Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Mkuu wangu JokaKuu, msome hapa chini kiongozi wenu Lema anawatoa wasiwasi kuhusu Zitto Kabwe.


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimewatoa hofu wanachama wake mkoani Shinyanga kikidai propaganda zinazoenezwa na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Bw. Zitto Kabwe, anayedai chama hicho kimepoteza mwelekeo si za kweli bali ni uongo.Mbunge wa Arusha Mjini ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Taifa, Bw. Godbless Lema, aliyasema hayo hivi karibuni mkoani Shinyanga kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Mahakama ya Mwanzo.Alisema chama chao bado kipo imara na hakitagawanyika kama inavyodaiwa na Bw. Kabwe ambaye CHADEMA kilimfukuza katika chama baada ya kukisaliti hivyo kukiuka Katiba ya chama hicho."Ndugu zangu wana Shinyanga, CHADEMA tupo imara na tutaendelea kuwa imara hadi tukamate dola na kuwakomboa Watanzania ambao wanateseka tangu tupate uhuru."Zitto hana ubavu wa kukigawa chama chetu kama anavyofikiri na kuamini...anahangaika bure, alitaka kukiua tukamshtukia na mimi ndiye mtu wa kwanza kubaini njama zake na wenzake akiwemo Samson Mwigamba na Profesa Kitila Mkumbo; hivyo hawatubabaishi kwa lolote,"-alisema.Bw. Lema aliongeza kuwa, Bw. Kabwe alikuwa chanzo cha kufifisha ushindi wa CHADEMA katika baadhi ya majimbo katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 baada ya kutoa taarifa za uongo kwa wasimamizi wa uchaguzi katika majimbo ya Katavi, Musoma Vijijini na Singida Mjini na kusababisha wagombea wa CCM wapite bila kupingwa.
 
.............?
Nguruvi nilisema wewe mzito sana kusoma kitu ukaelewa. Nimesema Maendeleo ya watu hupimwa kwa HDI sikusema HDI huonyesha Inequality. isipokuwa Inequality ina impact kubwa sio kwa kundi la watu bali hata uzalishaji wao. Ndio maana hutoa mifano kama hiyo ya Shinyanga na hata marekani wanaweza zungumzia tofauti baina ya Michigan na California kwa kutumia vigezo.

Hivyo ujue tofauti za maelezo yangu kwanza, kuna inequality katika mfumo wetu juu ya Matajiri na Maskini kiasi kwamba maskini wanazidi kuongezeka, HDI haipimi inequality hiyo wala haipimi sababu haswa zilizosababisha nchi yetu kuwa na kiwango cha chini iwe hata Elimu au Afya bali inaweza onyesha results. Tanzania tuna sababu zetu tofauti na Uganda na zipo nchi nyingine HDI ipo chini kwa sababu ya vita. Hivyo, maudhui ya hoja zangu ni kutazama sababu.

Swala la Zitto kuwa Supreme nalisoma kwenu tu kwa sababu ya maelezo yake lakini kwa vitendo kusema kweli Chadema kama chama ni supremacy fulani yaani wapo watu hawaguswi. Kuna kundi fulani hilo usiliseme vibaya ukianza tu unatupwa nje. Zitto hajamfukuza mtu chama wala hajaonyesha kutoa amri au kuyatumia vibaya mamlaka yake. Tunayaona kwa wengine na sio mara moja.

Sababu gani mnamwita Supreme ni kwa sababu amechukua Urais wa ACT. Basi hakuna sababu nyingine yaani mtu alotaka kuwa na dream yake juu ya kuanzisha chama chenye kufuata Itikadi ya Mwalimu kafanmikiwa imekuwa taabu kama kawaida ya mwafrika. WIVU na MAJUNGU ili asipatikane mtu wa kupanda juu zaidi yao...Vita ya kaa ndani ya kapu la mvuvi.
 

Alinda:

Ufafanuzi: nadhani katika posti yangu nimesema unachukia, sijasema unamchukia mkenya au unawachukia wakenya. Kuchukia na kuwachukia ni vitu viwili tofauti japokuwa shina la neno ni moja. Kuna watanzania wengi wanachukia nafasi za kazi kuchukuliwa na wageni lakini hawachukii wageni wenye nafasi hizo.

Kuhusu suala lako la pili, anayepaswa kutoa majibu kamili ya posti no. 870 ni Nguruvi3. Huyo ndie ulimwandikia (addressee). Sisi wengine kama wachangiaji tuna ruhusa ya kusoma, kujibu, au kuchomekea tu. Nimechomekea tu.

Hili kukutendea haki, itabidi niendelee kujibu no. 837 (Iliyopo chini). Naona kuna vitu vyenye uzito kwa upande wako ambavyo niliviacha.



Kwa maoni yangu binafsi. Watanzania wote tunawajibika kwa umasikini wa watanzania wengine. Kama Mwingereza anatoa sehemu ya kodi yake hili nchi zingine masikini za Ulaya ziweze kuendelea, kwanini mchagga asiwe sehemu ya maendeleo ya msukuma au msukuma kuwa sehemu ya maendeleo ya mchagga au mhehe?

Birth rate ya watu masikini ni kubwa kuliko ya watu matajiri. Na kwa kutumia demokrasi tunayotumia, wanasiasa wataomba kura za masikini. Je unataka wanasiasa waambie nini masikini? Unataka waambie nyie sio wacharikaji. Mkichakarika kama wenzenu, mambo yatakuwa mswanu.
 

Mkandara:

Kuna watu wako desparate ya kuwa vyama viwili vikubwa vya upinzani kama USA na UK. Hivyo kwao ni muhimu kwa vyama vya upinzani kuwa pamoja hata kama watu wako incompatible.

Mchambuzi ni CCM lakini kwa sababu ana mawazo ya kuona chama kikubwa cha upinzani kitakachokistua chama chake, anaona vibaya Zitto kuhama CDM. Anashindwa kusafisha uozo uliopo CCM lakini anaona ni haki kumnyooshea vidole Zitto.

Ukweli wa mambo hakuna watu wanafiki kama waliobaki CCM.
 
Haswaa mkuu unajua hawa wenzetu wagumu sana kuelewa mtu anapolalamikia mfumo wanashindwaje kuutazama mfumo badala yake wanatatafsiri maneno ya mtu kwa sababu zao....

Mimi nimesema humu mengi juu ya Barricks haina maana Barrick ndio wezi ama ndio wanatufanya tuwe maskini bali Mfomo uliopo ndio tunauzungumzia. Tukizungumzia mfumo unaowezesha tuwe na Matajiri wachache na kujenga maskini wengi kama Pyramid haina maana tunawachukua Matajiri laa hasha bali tunatazama mfumo. hao wageni sio kosa lao bali mfumo ndio umetoa mianya hiyo na kadhalika, tunauchukia mfumo sio walowezeshwa. Na ndiyo ilivyo hata katika Usemi wa Zitto lazima uwe na mifano hai kuonyesha mfumo mbovu na kwa hofu hii ya kutawaliwa kimawazo ndio maana tunashindwa hata kuelewa kwa nini tanzania Maskini.

Mfano wa Zitto is exactly unaonyesha Shinyanga sio maskini lakini watu wake maskini, tumefanya hivyo kwa tanzania na Maleysia haina maana Maleysia wanahusika na kutofanikiwa kwetu. Bali sisi tuna tatizo la mikataba na ufisadi ambao imefikia kutungiwa sheria kali dhidi ya utafiti juu ya upatikanaji wa habari mtandaoni na kuua Access to information and privacy act, kwa sababu tunaamini katika Siri hata majumbani
 
Asiyetaka kuelewa maana kamwe hataweza kuelewa maana. Nisome hapo juu kwa Nguruvi pengine unachukua japo moja.
 
Mkuu , hayo unayosema ndiyo yangewezesha taifa kusongambele.

Shinyanga na Mwanza wakifanikiwa taifa ,imefanikiwa.

CCM haijawezakutumia fursa hizo, Supreme leader anaona wananchi wa K’njaro na Arusha ndiotatizo


Frustration zake haziwezi kuvumiliwa akitumbukiza chuki naubinafsi. Zitakemewa.
Siasa za ulaghai hapana
 
Katika bandiko 862 nimemuelezea Mkandara kama disingenuous person.

Katika bandiki# 872 Mag3 kameuleza kama kinyonga. Nadhani mnaweza kuona picha halisi
 
Zitto blames Wachaga for wasukuma's impoverishment. Anabagua na kuchonganisha makabila. Nyerere didn't do that, instead he strived to Unite all ethnic groups against one dominant force that was exploiting and dehumanizing Africans.

There you go buddy. People are united when there's a common issue or enemy. Nyerere managed to unite us because all tribes were in the same boat. We were all under colonial rule.

Now that we are free, we should start dealing with domestic dramas. Don't you think so?
 
Swali Mkandara anajificha fichani hili:

Kulikuwa na mantiki gani kwa supreme leader kulinganisha Kilimanjaro (namba 9 kimaendeleo), Arusha(namba 7) na Shinyanga/Mwanza?


Swali hili lina maana kubwa, kwanza, ukisoma maelezo ya Mkandara ''Shinyanga wanachangia Zaidi hawapewi stahiki, Kilimanjaro wanachingia kidogo wanapata stahiki''

1 Hayo si maelezo ya Zitto, ni maneno ya Mkandara ambaye katika bandiko #885 ametuhumu watu kutoa tasfiri zao, yeye anatoa yake, amejipa haki hiyo. Hapa anaonyesha ukinyonga aliousema Mag3 na disingenuous isiyohitaji cert. kuibaini

2. Katika aya ya pili, Mkandara anaonyesha kkuna ‘inequality' inaweza kuleta social tension, moral question, fairness na social injustice. Katika hali ya unafiki amesahau katika aya hiyo ameilaumu serikali kwa kuelekeza pesa kwa ziara za rais na wabunge. Ni unafiki mkubwa sana ,Huwezi kuilamu serikali kwa kutumia mikoa ya kaskazini

Huwezi kutoa mfano wa Kilimanjaro/Arusha Vs Mwanza/Shinyanga kisha ukaongela social injustice, inequality na moral question. Maana ya Mkanadara kama ilivyo ya Zitto ni kuwa mikoa ya kaskazini inapata Zaidi na hivyo kuleta inequality

Katika hali ya unafiki ule ule wa supreme, Mkandara anailaumu serikali, huku akionyesha wazi upendeleo wa mikoa ya K'njaro/Arusha

Swali la pili
Mkandara tuonyeshe stahiki wanayopata watu wa K'njaro ambayo watu wa Mwanza na Shinyanga hawapati.

Huwezi kusema ‘stahiki' bila kuonyesha ni ipi. Huo ndio uchochezi kama ule wa kusema K'njaro/Arusha zinachangia kidogo na Shinyanga Zaidi, kimaendeleo Shinyanga ipo nyuma wa Supreme leader

Swali la tatu
Kulikuwa na mantiki gani hasa ya kuchagua mikoa miwili isiyokuwepo katika 6 za mwanzo za maendeleo.

Zitto na Mkandara mnaangalia vigezo gani hadi kufikia hatua hiyo.


Swali la nne, ni mikoa gani ipo katika 5 bora, na inatofautianaje na Shinyanga/Mwanza ?
 
Mkandara , kama kuna kundi lisiloguswa, una jukumu kama raia kuonyesha matatizo yaliyopo na wanajamvi watajumuika nawe.

Nakushauri uanzishe uzi kama huu ili tuchangie huko. Sisi tumeonyesha mfano kuwa pale tusipokubaliana napo tutaweka wazi. Hivyo una nafasi ya kufanya hivyo bila ku-adulterate mjadala, kuupindisha ili kuondoa ukweli unaomkabili supreme


Supreme leader anawajibika kwa kauli zake za uchochezi, za kutaka kuvuruga taifa.

Tunajua historia yake ni kuleta sintofahamu ndani ya vyama vya siasa. Inapovuka mipaka na kuingia katika utaifa, hatutakaa kimya.

Nawe pia usikae kimya kama wapo wanaotenda kinyume. Lakini pia usitake ku insinuate habari zako katika uzi usiohusika


Pili, kumwita supreme leader siyo sisi. Chama chake kinamtambua kama kiongozi mkuu.

Unless uje na tafasiri nyingine supreme leaderni tafsiri halali.

Ni kama vile Kim II sung(Grate leader), Kim Jong (Dear leader).

ACT wana mfumo kama huo, ambako Anna ni Mwenyekiti na Zitto ni supreme leader.

Kwa maneno mengine, ni kama Iran ambako kuna Rais wa nchi na kiongozi mkuu wa nchi kama Khomeni au Khemenei


Neno supreme leader lina maana kiongozi mkuu. La sivyo tuambie kiongozi mkuu kwa lugha ya kigeni anaitwa nani, nasi tutaheshimu

Supreme leader anaweza kuota ndoto zote bila kikwazo aukizuizi.

Ndoto zake zisielekee kuligawa na kulivuruga taifa kwa misingi ya ukanda.

Huko tutaingilia kati ndoto hizo kwani zitakuwa si ndoto bali njozi.

Tunajua njozi zinaweza kuwa na matokeo mabaya na hatutapenda matokeo hayo katika taifa letu.

Anaweza kufanya siasa hizo anakojua si Tanzania. Hatuta kaa kimya kamwe!


Chama cha supreme hakiwezi kulinganishwa na maono ya Nyerere.Tungekuomba umwache mzee Nyerere apumzike kwa Amani. Nyerere alipigania taifa,supreme anapigania kugawa nchi. Usifaninishe kichuguu na mlima Kilimanjaro

Hatuna wivu wala majungu, maneno anayesema mwenyewe. Waraka waliandika wenyewe, na sasa yupo katika rekodi akieneza siasa za kushambulia mikoa ya kaskazini dhidi ya kanda ya ziwa. Hatuwezi kukaa kimya wananchi wakichonganishwa na genge dogo lisilifokia watu 10 lenye kueneza uongo, uzushi na unafiki. Hatutakaa kimya asilani
 
Mkuu Kwani kwasasa hivi hali iko vipi? Hebu fafanua
 
Ingawa ili swali siyo langu lakini na mimi naomba kujazia kiduchu.

Mkuu naona umeamua kumuwekea Zitto maneno mdomoni kuwa kachagua mikoa miwili tu kuitaja Arusha na Kilimanjaro siyo kweli Zitto kaitaja mikoa mingi tu msome.

Zitto.

Tanga ni ya 8 katika kuchangia Pato la Taifa. Pia ni mkoa wa 8 kwa kiwango cha maendeleo ya watu wake.Mikoa yenye Maendeleo zaidi ni Arusha, Kilimanjaro na Dar es Salaam. Hata hivyo Kilimanjaro ni ya 9 katika kuchangia Pato la Taifa na Arusha ni ya 7.Mikoa iliyo nyuma zaidi kimaendeleo nchini ni Kigoma, Singida, Dodoma, Kagera na Tabora. Hata hivyo Tabora ni mkoa wa 10 kwa kuchangia katika Pato la Taifa na Kagera ni mkoa wa 11 katika GDP.Mikoa yenye mchango mdogo zaidi kwenye Pato la Taifa ni Pwani (1.85%), Lindi (1.89%) na Singida (1.92%). Hata hivyo Lindi inashika nafasi ya 9 kwa Maendeleo, juu ya Shinyanga inayochangia 6% katika GDP.Dar inaongoza kwa kuchangia Pato la Taifa ambapo mchango wake kwenye pato la Taifa ni 16.9%. Inafuatiwa na Mwanza [kabla haijagawanywa] 9.2%, Mbeya 7.3%, Shinyanga 6% na Iringa 5.3%. Hata hivyo Shinyanga ni mmoja wa mikoa yenye umasikini wa kutupwa licha ya kuwa namba 4 katika kuchangia Pato la Taifa.Ndio maana ni lazima kubomoa mfumo wa sasa wa uchumi. Huwezi kuwa na mkoa unashika namba 5 kuchangia Pato la Taifa lakini unashika namba 16 kati ya mikoa 21 kwa maendeleo ya watu. Shinyanga ina migodi 2 ya dhahabu na migodi 2 ya Almasi. Shinyanga ina Ng'ombe na Pamba.Shinyanga tarehe 17 Aprili, tujadiliane jinsi ya kufanya mapinduzi ya kiuchumi mkoani mwenu.

Cc; Mkandara Barubaru
 
Last edited by a moderator:
Kuna uwezekano katoa clarification huko face book

Mkandara atakuwa shahidi mzuri tu kwasababu kuanzia jukwa lasiasa hadi hapa, yeye ni kinara wa hoja husika.

Msome hapo juu, '' Shinyanga inachangia Zaidi haipati stahiki, Kilimanjaro inachangia kidogo inapata stahiki''


Mwenzako team Adharusi kaja na data kabisa

Nashangaa hukuona hayo yote. All in all,tunajua alifanya shambulio la kisiasa dhidi ya mikoa ya kaskazini
 
Mkuu.

Zitto kaamua kuwa huru,ni ukweli mtupu kwamba Shinyanga haistahili kuwa ilivyo Leo, na hapa hakuna upinzani ulioguswa bali serikali ya CCM inakumbushwa kujitafakari upya la sivyo yale ya Mtwara yanaweza jitokeza mikoa mingine kama Tanga na Shinyanga.
 
Hiki ndicho alichokisema Zitto inaonekana hata wewe ukumsililiza bahati nzuri hii hotuba yake ilikwa live Radio Free na huu uzi upo JF wala siyo Facebook pita na majukwaa mengine mkuu.

Nadhani umeona Zitto alivyotambaa kwenye hotuba yake kataja mikoa mingi tu tofauti na wewe umechagua mikoa miwili Arusha na Kilimanjaro.

Vipi kuhusu kuitaja Dar es Salaam alikuwa anatoa shambulio kwa Wazaramo?
 
Last edited by a moderator:

Mkuu toa hotuba aliyotoa kule kwa wasukuma, achana na hotuba za facebook na redioni.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu toa hotuba aliyotoa kule kwa wasukuma, achana na hotuba za facebook na redioni.
Mkuu wakati mwingine tumia akili yako aliyekupa Mungu siyo kila anachosema Nguruvi3 wewe unafuata tu mkuu.

Unataka hotuba gani zaidi ya hii? Hii hotuba hii mbona tumeijadili sana jukwaa la siasa kabla ya kuja kujadiliwa hapa.

Nendeni jukwaa la siasa mtakakutana na huu uzi haya maneno Zito kayaongelea Mwanza viwanja vya Furahisha kama wewe unayo hotuba ingine ya usukumani tofauti na hii tuwekee mkuu.

Masikini kumbe hata hujui hotuba ya Zitto kule Mwanza viwanja vya furahisha ilikuwa inarushwa live na Radio Free, hautaki hotuba ya kwenye radio unataka hotuba gani.

Wakati mwingine kuwa huru kifikra utajifunza mengi mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Haya ni maneno ya Zitto Kabwe katika facebook yake tarehe 5 April..

Dar inaongoza kwa kuchangia Pato la Taifa ambapo mchango wake kwenye pato la Taifa ni 16.9%. Inafuatiwa na Mwanza [kabla haijagawanywa] 9.2%, Mbeya 7.3%, Shinyanga 6% na Iringa 5.3%. Hata hivyo Shinyanga ni mmoja wa mikoa yenye umasikini wa kutupwa licha ya kuwa namba 4 katika kuchangia Pato la Taifa.

Ndio maana ni lazima kubomoa mfumo wa sasa wa uchumi. Huwezi kuwa na mkoa unashika namba 5 kuchangia Pato la Taifa lakini unashika namba 16 kati ya mikoa 21 kwa maendeleo ya watu. Shinyanga ina migodi 2 ya dhahabu na migodi 2 ya Almasi. Shinyanga ina Ng'ombe na Pamba.
Shinyanga tarehe 17 Aprili, tujadiliane jinsi ya kufanya mapinduzi ya kiuchumi mkoani mwenu



Na hapa ni katika faceboo ya Zitto ya tarehe hiyo 5. April
Mikoa yenye Maendeleo zaidi ni Arusha, Kilimanjaro na Dar es Salaam. Hata hivyo Kilimanjaro ni ya 9 katika kuchangia Pato la Taifa na Arusha ni ya 7.
Ritz kinachojadiliwa ni hicho kipengele ambacho Zitto aliamua kwa makusudi kukichomoa katika report kwa chuki zake kwa watu wa Kili/ARusha.
Kama hisinge kuwa chuki basi Mkoa wa kujadiliwa ulikuwa ni Lindi maana ni mkoa ambao unachangia kidogo sana katika pato la taifa lakini ni mkoa wa 9 kimaendeleo. Sasa tujiulize kwanini Lindi. Lakini si mikoa ambayo Kil/Arusha maana hii mikoa hiko katika mikoa 10 ya uchangiaji wa pato la taifa.
 
Last edited by a moderator:
Alinda.

Bahati nzuri hayo maneno mimi binafsi nimeyasikia kwa masikio yangu alivyokuwa anahutubia Mwanza kwenye viwanja vya furahisha kupitia Radio Free.

Nadhani hii hotuba unaweza kuipata pia kwenye youtube au audio ipo.


Halafu kwa nini nyie mmeamua kuchagua mikoa ya kujadili wakati mnaacha mkoa wa kwanza Dar es Salaam na mikoa mingine.

Labda nikuulize hii kauli ya Zitto tunaojadili hapa aliongelea wapi? Maana wewe unasema tujadili aliyaoandika Facebook na Twitter jamaa zako hawataki tujadili ya huko ndiyo maana mimi nikaja ha hotuba ya Furahisha Mwanza.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…