Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
RASIMU YA WARIOBA IMEANDIKWA KWA MFUMO WA SERIKALI 3
KUIFUMUA NI KUBADILISHA KILA KITU
MAMLAKA YA KUANDIKA RASIMU MBADALA YAMETOKA WAPI?
Bunge la katiba limeanza kuijadili rasimu kupitia kamati. Kamati hizo zimepewa vifungu viwili, cha kwanza na cha sita vinavyozungumzia muundo wa serikali.
Katika mazingira ya kawaida hiyo ingekuwa kazi ya kujadili na kupiga kura.
Kwa mbinu za Samwel Sitta na CCM, wameamua kuanza na vifungu hivyo ili wafumue rasimu ya tume kwa kupendekeza mfumo wa serikali 2 wanaoutaka.
CCM na Rais Kikwete wamehoji uhalali wa 'sample size' ya tume, wakisema watu 20,000 hawawakilisha maoni ya watu milioni 41. Upotoshaji huu haukuzingatia ukweli, hiyo ilikuwa sample size na kitaalamu inakubalika. Milioni 41 ni pamoja na vichanga na watoto.
Baada ya kuona kitaalamu hilo limeshindikana, CCM wamekuja na mbinu wakiwa wamejipanga ionekane maoni ya tume hayafai.
Kitu wasichoelewa ni kuwa tume ilipewa uhalali wa kisheria na maoni yake yamejengwa kwa msingi huo. Je, watakapobadilisha na kuweka kifungu cha serikali 2, nani amewapa mandate hiyo?
Kitaalamu wanataka kutuambia kuwa sample size ya watu 600 ni kubwa sana kuliko 20,000 na hivyo wana haki ya kuandika rasimu mbadala.
CCM wameshindwa kuelewa kuwa rasimu nzima ipo katika mfumo wa serikali 3, sehemu kubwa ikiwa ni ile ya shirikisho zaidi kuliko washirika wa muungano.
Mambo ya kawaida kama haki za binadamu, ukisoma yapo kulingana na mfumo uliotarajiwa.
Jaribio la kufumua rasimu litazua tatizo la rasimu nyingine ya watu 600 au chini ya hapo.
Mpango wa kuingiza rasimu ya CCM upo mbioni. Lakini je;
1. CCM itaweza kuingiza mfumo wao wa serikali 2 zikiwa na mabunge 3 bila tatizo?
CCM wanasema kutakuwa na bunge la Tanganyika kwa mambo ya Tanganyika.
Swali la kujiuliza hilo bunge la Tanganyika litasimamia serikali ipi?
Litaongozwa na kiongozi gani wa serikali asiye na uhusiano na serikali kuu?
Litahudumiwa na gharama za serikali ipi ikiwa tuna serikali ya JMT na SMZ?
2. Kwa kuangalia mabadiliko ya 10 ya katiba ya znz ya mwaka 2010, mapendekezo ya CCM yatafanyikaje? znz ni nchi, je, CCM itakuwa na uwezo wa kuwalazimisha wznz wakubaliane na kufumua katiba yao ili ikidhi mahitaji ya uwepo wa bunge la Tanganyika.
Je, kisiasa hilo litakubalika znz?
3. Malalamiko ya zanzibar ni hali ya Tanganyika kuvaa koti la Tanzania.
Kwa muundo wa CCM kuna uwezkano gani wa kuondoa hisia hizo iwapo kuna bunge la Tanganyika linalohudumiwa na JMT?
Hoja ya bunge la Tanganyika inajirudia hapa kwa kuangalia malalamiko ya wazanzibar pia
4. Malalamiko ya Tanganyika ni kubeba gharama kubwa za muungano.
Tume ya Warioba imepunguza mambo hayo kutoka 22 hadi mambo 7.
Hilo pia ni dai la znz kuwa mambo yameongezwa kinyemela. Kwa muundo uliokusudiwa na CCM, gharama za serikali ya JMT zitachangiwaje?
Na je mapendekezo ya CCM yatapunguza mambo chini ya yale 7 . Endapo haitawezekana, vipi suala la gharama kwa tume ya Warioba lionekane kubwa kuliko mapendekezo ya CCM
5. Rasimu ya Warioba inasisitiza uwepo wa chombo cha tatu cha sheria.
Endapo CCM watafumua rasimu ya Warioba, chombo hicho cha tatu watakiweka katika sehemu gani ya rasimu yao, na je huo si mwanzo wa kuandika rasimu mpya kabisa nje ya utaratibu?
