Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
DURU: TATHMINI YA CHAGUZI ZA SERIKALI ZA MITAA
Uchaguzi wa serikali za mitaa unaendelea kukiwa na marudio, mikanganyiko na kila aina ya vurugu.
Kuna dalili maandalizi hayakuwa mazuri kwa kiwango chochote kinachofikirika
Matokeo hayawezi kutoa kipimo halisi cha hali ya kisiasa kwa uhalisia wake. Hata hivyo, yanaweza kutoa picha isiyo na rangi kamili ya hali halisi katika muda tulio nao
Matokeo yanaweza kutafsiriwa kwa namna nyingi.
Hivi karibuni kulikuwa na utafiti uliotoa matokeo kuhusu vyama vya kisiasa na wagombe wa Urais kwa mwaka 2015
Lakini pia,kumekuwepo na mambo yaliyoligusa taifa.
Suala la katiba, kashfa za Escrow na uendeshwaji wa bunge na serikali kwa ujumla.
Ni wakati ambapo vyama vya upinzani vimejaribu kuwa karibu kuliko wakati mwingine.
Na ni wakati tunaelekea katika uchaguzi wa mwaka 2015
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, chaguzi za serikali za mitaa zimekuwa na mvuto tofauti na siku za nyuma.
Pengine linachagizwa na ukweli kuwa mitaani/vijijini wapo wapiga kura tofauti na dhana ya wapiga kura wa mjini.
Serikali za mitaa imekuwa ni ngome kubwa kwa CCM kwa kutambua kuwa idadi ya watu wasiokitakia chama hicho mema wengi wapo mijini,idadi isiyoweza kuathiri chaguzi kama za wabunge na Marais kwa upande wao
Baada ya kujikita katika udiwani, vyama vya upinzani vimeanza kuweka mizizi huko vijijini na mitaani.
Swali, je kuna matokeo yanayoweza kuakisi jitihada zao wakiwa wameungana?
Uchaguzi wa serikali za mitaa kwa Tanzania bara, hauwezi kutathiminiwa bila kufikiria Zanzibar.
Ukweli ni kuwa chaguzi za mitaa ni hatua ya mwanzo inayosimika mizizi kuelekea chaguzi za taifa.
Matokeo ya chaguzi za mitaa yana athari kwa chaguzi za bunge na Rais, hivyo, kuzitathmini kwa kuangalia upande mmoja kunaweza kutoa picha isiyo sahihi.
Ni kwa mtazamo huo, kumekuwepo na shamra shamra na majonzi kwa kila upande.
Ni mapema mno kutoa tahmini ya jumla kwa kuzingatia mazingira ya chaguzi, utata na wingi au ubora wa ushindi
Duru tutajaribu kuangalia kwa namna tofauti na kutafsiri matokeo kwa kiwango kitakachopatatikana au kuelezwa.
Tutakuwa na mabandiko mfululizo yakiangalia na kutahmini mambo yafuatayo kabla ya kutoa hitimisho linaloweza kueleza maana ya chaguzi hizi.
Tutafanya hivyo kwa kuangalia mambo kadha wa kadha;
1.Hali na mazingira ya chauguzi (Free and fair election)
2.Wingi au upungufu wa viti(Quantity)
3.Ubora au udhaifu wa ushindi (Quality)
4.Mgawanyo wa wapiga kura (demographic)
5.Nguvu na udhaifu wa vyama (Weakness and strength)
6.Sababu zilizochangia matokeo (contributing factors)
7.Mwenendo mzima wa hali ya kisiasa(political landscape)
8.Nini kinaweza kutokea katika siku, mwezi au mwaka ujao(future)
Yupo mwanasisasa wa Uingereza aliyewahi kusema,siku moja ni muda mrefu sana katika siasa.
Lolote linaweza kutokea na kubadilisha hali ya kisiasa
Wapo wanajamvi wenzetu waliowahi kutoa kauli zinazojadilika kwa hali ya sasa
Pasco aliwahi kusema CCM imechokwa CDM hawajajipanga Mchambuzi akasema, even magician runs out of trick hata wanamazingaombwe huishiwa na mbinu
MwanDiwani kasema upinzani ni vyama vya msimu
Hebu tuangalie kwa upana nini kinapatikana kutokana na chaguzi hizi
Itaendelea sehemu ya I
Uchaguzi wa serikali za mitaa unaendelea kukiwa na marudio, mikanganyiko na kila aina ya vurugu.
Kuna dalili maandalizi hayakuwa mazuri kwa kiwango chochote kinachofikirika
Matokeo hayawezi kutoa kipimo halisi cha hali ya kisiasa kwa uhalisia wake. Hata hivyo, yanaweza kutoa picha isiyo na rangi kamili ya hali halisi katika muda tulio nao
Matokeo yanaweza kutafsiriwa kwa namna nyingi.
Hivi karibuni kulikuwa na utafiti uliotoa matokeo kuhusu vyama vya kisiasa na wagombe wa Urais kwa mwaka 2015
Lakini pia,kumekuwepo na mambo yaliyoligusa taifa.
Suala la katiba, kashfa za Escrow na uendeshwaji wa bunge na serikali kwa ujumla.
Ni wakati ambapo vyama vya upinzani vimejaribu kuwa karibu kuliko wakati mwingine.
Na ni wakati tunaelekea katika uchaguzi wa mwaka 2015
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, chaguzi za serikali za mitaa zimekuwa na mvuto tofauti na siku za nyuma.
Pengine linachagizwa na ukweli kuwa mitaani/vijijini wapo wapiga kura tofauti na dhana ya wapiga kura wa mjini.
Serikali za mitaa imekuwa ni ngome kubwa kwa CCM kwa kutambua kuwa idadi ya watu wasiokitakia chama hicho mema wengi wapo mijini,idadi isiyoweza kuathiri chaguzi kama za wabunge na Marais kwa upande wao
Baada ya kujikita katika udiwani, vyama vya upinzani vimeanza kuweka mizizi huko vijijini na mitaani.
Swali, je kuna matokeo yanayoweza kuakisi jitihada zao wakiwa wameungana?
Uchaguzi wa serikali za mitaa kwa Tanzania bara, hauwezi kutathiminiwa bila kufikiria Zanzibar.
Ukweli ni kuwa chaguzi za mitaa ni hatua ya mwanzo inayosimika mizizi kuelekea chaguzi za taifa.
Matokeo ya chaguzi za mitaa yana athari kwa chaguzi za bunge na Rais, hivyo, kuzitathmini kwa kuangalia upande mmoja kunaweza kutoa picha isiyo sahihi.
Ni kwa mtazamo huo, kumekuwepo na shamra shamra na majonzi kwa kila upande.
Ni mapema mno kutoa tahmini ya jumla kwa kuzingatia mazingira ya chaguzi, utata na wingi au ubora wa ushindi
Duru tutajaribu kuangalia kwa namna tofauti na kutafsiri matokeo kwa kiwango kitakachopatatikana au kuelezwa.
Tutakuwa na mabandiko mfululizo yakiangalia na kutahmini mambo yafuatayo kabla ya kutoa hitimisho linaloweza kueleza maana ya chaguzi hizi.
Tutafanya hivyo kwa kuangalia mambo kadha wa kadha;
1.Hali na mazingira ya chauguzi (Free and fair election)
2.Wingi au upungufu wa viti(Quantity)
3.Ubora au udhaifu wa ushindi (Quality)
4.Mgawanyo wa wapiga kura (demographic)
5.Nguvu na udhaifu wa vyama (Weakness and strength)
6.Sababu zilizochangia matokeo (contributing factors)
7.Mwenendo mzima wa hali ya kisiasa(political landscape)
8.Nini kinaweza kutokea katika siku, mwezi au mwaka ujao(future)
Yupo mwanasisasa wa Uingereza aliyewahi kusema,siku moja ni muda mrefu sana katika siasa.
Lolote linaweza kutokea na kubadilisha hali ya kisiasa
Wapo wanajamvi wenzetu waliowahi kutoa kauli zinazojadilika kwa hali ya sasa
Pasco aliwahi kusema CCM imechokwa CDM hawajajipanga Mchambuzi akasema, even magician runs out of trick hata wanamazingaombwe huishiwa na mbinu
MwanDiwani kasema upinzani ni vyama vya msimu
Hebu tuangalie kwa upana nini kinapatikana kutokana na chaguzi hizi
Itaendelea sehemu ya I
Last edited by a moderator: