Thecoder
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 1,590
- 4,244
Natumai mko salama.
Kama kichwa cha habari kinavyosema kwamba dunia ni uwanja wa vita za hatima kwahiyo kila mtu ambae yuko hapa duniani anapaswa kujua kwamba yuko vitani na swala la kushinda au kushindwa ni juu ya mtu mwenyewe.
Sasa iko hivi...
Kimsingi ni kwamba kila mwanadamu ambae yuko kwenye hii dunia hayupo hapa kwa bahati mbaya na inawezekana wazazi waliomzaa mtu huyo wanaamini wamemleta huyo mtu hapa duniani kibahati mbaya ila kiroho hakuna kitu kinachoitwa bahati mbaya.
Maadam umezaliwa na uko hapa duniani basi kaa ukijua kuna mission unatakiwa uitimize na hii mission ndio ambayo tunaita hatima na pindi utakapoitimiza mission hiyo basi hapo ndio utakapopata uhuisho wa roho yako na kuifanya iwe hai milele na roho ambayo iko hai ndio roho ambayo husikia inaposemeshwa na ndio maana katika asili za kiafrika hasa hapa nyumbani Tanzania unakutana na kitu kinaitwa mizimu.
Sasa mizimu ni nini? Mizimu ni roho ambazo ziliishi kwenye milli ya watu fulani kwa uadilifu kwa maana ziliweza kujua zipo hapa duniani kwa lengo gani yaani hatima yao na wakapigana vita ya kuiendea hiyo hatima na wakafanikiwa kwa kiasi kikubwa na pindi deadline yao ya kuishi hapa duniani ilipofika zile roho zao ziliweza kuuhishwa na kupata uzima wa milele.
Kwahiyo Sasa katika ile mitetemo ya mfumo nyota ya koo na koo ukiweza kujiungamanisha kiroho na roho za babu ambao unawajua walikua manguli katika upande wa kutibu au kwenye jambo lolote lile ambalo lilikua hatima ya babu huyo ila ilimradi tu uwe na uhakika kwamba alifanya kweli makubwa na sifa zake hadi leo bado zipo hapo kijijini basi ukijiungamanisha tu na roho za watu wa namna hii huwa zinasikia na zinatoa majibu papo kwa hapo.
Nimesema uwe na uhakika kwasababu usije ukaenda kujiungamanisha na mtu ambae huna uhakika nae na ukaenda kuvaa roho za ajabu zikakutesa kwenye maisha yako na hapa ndipo ambapo watu wengi wanachukia haya mambo ya mizimu kwasababu huwa ni ngumu kujua babu yako mzaa babu yako alichokifanya kama kilisaidia kuongeza positive energy hapa duniani au laa (hapa nitapazungumzia vizuri huko mbele na utajua kwanini watu wanakimbilia kwa Yesu au Muhammad huku wakiacha mizimu ya babu zao kule kijijini).
Kwasasa turudi hapa kidogo...
Kikawaida binadamu huwa yuko na pande kuu mbili yaani ya damu na nyama na ya kiroho.
Upande wa kiroho ndio Upande ambao umembeba mtu halisi na ndio upande ambao unamuunganisha mtu na ulimwengu wa asili yake na upande huu huu unapokuwa hapa duniani huwa unatumika kama redio call na kwanini kama radio call basi nitakwenda kukuelezea hapo mbele kidogo. Na upande wa damu na nyama ndio upande ambao unamuunganisha mtu na ulimwengu huu wa vita za hatima.
Wakati mtu anapozaliwa huwa anakua anaishi zaidi kwenye ulimwengu wa kiroho kuliko ulimwengu huu wa damu na nyama ila kadri anavyokua na kujifunza mambo mapya ile mitetemo yake ya ulimwengu wa asili yake inapungua na ya ulimwengu huu inaongezeka hadi kufikia kwenye ukubwa toshelezi na hapa ndio mtu anaanza kuishi maisha ya ulimwengu huu wa damu na nyama na kusahau namna ya kuishi ulimwengu wa kiroho.