6. CCM inapendekeza yawepo mambo ya muungano na yasiyo ya muungano.
Katika rasimu ya Warioba mambo hayo yametengwa kwa kuzingatia uwepo wa serikali 3, za washirika na ile ya pamoja.
Je, kwa muundo wa serikali 2 na bunge la Tanganyika, mambo yanayoihusu Tanganyika yatahudumiwa na serikali ipi? Na ni vipi mambo hayo yanaweza kutengwa iwapo hakuna serikali ya kushughulikia.
Hoja ya kuwepo kwa bunge la Tanganyika bila serikali ni uwepo wa mhimili mmoja ukiwa hauna washirika wake ambao ni serikali na mfumo wa sheria.
Vipi mambo yasiyo ya muungano yanaweza kushughulikiwa na bunge la Tanganyika bila uwepo wa serikali ya Tanganyika.
7. Kwa vile bunge la katiba linataka kufumua rasimu ya Warioba, ni vipi mambo yaiyoshindikana miaka 50 yanaweza kupatiwa ufumbuzi na watu 600 kwa siku 60?
8. Suala la mapato na mgawanyo wake litashughulikiwa vipi iwapo kuna Tanzania ambayo znz inadai imo ! Watanganyika watakuwa na amani gani juu ya mchango wa znz katika muungano, ikiwa miaka 20 hawajachangia chochote.
9. Masuala ya ulinzi na usalama ambayo Tanganyika iimeyabeba yatatafutiwa ufumbuzi gani ili Znz nayo ichangie bila kumtupia mzigo huo Mtanganyika?
10. Mfumo wa CCM unaopendekezwa umelenga nini? Kumaliza tatizo la malalamiko ya wazanzibar kwa kuwapa mamlaka zaidi, au kumaliza tatizo la Tanganyika kwa kubeba muungano peke yake au kuridhisha pande zote.
Kwa mfumo wa serikali 2 ni kwa njia gani hilo linawezekana bila upande mmoja kulalamika ima kwa kuonewa au kuumizwa.
11. Kama znz wana fiscal autonomy, mwisho wa autonomy yao ni upi ikiwa katiba yao ni juu ya katiba ya JMT. Na je, znz wapo tayari kurekebisha katiba yao ili kukidhi haja ya mfumo wa CCM. Ni kwanini tudhani znz inapaswa kuwa na fiscal autonomy na wala si Tanganyika.
Je, haki ya Mtanganyika kuwa na fiscal autonomy yao ipo wapi na kwanini Tanganyika isipewa autonomy kama mshirika wa muungano znz alivyopewa.
12 Endapo znz inadai historia na ulinzi wa rasilimali zake, hizi za Tanganyika nani ni custodian wake na kwanini historia na rasilimali za Tanganyika ziwe za Tanzania.
Wanaduru haya ni baadhi ya mambo tunayotakiwa tuyajadili kwa pamoja.
Rasimu ya CCM inayoingizwa kinyemela na Samwel Sitta si tu ni hatari kwa kustakabali wa taifa bali ni catalyst ya vurugu katika miezi michache ijayo.
Tafadhali pitia nyuzi zifuatazo kama sehemu ya mjadala huu.
https://www.jamiiforums.com/great-t...shaji-na-kiwewe-cha-kuzinduka-tanganyika.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...a-katiba-je-katiba-itatokana-na-wananchi.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...-gharama-za-muungano-siri-isiyozungumzwa.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...ba-ya-jk-kuzindua-bunge-maalum-la-katiba.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...asa-vijana-katiba-mpya-na-kiu-ya-uongozi.html
Tusemezane
cc JokaKuu Mwigulu Nchemba John Mnyika Mchambuzi Mzee Mwanakijiji Bongolander Mag3 Ngongo zumbemkuu Mkandara Mtanganyika Nape Nnauye Zakumi Mimi baba HKigwangalla Dr F. Ndugulile Anna Tibaijuka AshaDii Barubaru GHIBUU Pasco Ben Saanane Ritz
KUIFUMUA NI KUBADILISHA KILA KITU
MAMLAKA YA KUANDIKA RASIMU MBADALA YAMETOKA WAPI?
Bunge la katiba limeanza kuijadili rasimu kupitia kamati. Kamati hizo zimepewa vifungu viwili, cha kwanza na cha sita vinavyozungumzia muundo wa serikali.
Katika mazingira ya kawaida hiyo ingekuwa kazi ya kujadili na kupiga kura.
Kwa mbinu za Samwel Sitta na CCM, wameamua kuanza na vifungu hivyo ili wafumue rasimu ya tume kwa kupendekeza mfumo wa serikali 2 wanaoutaka.
CCM na Rais Kikwete wamehoji uhalali wa 'sample size' ya tume, wakisema watu 20,000 hawawakilisha maoni ya watu milioni 41. Upotoshaji huu haukuzingatia ukweli, hiyo ilikuwa sample size na kitaalamu inakubalika. Milioni 41 ni pamoja na vichanga na watoto.
Baada ya kuona kitaalamu hilo limeshindikana, CCM wamekuja na mbinu wakiwa wamejipanga ionekane maoni ya tume hayafai.
Kitu wasichoelewa ni kuwa tume ilipewa uhalali wa kisheria na maoni yake yamejengwa kwa msingi huo. Je, watakapobadilisha na kuweka kifungu cha serikali 2, nani amewapa mandate hiyo?
Kitaalamu wanataka kutuambia kuwa sample size ya watu 600 ni kubwa sana kuliko 20,000 na hivyo wana haki ya kuandika rasimu mbadala.
CCM wameshindwa kuelewa kuwa rasimu nzima ipo katika mfumo wa serikali 3, sehemu kubwa ikiwa ni ile ya shirikisho zaidi kuliko washirika wa muungano.
Mambo ya kawaida kama haki za binadamu, ukisoma yapo kulingana na mfumo uliotarajiwa.
Jaribio la kufumua rasimu litazua tatizo la rasimu nyingine ya watu 600 au chini ya hapo.
Mpango wa kuingiza rasimu ya CCM upo mbioni. Lakini je;
1. CCM itaweza kuingiza mfumo wao wa serikali 2 zikiwa na mabunge 3 bila tatizo?
CCM wanasema kutakuwa na bunge la Tanganyika kwa mambo ya Tanganyika.
Swali la kujiuliza hilo bunge la Tanganyika litasimamia serikali ipi?
Litaongozwa na kiongozi gani wa serikali asiye na uhusiano na serikali kuu?
Litahudumiwa na gharama za serikali ipi ikiwa tuna serikali ya JMT na SMZ?
2. Kwa kuangalia mabadiliko ya 10 ya katiba ya znz ya mwaka 2010, mapendekezo ya CCM yatafanyikaje? znz ni nchi, je, CCM itakuwa na uwezo wa kuwalazimisha wznz wakubaliane na kufumua katiba yao ili ikidhi mahitaji ya uwepo wa bunge la Tanganyika.
Je, kisiasa hilo litakubalika znz?
3. Malalamiko ya zanzibar ni hali ya Tanganyika kuvaa koti la Tanzania.
Kwa muundo wa CCM kuna uwezkano gani wa kuondoa hisia hizo iwapo kuna bunge la Tanganyika linalohudumiwa na JMT?
Hoja ya bunge la Tanganyika inajirudia hapa kwa kuangalia malalamiko ya wazanzibar pia
4. Malalamiko ya Tanganyika ni kubeba gharama kubwa za muungano.
Tume ya Warioba imepunguza mambo hayo kutoka 22 hadi mambo 7.
Hilo pia ni dai la znz kuwa mambo yameongezwa kinyemela. Kwa muundo uliokusudiwa na CCM, gharama za serikali ya JMT zitachangiwaje?
Na je mapendekezo ya CCM yatapunguza mambo chini ya yale 7 . Endapo haitawezekana, vipi suala la gharama kwa tume ya Warioba lionekane kubwa kuliko mapendekezo ya CCM
5. Rasimu ya Warioba inasisitiza uwepo wa chombo cha tatu cha sheria.
Endapo CCM watafumua rasimu ya Warioba, chombo hicho cha tatu watakiweka katika sehemu gani ya rasimu yao, na je huo si mwanzo wa kuandika rasimu mpya kabisa nje ya utaratibu?
6. CCM inapendekeza yawepo mambo ya muungano na yasiyo ya muungano.
Katika rasimu ya Warioba mambo hayo yametengwa kwa kuzingatia uwepo wa serikali 3, za washirika na ile ya pamoja.
Je, kwa muundo wa serikali 2 na bunge la Tanganyika, mambo yanayoihusu Tanganyika yatahudumiwa na serikali ipi? Na ni vipi mambo hayo yanaweza kutengwa iwapo hakuna serikali ya kushughulikia.
Hoja ya kuwepo kwa bunge la Tanganyika bila serikali ni uwepo wa mhimili mmoja ukiwa hauna washirika wake ambao ni serikali na mfumo wa sheria.
Vipi mambo yasiyo ya muungano yanaweza kushughulikiwa na bunge la Tanganyika bila uwepo wa serikali ya Tanganyika.
7. Kwa vile bunge la katiba linataka kufumua rasimu ya Warioba, ni vipi mambo yaiyoshindikana miaka 50 yanaweza kupatiwa ufumbuzi na watu 600 kwa siku 60?
8. Suala la mapato na mgawanyo wake litashughulikiwa vipi iwapo kuna Tanzania ambayo znz inadai imo ! Watanganyika watakuwa na amani gani juu ya mchango wa znz katika muungano, ikiwa miaka 20 hawajachangia chochote.
9. Masuala ya ulinzi na usalama ambayo Tanganyika iimeyabeba yatatafutiwa ufumbuzi gani ili Znz nayo ichangie bila kumtupia mzigo huo Mtanganyika?
10. Mfumo wa CCM unaopendekezwa umelenga nini? Kumaliza tatizo la malalamiko ya wazanzibar kwa kuwapa mamlaka zaidi, au kumaliza tatizo la Tanganyika kwa kubeba muungano peke yake au kuridhisha pande zote.
Kwa mfumo wa serikali 2 ni kwa njia gani hilo linawezekana bila upande mmoja kulalamika ima kwa kuonewa au kuumizwa.
11. Kama znz wana fiscal autonomy, mwisho wa autonomy yao ni upi ikiwa katiba yao ni juu ya katiba ya JMT. Na je, znz wapo tayari kurekebisha katiba yao ili kukidhi haja ya mfumo wa CCM. Ni kwanini tudhani znz inapaswa kuwa na fiscal autonomy na wala si Tanganyika.
Je, haki ya Mtanganyika kuwa na fiscal autonomy yao ipo wapi na kwanini Tanganyika isipewa autonomy kama mshirika wa muungano znz alivyopewa.
12 Endapo znz inadai historia na ulinzi wa rasilimali zake, hizi za Tanganyika nani ni custodian wake na kwanini historia na rasilimali za Tanganyika ziwe za Tanzania.
Wanaduru haya ni baadhi ya mambo tunayotakiwa tuyajadili kwa pamoja.
Rasimu ya CCM inayoingizwa kinyemela na Samwel Sitta si tu ni hatari kwa kustakabali wa taifa bali ni catalyst ya vurugu katika miezi michache ijayo.
Tafadhali pitia nyuzi zifuatazo kama sehemu ya mjadala huu.
https://www.jamiiforums.com/great-t...shaji-na-kiwewe-cha-kuzinduka-tanganyika.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...a-katiba-je-katiba-itatokana-na-wananchi.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...-gharama-za-muungano-siri-isiyozungumzwa.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...ba-ya-jk-kuzindua-bunge-maalum-la-katiba.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...asa-vijana-katiba-mpya-na-kiu-ya-uongozi.html
Tusemezane
cc JokaKuu Mwigulu Nchemba John Mnyika Mchambuzi Mzee Mwanakijiji Bongolander Mag3 Ngongo zumbemkuu Mkandara Mtanganyika Nape Nnauye Zakumi Mimi baba HKigwangalla Dr F. Ndugulile Anna Tibaijuka AshaDii Barubaru GHIBUU Pasco Ben Saanane Ritz
Last edited by a moderator: