Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Nadhani sasa unataka kunishawishi kwa nguvu nipuuze mabandiko yako...! Hoja kuu hapa ni Chama cha ACT-Mpini wa CCM kumaliza upinzani. Sub-hoja ni Kauli ya SL kuligawa taifa kwa kuwachonganisha watanzania aliyoitoa kanda ya Ziwa.
Hizo hoja mnapanga nyie tu mkuu Nguruvi3 anasema toka tarehe 5 anajadili kauli ya Zitto mimi kuhoji imekuwa kosa unaniwekea mipaka daah!!! Mkuu naomba unipuuze tu hamna shida.
 
Last edited by a moderator:
Gamba la Nyoka, naomba nikupe ushauri kidogo tu...kabla hujachangia jaribu kupitia michango mbambali ya nyuma ujue tulitoka wapi, tuko wapi na tunaelekea wapi. Ndio maana sisi wengine tunaonekana humu mara chache sana kwani kila nikirudi naanza kwanza kusoma michango yote iliyotangulia kuanzia siku nilipo log off...nasoma kila kitu na kila post kabla ya kuchangia . Bila hivyo mtu unajikuta unakurupuka tu na kuonekana kama laughing stock kwa kudandia treni kwa mbele. Huo ni ushauri tu, ni haki yako kuupokea au kutoupokea.

Gamba la Nyoka, kwa sasa sitakuchosha kwa maneno mengi ila baada ya tahadhari hiyo fupi naomba turudi kwenye mada, Chama cha ACT - Mpini wa CCM kumaliza upinzani! Tuendeleeee!
 
Nadhani sasa unataka kunishawishi kwa nguvu nipuuze mabandiko yako...! Hoja kuu hapa ni Chama cha ACT-Mpini wa CCM kumaliza upinzani. Sub-hoja ni Kauli ya SL kuligawa taifa kwa kuwachonganisha watanzania aliyoitoa kanda ya Ziwa.
Mkuu hebu pitia mabandiko yake uone. Amekuwa ananukuu hata yasiyohusiana na mjadala. Anafanya hivyo kwa makusudi akijua watu wataondoka kwenye mjadala halisi

Mada ipo wazi, ACT kama mpini, tumejadili kwa undani. Katika hayo, tumejadili pia kauli ya ACT kuhusu mgawanyo wa pato la taifa, maendeleo ya maeneo husika ynayotuhumiwa na jinsi kauli hiyo ilivyoleta mfarakano tena tukitumia hoja zao.
Takwimu za aina 3 zimeletwa, hakuna hata moja inayomtyetea zaidi ya kuweka ukweli wazi

Sasa watu watauliza, kwanini kauli ya supreme leader iwe ya ACT?

Jibu ni rahisi, kwa mujibu wa katiba ya ACT, Supreme leader ni nuru na taswira ya chama.

Hivyo, kwa kauli zake, msimamo wa ACT ni pamoja na matamko yake, hotuba zake, twits n.k zinazoonyesha mbinu kali za kuligawa taifa

Ukisoma uzi nilioweka hapo juu kutoka jukwaa la siasa utagundua jinsi wananchi walivyoungana bila kujali itikadi zao za aina yoyote kupinga kwa nguvu hoja ya supreme leader kuhusu mikoa ya kaskazini.

Angalia mchangiaji mmoja aliyezungumza kwa hisia sana na uchungu kutokana na maneno ya supreme leader

Unaweza kuona maneno kama makali, lakini angalia hoja na hisia zake, utagundua kaumia sana na jinsi taifa linavyoanza kumegwa katika misingi mibaya sana [
Hivyo, kuacha ACT na supreme waendelee kusambaza mbegu hii mbaya ni kuliweka taifa rehani
Tutalaumiwa na kusotwa madole na watoto au wajukuu zetu kwa kukaa kimya wakati nchi inaandaliwa maafa

Hakuna mtu anayetaka kuwa kiongozi wa taifa hili, wakati huo huo akigawa taifa vipande vipande, akionyesha chuki za wazi dhidi ya wananchi wa eneo jingine

Hali hiyo si nzuri kitaifa, kijamii na kisiasa na inabidi tuikemee

Usishangae mjadala unayumbishwa ili kuondoa focus yetu dhidi ya ACT kama mpini wa kumaliza upinzani

Wanafahamu tayari deal imeshtukiwa, sasa tunasoma vioja na viroja. Just kutuondoa katika mada

Njia ni nyepesi, ukiona kuna kuchepuka katika mada, ignore. Wanataka kutuvuta tuingie katika mtego wao

Tunasema Ney, mada ACT-Mpini wa kumaliza upinzani
 
Hivyo, kuacha ACT na supreme waendelee kusambaza mbegu hii mbaya ni kuliweka taifa rehani
Tutalaumiwa na kusotwa madole na watoto au wajukuu zetu kwa kukaa kimya wakati nchi inaandaliwa maafa

Hakuna mtu anayetaka kuwa kiongozi wa taifa hili, wakati huo huo akigawa taifa vipande vipande, akionyesha chuki za wazi dhidi ya wananchi wa eneo jingine

Hali hiyo si nzuri kitaifa, kijamii na kisiasa na inabidi tuikemee

Usishangaa mjadala unayumbishwa ili kuondoa focus yetu dhidi ya ACT kama mpini wa kumaliza upinzani
Wanafahamu tayari deal imeshtukiwa, sasa tunasoma vioja na viroja. Just kutuondoa katika mada
Njia ni nyepesi, ukiona kuna kuchepuka katika mada, ignore. Wanataka kutuvuta tuingie katika mtego wao

Tunasema Ney, mada ACT-Mpini wa kumaliza upinzani[/QUOTE]

Matusi kwa Zitto wewe unaita hisia daah Zitto anatukanwa Punguani Wahed mwenye damu ya Kirundi wewe unaita hisia...aisee!! Kweli huu mpini.
 
Last edited by a moderator:
Yes, ni mpini kwasababu wamebeba agenda za dudumizi CCM za kulimega taifa kama walivyoanza miaka michache iliyopita

Ni mpini, kwasababu badala ya ku deal na matatizo, wao wanaungana na dudumizi katika kueneza chuki za kikabila na kikanda.

Badala ya kueleza kwanini sisi ni masikini, wanaeleza jinsi wanavyoweza kuchukua majimbo ya upinzani

Badala ya kueleza kwanini mfumo huu wa kiccm haondoki licha ya taabu za wananchi, wao wanajaza wananchi hasira dhidi ya wenzao.

Leo taifa linajadili kauli za mtu mmoja badala ya matatizo yanayotukumba.

Yes, linajadili kwasababu huwezi kupuuzia unyoya ukiingia jichoni.

Ni makosa sana kwasababu mbuyu ulianza katika udogo kama mchicha.

Lumumba wapo kimyaa kwasababu kazi 'inaendelea uzuri'' waliopewa contract wanafanya vema.

Kwa mwenzetu gamba, zamani tukitumia sana msemo 'dafrao''

Baada ya kudandia kwa mbele, amekutana na hoja na hakika anaonekana ...stock
 
Adharusi, Kwanza naomba nikusahihishe kidogo, kwanza mimi ni Mag3 na si Mage3, pili si kweli kuwa takwimu kama zinajitosheleza nitazikataa eti kwa vile tu ziko kinyume na mtizamo wetu kwa Supreme Leader. Zitto nina hakika anaufuatilia uzi huu na hata si ajabu akawa moja katika wachangiaji, who knows!

Ingawa JF imeruhusu watu kuwa na IDs zaidi ya moja lakini nakuhakikishia mimi ni katika wachache ambao ID ni ile ile niliyoingia nayo JF, haibadiliki kama msimamo wangu usivyobadilika hovyo. Mimi si bendera fuata upepo, kama kuna jema nitalipokea na kulitetea na kama ni ubaya nitaukemea na kuupinga bila kusita wala kumtazama mtu usoni.

Imani yangu kwa Zitto ilianza kupotea zamani sana na rekodi ziko humu JF za mimi kuanza kutilia shaka msimamo wake kwa mambo mbali mbali toka mwaka 2009 kabla ya uchaguzi wa mwaka 2010. Kama angesikiliza ushauri wetu na kuzifanyia kazi, sidhani kama tungefika hapa tulipo wala yeye kujikuta huko alipo.

Ni ukweli ulio wazi kwamba upinzani Tanzania unataka moyo na wapo wengi waliangukia njiani. Wapo ambao bila kificho waliamua kurudi chama tawala baada ya mikikimikiki ya Upinzani kuwashinda. Wako pia ambao walikosa ujasiri huo na hivyo kwa unafiki na tamaa zao wakabaki upinzani kutumika kama mada inavyosema.

Najiuliza kwa nini mtu asubiri hadi mwaka wa uchaguzi 2010 aanzishe chama na kukiita CCJ? Kwa nini mtu asubiri hadi mwaka wa uchaguzi 2015 aanzishe chama na kukiita ACT? CCJ ilikuwa iwe mpini kwa CCM, ikazuiliwa isione hata mlango wa msajili lakini ACT, mpini wa Upinzani, ikasajiliwa bila hata kutosheleza matakwa ya katiba!

Waliokuwa waanzilishi na viongozi wa CCJ hivi sasa ni mawaziri kwenye serikali ya CCM, je waanziliashi na viongozi wa ACT wana ajenda gani? Je kama lengo lao litafanikiwa na Upinzani ushindwe kutwaa madaraka, wameahidiwa nini? Kuna maswali kibao lakini kubwa ni namna ACT inavyopewa msaada wa hali na mali na chama tawala.

Wote tumeshuhudia ACT wakiyapa majimbo yaliyoko Upinzani kipaumbele kama majimbo ambayo watafanya juu chini kuyatwaa. Tumeshuhudia wakiwaita viongozi wa Upinzani waroho wa madaraka wakiwafananisha na wasaka tonge. Tumeshuhudia wakiwaonya na kuwakataza wanachama wao kushirikiana na umoja wa Upinzani, UKAWA!

Nikikumbuka watu waliopigwa virungu na FFU wakiongozwa na Mrema wakidai mabadiliko. Nikiwafikiria waliopoteza maisha, kuumizwa, kupata vilema vya kudumu wakipigania mfumo mpya huru, wakipoteza ajira zao bila kujua wao na wapendwa wao watakula wapi, wazee wastaafu wa Afrika Mashariki wakifa bila mafao kwani zimeliwa...

Halafu miaka 25 baadaye wanatokea watu wanajidai wao ndio wanataka kuleta mabadiliko ya kweli, wanataka kula kivulini wakati wenzao walihangaika juani, wengine hawajui hata hayo mabadiliko yalikujaje, hawajawahi kuvuja hata damu hata tone, leo wanaona wao ndio zaidi, wako tayari kuwasaliti wahanga wenye makovu ya CCM, ya polisi...

Inashangaza, inasikititisha, inaudhi na inakasirisha...what the hell!
 
Last edited by a moderator:
Haya ni maneno ya Mkandara ""Bibie nina kumbukumbu nzuri tu za mjadala huu kwa sababu ilifikia tukajiuliza sababu ya Zitto kusema Shinyanga inachangia kuliko Kilimanjaro na Arusha kapata wapi takwimu. Mchambuzi akaja na za TRA kiasi hata mimi nikasema kama ndivyo itabidi tumuulize Zitto mwenyewe. Hata mimi sikuelewa lengo lake ilikuwa nini unakumbuka?

Mjadala ukaendelea, na ndipo Adharusi akaja kusema Zitto kazitoa HDR repoti ya mwaka 2014, ikawa ubishimwingine ambao umechukua sura hii, nami nikasema kama ndivyo hakuna ubaya maana kiongozi yeyote wa siasa lazima awe na vigezo kama hivi. JokaKuu akapinga akisema sawa unaweza tumia vigezo, lakini Zitto kuzitaja Kilimanjaro na Arusha alikuwa na sababu zake za kibaguzi. Au nakosea?..

Nilipochukua muda kuwasoma wote Ritz na Adharusi, nikaona maelezo yao yanafanana kabisa isipokuwa Adharusi kachukua sehemu zinazohusiana na mjadala kuelezea wapi Zitto katoa takwimu hizo. Ikawa kosa jingine kwa Zitto kutumia takwimu za HDR sio zake na ndio nikauliza kwani Mchambuzi alipotumia za TRA ilikuwa kosa? mbona mimi sikuona kosa. Na kama mnaziona takwimu hizo sio sawa basi wa kulaumiwa ni HDR sio Zitto, maana watakuwa wao ndio wamedanganya.

Sasa ukweli tumeupata na nadhani itakuwa vizuri jamani mnyonge mnyongeni laini haki yake mpeni! Msibadilishe maneno na kumzulia mtu uongo ili tu kuhakikisha ACT haipati kukubaliwa Kilimanjaro na Arusha. Maelezo ya Adharusi umeyaona ni kwamba amechukua baadhi ya sehemu lakini mfululizo wa Hotuba kamili kautoa vizuri tu Ritz maana ukimsoma Adharusi utaona hoja hazifuatani sawa akitumia neno pia akasema ambalo ni ongezeo la mwandishi wa makala hiyo ktk kumbukumbu zake, not exactly Zitto alivyosema, ni kiswahili rahisi kabisa."""
Last edited by Mkandara; Today at 17:25.



Kaka yangu Mkandara hivi mara hii umesahau ulichoandika wewe mwenyewe? nimefanya kazi kubwa ya kurudi nyuma na kuangalia ulichoandika. Na hapo chini ndo mtirirko kamili kati yako na nguvuri3 na Mchambuzi.. Na hapo kwenye nyekundu unakubalina juu ya pato la taifa. (Na kwa hili ninapenda kujipongeza kuwa kumbukumbu zangu zilikuwa sawa.)


Well, tutaviangalia vigezo hivyo hakuna shaka

Wakati tunafanya hayo, tunaomba utuambie 'Kilimanjaro kapewa na nani'' ?



 
Last edited by a moderator:
Alinda tafadhali fanya editing ili uweze kum-quote Mkandara vizuri. Samahani, maelezo ya mwanzo yanaonekana kama yako hadi pale edited by..
 
sasa mbona niliyoyasema ndio haya haya. kwanza nimetofautsha baina ya Tax na Pato la Taifa kwa ujumla wake na imedhihirisha wazi kwamba mimi nilikuwa katika mjadala huu sikutaka kuchukua maneno ya nje. Nikataka kujua Zitto na Mchambuzi wametumia vigezo gani. na kikaweza tenganisha vizuri watu mpate kufahamu kwamba Tax collection sio kitu kizima, we collect taxes toka mapato yote ya ndani na nje lakini hii ni sehemu tu ya fedha zote maana kama wewe mfanya Biashara Ulozalisha billioni 10 na kulipa tax millioni 30 zitahesabiwa zote billioni10 na millioni 30 kama Pato la Taifa. Na mwisho wa siku tumeona kwamba Mchambuzi alitumia tax collection za TRA na Zitto alitumia GDP na HDI maana kumbuka vitu hivi vina mahusiano sana japo tofauti.

kitaalam na kiuchumi penye maskini wengi kuna upungufu wa MTAJI hivyo kuathiri ELIMU, AFYA na UZALISHAJI (Maendeleo) na ndio maana mara nyingi kuna hope ya kwamba nchi maskini yenye ongezeko kubwa la GDP mara nyingi kuna trickle down kuondoa Umaskini wao na Umaskini ukiondoka elimu, Afya, uzalishaji na maisha ya watu huboreka. hii hata iwe katika maisha yetu wenyewe unapopata ajira na mshahara mzuri unaweza kukabiri mahitajhi yako zaidi nakufuta umaskini. Utaweza wapeleka watoto wako shule na hata kuduma bora za Afya na kadhalika, Uzalishaji ukipungua huondoa ajira na hivyo shida kuendelea ama kuongezeka.

Sasa huwezi chukua moja ukalijengea hoja ukasahau kiini chake na ndicho tulichokuwa tukikitafuta. na mimi muda wote nimekuwa nikisema kosa ni la Kimfumo sio Zitto wala nani. na ndio mifano uloitumia hapo chini kunyesha jinsi mfumo mbovu unavyoweza athiri maendeleo ya watu. kama vile wazazi wanaopata mshahara mzuri lakini vipaumbele vyao vikawa Hovyo huwezi kuwalalamikia ndugu walowezeshwa ila wazazi.
 


Soma kiduchu ulichoandika wewe na Waberoya...
 
Mada ni ACT kama mpini wa kumaliza upinzani. Naomba nichepuke kidogo kwasababu ubabaishaji wa maneno inaonekana kuwa tatizo la kitaifa.

Swali, Mkandara, mkoa gani umewezeshwa? Umewezeshwaje na kutumia rasilimali zipi?
 
Last edited by a moderator:
Soma kiduchu ulichoandika wewe na Waberoya...
Haswa na hii ndio reality pasipo kuzungumzia WATU. kama hoja yetu ingekuwa tunatazama Zitto au Mbowe wataweza vipi kubadilisha mikataba ambayo Mkapa aliweka hapo ingetupeleka kwingine kabisa maana tungezungumzia zaidi habari za kutaifisha miradi hiyo. Maswala ya kodi nadhani yamekwisha pitishwa mashirika hayo wanalipa sasa hivi kama kweli maana tunaambiwa tu wanalipa. Isipokuwa kodi zao zikusanywe wapi hapo ndio hatuna majibu kwa nini zikusanywe TRA - Dar badala ya mikoani ikiwa kodi zingine zinakusanywa mikoani lakini pia haiwezi kuwasaidia ikiwa wanachokatiwa ni kiasi kile kile inabidi sheria mpya zitungwe. pengine hapa ndipo Zitto na Mbowe wanapalenga zaidi kutoa ahadi zile Shinyanga.

Sasa hii iwe ndio fikra za ACT na Zitto kuhusu Shinyanga katika kufumua mfumo mzima safi maana kuna miradi mingi tu imesainiwa Kifisadi. Na kusema kweli mimi sioni tofauti kubwa baina ya Chadema na ACT katika fikra zao zaidi ya kwamba sasa hivi Zitto kapata jukwaa la kusemea maana alikwisha zidiwa ndani ya Chadema kwa kutoaminiwa. Nakumbuka mara ya mwisho Zitto nimemsikia ni kule Karatu akigombeza watendaji walotaka kumwagusha dr.Slaa kwa sababu hakuwa mbunge wao..
 
Gamba la Nyoka, Mkandara, Ritz, Adharusi, mmeona video clip aliyoweka TUJITEGEMEE? Katika hiyo clip, Zitto anasema kwamba kapu la Taifa ni GDP, na kwamba mchango wa Tabora kwenye kapu la taifa ni tumbaku. Lakini pamoja na hayo, tumbaku wanazochangia wananchi wa Tabora kwenye kapu la taifa, returns Zake (Mgao) sio sawa na mchango huo. Hadi Hapo tupo pamoja? Twendeni hatua kwa hatua.
 
Last edited by a moderator:
Mkandara unatisha...naomba nikukumbushe kidogo kuhusu majadiliano yaliyokuwa yakiendelea Jukwaa la Siasa kwenye mada iliyofananafanana na hii. Mwana JF anayejulikana kwa jina Abunuas, akiunga mkono msimamo na utetezi wako kwa Supreme Leader wa ACT, aliandika hivi, nanukuu;
Mkandara, huyu Abunuas ni mtu mwenye uwezo wa kuchangia humu jamvini, na kama aliweza kuelewa (maybe erroneouly) maneno ya Zitto, hebu fikiria watu wa kijijini Shinyanga waliokuwa wanamsikiliza. Kubali usikubali hii ni mbegu ya hatari kabisa Supreme Leader anataka kuipanda katika jamii na katu hatuwezi kukaa kimya.

Huyo ni mtu hatari wa kukemewa bila kificho na nawashukuru wote ambao bila kumung'unya maneno wamemkanya na kumtaka aache mara moja kupanda mbegu za chuki katika jamii. Kama wewe kwa mapenzi uliyo nayo kwake huoni hili basi na wewe mimi sisiti kukwambia acha mara moja kuunga mkono hizi njama za kupanda chuki katika jamii.
 
Mkuu Mag3 hatari inayosababishwa na kauli za supreme ni kubwa kuliko watu wanavyosoma.
Zifuatazo ni nukuu za mabandiko ya watu wiki mbili kabla ya mjadala kuanza hapa.
Someni kauli hizi Kauli ya Zitto imemfanya huyu ndugu aamini kuwa bajeti ya nchi inakwenda sehemu moja.
Tukumbuke Zitto aliwahi kuwa bungeni na hakuwahi kulalamika au kuonyesha bajeti kwenda sehemu moja
Huyu bwana hasira alizo nazo dhidi ya supreme na ACT , ameshajenga fikra za kuwashambulia waha pindi ‘xenophobia' anayohubiri supreme leader/ACT ikianza. Fikiria tayari ana wazo hilo, Zitto haoni hatari hii
Huyu ndugu ameshaamini maneno ya supreme leader/ACT kuwa mapato ya mkoa wake yanakwenda kwingine. Amechoka kuibiwa na Kilimanjaro/Arusha. Tayari fikra zimeshamjaa, haoni wala hatafuti ukweli .
Kila ukweli ameshausikia kutoka kwa Supreme/ACT
Kwa taarifa yako tu Zitto ana watarget wananchi wa callibre yako,zaid ya kutujengea chuki ya wenyewe kwa wenyewe hakuna la ziada....
Ndugu ameiona chuki na tatizo analojenga supreme/ACT. Katka hali hii kisiasa kuna tatizo kubwa sana kwa supreme na ACT. Heri ya wanao ona tatizo, swali, ni wangapi ukilinganisha na wale wanaomeza hotuba za supreme/ACT bila kufikiri? Mnaona sumu ya Zitto inavyolitafuna taifa? Huyu bwana anaamini ile mikoa aliyosema inaiba ni kweli. Kaamini ipo mikoa isiyochangia lakini inaiba kutoka serikali

 
Ndivyo Tulivyo yaani ukitaka kuwajua wadanganyika zungumzia chake tu utasikia.
Na saa hii habari ya UJAMAA matumbo moto maana wanajua UNYONYAJI utapigwa vita hata iwe mkoa kwa mkoa.
!!!......
Mkuu anaendelea kuaminisha umma anapigania masilahi mapana yataifa kama alivyosema supreme/ACT !!.
Wote wawili wanayo yao ya moyoni


Unafiki kitu kibaya sana, mwenyezi mungu hakawii kumtoa mnafiki kimaso maso

Pili, wanajamvi angalieni video iliyoletwa wakati Zitto anahutubia Tabora.
Video imekatwa wakati anaanza kushambulia Kilimanjaro

Hii ni mara nyingine tena, ukiacha Shinyanga na Mwanza

Historia inaonyesha alianza mashambulizi kwa Kilimanjaro tangu aliposema ‘Msiogope EAC, mbona Kilimanjaro imeendelea kuliko Kigoma'

Kwa mwendo huu bado tunausiwa tukae kimya!

Hapana, tutasema tu, kukaa kimya ni kulikana taifa na
nchi


.
 
Mkuu nadhani hawa watu wapo pande zote..Kwangu miye hyo Abunuas na Nicholas ni wamoja na hatari kama unavyoiona wewe. Tatizo la mijadala humu ni kwamba watu wanaweza kumuona Abunuas mtu hatari sana lakini wakashindwa kumuona Nicholas ila mtetezi wa upande unafanya hatari ile ile. Na wapo walomuona Nicholas hatari wakashindwa kumuona Abunuas kwa sababu wako naye.

Hawa wote mimi husema wenye tatizo ni wao, sio Abunuas wala Nicholas kwa sababu hata wao wanafikiria kama Abunuas au Nicholas wamechagua tu upande kutumia fikra na hisia zao za Ukabila ama Udini kutetea chao, lakini kama watakuwa open minded watazisoma hoja hizo na kugundua kwamba nchi yetu ina tatizo kubwa la Ukabila na Udini. na hii ndio hatari kubwa tulokuwa nayo maana sio kina Abunuas na Nicholas tu wanaoandika bali hata wanaosoma na kuchagua upande kushabikia ni hatari zaidi maana hawa ndio wataoshika mtutu kupigania chao baada ya kurubuniwa.

Na ndivyo ilivyo makazini, Leo ukisema Bima kumejaa Wakerewe utapigwa vita sana kwa sababu umelitaja Kabila japo kweli viongozi wa Bima wanatumia Ukabila katika kutoa ajira katika nafasi nyeti. Je, mwananchi anayetaka kulalamikia swala hilo atumie maneno gani kuyazungumzia? Je, kiongozi wa nchi anapotaka kukemea jambo kama hilo atumie maneno gani ambayo hayataeleweka ni kuwatenga Wakerewe, isieleweke sio kwamba hataki wapate ajira Bima bali wasipendelewe ktk swala la Ajira zinazopatikana hapo Bima. Huu ni mfano tu wa jinsi Ukabila na Udini ulivyokomaa nchini kiasi kwamba unalindwa na watu kuhakikisha hali hiyo inaendelea = UMIMI.
 
Mkuu Mkandara, kama kawaida unakwepa hoja; hoja hapa ni kwamba kama Abunuas, mtu mwenye uwezo wa kuchangia humu jamvini, aliweza kuelewa (maybe erroneouly) maneno ya Zitto, hebu fikiria watu wa kijijini Shinyanga waliokuwa wanamsikiliza Supreme Leader.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hatakujibu hata kwa bahati mbaya, atazunguka zunguka tu
Aliwahi kuulizwa kauli ya Zitto ipo sahihi? Jibu lake, mbona Mbowe kasema wasukuma…

Hapa swali lipo straight, kwamba kauli ya Zitto the supreme,kama Abunuasi ameielewa katika ukakasi huo, vipi mwananchi wa kawaida si atakuwa ameeelewa kama Abunawasi? jibu Mbona Nicholas kasema!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…