Na kutokana na kwamba binadamu anaishi zaidi katika ulimwengu wa damu na nyama kuliko ulimwengu wa kiroho hii imefanya wengi wetu tushindwe kuelewa lengo na dhumuni la sisi kuwa hapa duniani na badala yake tunaishi kulingana na mfumo wa kidunia na kushindwa kuelewa hatima zetu ni nini.
Na kitu cha kikuu na chaumuhimu zaidi kuhusu hatima ni kwamba kwenye hatima yako ndiko kuliko na bahati yako na vitu vyote ambavyo unapaswa kuvimiliki hapa duniani vipo kwenye hatima yako.
Kwahiyo watu wote ambao wanaziendea njia za hatima yao iwe kwa kujua au kwakutokujua huwa hawahangaiki kwenye swala la fedha kama ambavyo watu wanaoishi kwenye maisha yaliyo nje ya hatima zao hufanya.
Na ninaposema hatima kuna watu wanadhani nazungumzia kitu fulani ambacho ni maalumu sana yaani kitu ambacho hakiwezekani kugundulika kirahisi raising hivi, ila naomba nikutoe wasiwasi na nikwambie tu kwamba hakuna umaalumu wowote kwenye hatima kwasababu hatima ni mambo yote ambayo yanaweza kufanyika hapa duniani ili kuongeza nguvu chanya na kuifanya dunia iwe sehemu salama.
Kwa maana hiyo kuna watu hatima zao ni kuburudisha na kuna watu hatima zao ni kuvumbua mambo kadha wa kadha na kuna watu hatima zao ni kutibu watu wengine na kuna watu hatima zao ni kufundisha mambo mbalimbali na kadhalika.
Na ili uweze kufikia hatima yako lazima upite kwenye njia fulani na hiyo njia ndio huwa tunaiita kipawa au kipaji.
Ndio, ni kipaji kwahiyo wala usishtuke kwasababu hata wewe unachokipaji ambacho ukikitumia kitakupeleka moja kwa moja kwenye hatima yako na mara tu utakapofika kwenye hatima yako basi watu wote watajua kwamba yupo au alikuwepo mtu fulani ambae alifanya makubwa sana kwenye mambo haya ya burudani hasa upande huu wa mpira na mtu huyo aliitwa Leonel Messi au Christiano Ronaldo.
Au alikuwepo mtu ambae alifanya makubwa sana kwenye mambo haya ya uvumvuzi wa mambo ya kisayansi ambae aliitwa Isaac Newton.
Au alikuwepo mtu ambae alifanya makubwa sana kwenye haya mambo ya muziki wa rege ambae aliitwa Bob Marley.
Au alikuwepo mtu ambae alifanya makubwa sana kwenye upande wa mashoati na movie za kupigana za karate aliitwa Blue Lee.
Kwahiyo hii inakwenda zaidi na zaidi na kuwafikia vizazi na vizazi huku wakiishi na kuutukuza ufalme wako kwenye upande huo wa hatima yako bila kujali mwaka ambao deadline yako ilifika na wewe kurudi kwenye ulimwengu wa asili yako huku roho yako ikiuhishwa na kupata uzima wa milele.
Na lazima ujue pia kwamba ukubwa wa hatima baina ya mtu na mtu huwa umetofautiana yaani kuna watu wamebeba hatima za kidunia ila wapo waliobeba hatima za kibara na wapo waliobeba za kiukanda lakini pia wapo waliobeba za kinchi na wapo waliobeba hatima za kimkoa, kijiji, kiukoo na kifamilia.
Ili ujue hatima yako ni ya ukubwa gani basi mambo utakayoyafanya kiwepesi sana yaani bila kutumia nguvu utaona yanaenda yanafika kwenye ngazi fulani ila utakapotaka uvuke hiyo ngazi uende ngazi nyingine utaona unatumika nguvu kubwa sana lakini matokeo yake hayawi kama pale awali ambapo ulikua hautumii nguvu nyingi ila mambo yalikua yanaenda parefu, hapo unatakiwa ujue kwamba wewe ukubwa wa hatima yako mwisho wake ni hapo.
Na hapa najua umeanza kunielewa pia ninaposema kwenye hatima yako ndiko kuliko na bahati yako na pindi utakapoigundua hatima yako na kuifuata ile njia inayoelekea huko basi moja kwa moja utaanza kuona wepesi wa mambo katika upande wa umiliki wa fedha na Mali.
Kwahiyo kumbe mateso ambayo watu wengi wanayapata kwenye upande wa kifedha huwa sababu moja wapo ni kuishi maisha yaliyo nje ya hatima zao na hii hufanya watumie nguvu sana kwenye swala la utafutaji huku wakiambulia kidogo kisicholingana na nguvu walizotumia.
Na unakutana na mtu anasali sana lakini bado mambo hayakai kwenye line, na hii sio kwasababu maombi yako hayafiki kule lahasha maombi yako yanafika ila nimekwambia kila roho iko na codes na hizi codes ndio hatima yako iko humo ndani na Kimsingi ulimwengu wa juu haukutambui wewe kwa sura na umbo lako la damu na nyama ila unakutambua wewe kwa codes zilizopo rohoni mwako, kwahiyo unavyoomba ile mitetemo inaenda moja kwa moja hadi kwenye ule mfumo nyota wa asili yako na majibu yanaporudi yanarudi kwakufuata ile code ambayo ipo ndani ya roho zako kwa maana hiyo kama maombi ni kubarikiwa kwenye utafutaji wako baraka itaongezwa kwenye ile hatima iliyopo ndani yako.
Kwahiyo ikiwa wewe hatima yako ni udaktari halafu ukashindwa kuifuata hatima hiyo na ukaamua uende upande mwingine labda wa ujenzi na mambo yakakuwia magumu huko hadi kufikia hatua ya kupiga goti chini ili ujiungamanishe mitetemo ya mfumo nyota ya asili yako basi kuwa na hakika kwamba maombi yako yatafika na majibu yatarudi ila wewe utakua unapishana mwenyewe, yenyewe yanaenda kwenye afya wewe upo kwenye ujenzi.
Sasa hili ndio lengo la uumbaji, ni kwamba roho ilitengenezwa kwa codes na kila kitu kikawa kimewekwa ndani yake kisha unaletwa hapa duniani na unapumbazwa na mambo ya dunia hadi unasahau roho yako imebeba kitu gani maalumu na chaupekee ambacho unatakiwa kukifanya ili uweze kuongeza nguvu za mitetemo chanya itakayosaidia kuifanya dunia kuwa sehemu salama.
Na ukumbuke kwamba kwenye kila hatima iliyopo ndani ya mtu huwa imewekwa na deadline yake na hiyo deadline ikifika basi muhusika anarudi kwenye ulimwengu wa asili yake yaani anakufa kama mnavyosemaga.
Sasa mpumbazo huu wa dunia ukikukumba kwa kiasi kikubwa na ikapelekea ukaenda hadi siku ya deadline yako, basi hapo ndio utakua upande wa zile mbegu ambazo si bora na mbegu ambayo si bora huwa mkulima anakua na option mbili either aitupe au aipe nafasi ya pili.
Ikitupwa haitoonekana tena shambani milele na milele ila ikipewa nafasi ya pili basi mkulima atajaribu kuipanda tena ili aone kama italeta matunda au laa na ndio hapa Sasa unakutana na roho ambazo zipo kwenye miili ya watu ila roho hizo zilishawahi kuwa hapa duniani hapo kabla (watu wenye roho za namna hii wapo wengi tu).
Ngoja leo niishie hapa kwanza ila nimeanzia huku mbali kidogo ili nitakapounganisha ili niweze kukuelezea ni kwanamna gani dunia ni uwanja wa vita za hatima uweze kunielewa vizuri.
Kama kichwa cha habari kinavyosema kwamba dunia ni uwanja wa vita za hatima kwahiyo kila mtu ambae yuko hapa duniani anapaswa kujua kwamba yuko vitani na swala la kushinda au kushindwa ni juu ya mtu mwenyewe.
Sasa iko hivi...
Kimsingi ni kwamba kila mwanadamu ambae yuko kwenye hii dunia hayupo hapa kwa bahati mbaya na inawezekana wazazi waliomzaa mtu huyo wanaamini wamemleta huyo mtu hapa duniani kibahati mbaya ila kiroho hakuna kitu kinachoitwa bahati mbaya.
Maadam umezaliwa na uko hapa duniani basi kaa ukijua kuna mission unatakiwa uitimize na hii mission ndio ambayo tunaita hatima na pindi utakapoitimiza mission hiyo basi hapo ndio utakapopata uhuisho wa roho yako na kuifanya iwe hai milele na roho ambayo iko hai ndio roho ambayo husikia inaposemeshwa na ndio maana katika asili za kiafrika hasa hapa nyumbani Tanzania unakutana na kitu kinaitwa mizimu.
Sasa mizimu ni nini? Mizimu ni roho ambazo ziliishi kwenye milli ya watu fulani kwa uadilifu kwa maana ziliweza kujua zipo hapa duniani kwa lengo gani yaani hatima yao na wakapigana vita ya kuiendea hiyo hatima na wakafanikiwa kwa kiasi kikubwa na pindi deadline yao ya kuishi hapa duniani ilipofika zile roho zao ziliweza kuuhishwa na kupata uzima wa milele.
Kwahiyo Sasa katika ile mitetemo ya mfumo nyota ya koo na koo ukiweza kujiungamanisha kiroho na roho za babu ambao unawajua walikua manguli katika upande wa kutibu au kwenye jambo lolote lile ambalo lilikua hatima ya babu huyo ila ilimradi tu uwe na uhakika kwamba alifanya kweli makubwa na sifa zake hadi leo bado zipo hapo kijijini basi ukijiungamanisha tu na roho za watu wa namna hii huwa zinasikia na zinatoa majibu papo kwa hapo.
Nimesema uwe na uhakika kwasababu usije ukaenda kujiungamanisha na mtu ambae huna uhakika nae na ukaenda kuvaa roho za ajabu zikakutesa kwenye maisha yako na hapa ndipo ambapo watu wengi wanachukia haya mambo ya mizimu kwasababu huwa ni ngumu kujua babu yako mzaa babu yako alichokifanya kama kilisaidia kuongeza positive energy hapa duniani au laa (hapa nitapazungumzia vizuri huko mbele na utajua kwanini watu wanakimbilia kwa Yesu au Muhammad huku wakiacha mizimu ya babu zao kule kijijini).
Kwasasa turudi hapa kidogo...
Kikawaida binadamu huwa yuko na pande kuu mbili yaani ya damu na nyama na ya kiroho.
Upande wa kiroho ndio Upande ambao umembeba mtu halisi na ndio upande ambao unamuunganisha mtu na ulimwengu wa asili yake na upande huu huu unapokuwa hapa duniani huwa unatumika kama redio call na kwanini kama radio call basi nitakwenda kukuelezea hapo mbele kidogo. Na upande wa damu na nyama ndio upande ambao unamuunganisha mtu na ulimwengu huu wa vita za hatima.
Wakati mtu anapozaliwa huwa anakua anaishi zaidi kwenye ulimwengu wa kiroho kuliko ulimwengu huu wa damu na nyama ila kadri anavyokua na kujifunza mambo mapya ile mitetemo yake ya ulimwengu wa asili yake inapungua na ya ulimwengu huu inaongezeka hadi kufikia kwenye ukubwa toshelezi na hapa ndio mtu anaanza kuishi maisha ya ulimwengu huu wa damu na nyama na kusahau namna ya kuishi ulimwengu wa kiroho.
Na kutokana na kwamba binadamu anaishi zaidi katika ulimwengu wa damu na nyama kuliko ulimwengu wa kiroho hii imefanya wengi wetu tushindwe kuelewa lengo na dhumuni la sisi kuwa hapa duniani na badala yake tunaishi kulingana na mfumo wa kidunia na kushindwa kuelewa hatima zetu ni nini.
Na kitu cha kikuu na chaumuhimu zaidi kuhusu hatima ni kwamba kwenye hatima yako ndiko kuliko na bahati yako na vitu vyote ambavyo unapaswa kuvimiliki hapa duniani vipo kwenye hatima yako.
Kwahiyo watu wote ambao wanaziendea njia za hatima yao iwe kwa kujua au kwakutokujua huwa hawahangaiki kwenye swala la fedha kama ambavyo watu wanaoishi kwenye maisha yaliyo nje ya hatima zao hufanya.
Na ninaposema hatima kuna watu wanadhani nazungumzia kitu fulani ambacho ni maalumu sana yaani kitu ambacho hakiwezekani kugundulika kirahisi raising hivi, ila naomba nikutoe wasiwasi na nikwambie tu kwamba hakuna umaalumu wowote kwenye hatima kwasababu hatima ni mambo yote ambayo yanaweza kufanyika hapa duniani ili kuongeza nguvu chanya na kuifanya dunia iwe sehemu salama.
Kwa maana hiyo kuna watu hatima zao ni kuburudisha na kuna watu hatima zao ni kuvumbua mambo kadha wa kadha na kuna watu hatima zao ni kutibu watu wengine na kuna watu hatima zao ni kufundisha mambo mbalimbali na kadhalika.
Na ili uweze kufikia hatima yako lazima upite kwenye njia fulani na hiyo njia ndio huwa tunaiita kipawa au kipaji.
Ndio, ni kipaji kwahiyo wala usishtuke kwasababu hata wewe unachokipaji ambacho ukikitumia kitakupeleka moja kwa moja kwenye hatima yako na mara tu utakapofika kwenye hatima yako basi watu wote watajua kwamba yupo au alikuwepo mtu fulani ambae alifanya makubwa sana kwenye mambo haya ya burudani hasa upande huu wa mpira na mtu huyo aliitwa Leonel Messi au Christiano Ronaldo.
Au alikuwepo mtu ambae alifanya makubwa sana kwenye mambo haya ya uvumvuzi wa mambo ya kisayansi ambae aliitwa Isaac Newton.
Au alikuwepo mtu ambae alifanya makubwa sana kwenye haya mambo ya muziki wa rege ambae aliitwa Bob Marley.
Au alikuwepo mtu ambae alifanya makubwa sana kwenye upande wa mashoati na movie za kupigana za karate aliitwa Blue Lee.
Kwahiyo hii inakwenda zaidi na zaidi na kuwafikia vizazi na vizazi huku wakiishi na kuutukuza ufalme wako kwenye upande huo wa hatima yako bila kujali mwaka ambao deadline yako ilifika na wewe kurudi kwenye ulimwengu wa asili yako huku roho yako ikiuhishwa na kupata uzima wa milele.
Na lazima ujue pia kwamba ukubwa wa hatima baina ya mtu na mtu huwa umetofautiana yaani kuna watu wamebeba hatima za kidunia ila wapo waliobeba hatima za kibara na wapo waliobeba za kiukanda lakini pia wapo waliobeba za kinchi na wapo waliobeba hatima za kimkoa, kijiji, kiukoo na kifamilia.
Ili ujue hatima yako ni ya ukubwa gani basi mambo utakayoyafanya kiwepesi sana yaani bila kutumia nguvu utaona yanaenda yanafika kwenye ngazi fulani ila utakapotaka uvuke hiyo ngazi uende ngazi nyingine utaona unatumika nguvu kubwa sana lakini matokeo yake hayawi kama pale awali ambapo ulikua hautumii nguvu nyingi ila mambo yalikua yanaenda parefu, hapo unatakiwa ujue kwamba wewe ukubwa wa hatima yako mwisho wake ni hapo.
Na hapa najua umeanza kunielewa pia ninaposema kwenye hatima yako ndiko kuliko na bahati yako na pindi utakapoigundua hatima yako na kuifuata ile njia inayoelekea huko basi moja kwa moja utaanza kuona wepesi wa mambo katika upande wa umiliki wa fedha na Mali.
Kwahiyo kumbe mateso ambayo watu wengi wanayapata kwenye upande wa kifedha huwa sababu moja wapo ni kuishi maisha yaliyo nje ya hatima zao na hii hufanya watumie nguvu sana kwenye swala la utafutaji huku wakiambulia kidogo kisicholingana na nguvu walizotumia.
Na unakutana na mtu anasali sana lakini bado mambo hayakai kwenye line, na hii sio kwasababu maombi yako hayafiki kule lahasha maombi yako yanafika ila nimekwambia kila roho iko na codes na hizi codes ndio hatima yako iko humo ndani na Kimsingi ulimwengu wa juu haukutambui wewe kwa sura na umbo lako la damu na nyama ila unakutambua wewe kwa codes zilizopo rohoni mwako, kwahiyo unavyoomba ile mitetemo inaenda moja kwa moja hadi kwenye ule mfumo nyota wa asili yako na majibu yanaporudi yanarudi kwakufuata ile code ambayo ipo ndani ya roho zako kwa maana hiyo kama maombi ni kubarikiwa kwenye utafutaji wako baraka itaongezwa kwenye ile hatima iliyopo ndani yako.
Kwahiyo ikiwa wewe hatima yako ni udaktari halafu ukashindwa kuifuata hatima hiyo na ukaamua uende upande mwingine labda wa ujenzi na mambo yakakuwia magumu huko hadi kufikia hatua ya kupiga goti chini ili ujiungamanishe mitetemo ya mfumo nyota ya asili yako basi kuwa na hakika kwamba maombi yako yatafika na majibu yatarudi ila wewe utakua unapishana mwenyewe, yenyewe yanaenda kwenye afya wewe upo kwenye ujenzi.
Sasa hili ndio lengo la uumbaji, ni kwamba roho ilitengenezwa kwa codes na kila kitu kikawa kimewekwa ndani yake kisha unaletwa hapa duniani na unapumbazwa na mambo ya dunia hadi unasahau roho yako imebeba kitu gani maalumu na chaupekee ambacho unatakiwa kukifanya ili uweze kuongeza nguvu za mitetemo chanya itakayosaidia kuifanya dunia kuwa sehemu salama.
Na ukumbuke kwamba kwenye kila hatima iliyopo ndani ya mtu huwa imewekwa na deadline yake na hiyo deadline ikifika basi muhusika anarudi kwenye ulimwengu wa asili yake yaani anakufa kama mnavyosemaga.
Sasa mpumbazo huu wa dunia ukikukumba kwa kiasi kikubwa na ikapelekea ukaenda hadi siku ya deadline yako, basi hapo ndio utakua upande wa zile mbegu ambazo si bora na mbegu ambayo si bora huwa mkulima anakua na option mbili either aitupe au aipe nafasi ya pili.
Ikitupwa haitoonekana tena shambani milele na milele ila ikipewa nafasi ya pili basi mkulima atajaribu kuipanda tena ili aone kama italeta matunda au laa na ndio hapa Sasa unakutana na roho ambazo zipo kwenye miili ya watu ila roho hizo zilishawahi kuwa hapa duniani hapo kabla (watu wenye roho za namna hii wapo wengi tu).
Ngoja leo niishie hapa kwanza ila nimeanzia huku mbali kidogo ili nitakapounganisha ili niweze kukuelezea ni kwanamna gani dunia ni uwanja wa vita za hatima uweze kunielewa vizuri.