufia kwa mganga
 
Mwisho wa siku huyo anaweza kuwageuza mbuzi dume
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…