Duru za Siasa Special: Mgogoro kambi ya Upinzani (CHADEMA)

Nguruvi3

Platinum Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
15,773
Reaction score
32,431
Ndugu wana jamvi na duru za siasa.
Kwanza taarifa hii haijakanushwa na uongozi wa CDM au idara yoyotE na inabaki
ilivyosambazwa katika .
Pili, Chadema wamesema wazi wahusika wamekiri kuhusika na habari hii
Tatu, tunafahamu kuwa watuhumiwa watakuwa na kikao kujibu yaliyoelekezwa kwao na wanahaki ya kusikilizwa ili kupata ‘habari iliyo na uwiano'

Itakapodhihirika kuwa taarifa hii haina ukweli, wahusika kuikana ,uongozi wa CDM utapaswa kujiuzulu kwa sababu ni kosa la kukosa imani, kuvunja uaminifu, kudanganya, kuhadaa na kupaka watu matope.

Kwa wakati huu tutaijadili habari hii kama ilivyoletwa.

Tunafahamu baadhi ya maoni yataweza kutumika katika kujenga au kujibu hoja kwa mikutano kati ya watuhumiwa na wana habari, hilo halitaondoa ukweli kuhusu tunachokiona hakikufanyika, kimefanyika, kina ukweli, kina udanganyifu au upotoshaji.

Tusimame katika ukweli tukiongozwa na fikra wala si hisia, chuki kwakuelewa kuwa upinzani ni sehemu muhimu`ya ustawi wa demokrasia na maendeleo ya nchi yetu.

Post inayofuata tutaanza kuchambua hoja moja baada ya nyingine bila upendeleo au uonevu lakini pia bila huruma au ushawishi wa namna yoyote.

Wana duru lets get strated

Other links
https://www.jamiiforums.com/great-t...ba-ya-jk-kuzindua-bunge-maalum-la-katiba.html

https://www.jamiiforums.com/great-t...shaji-na-kiwewe-cha-kuzinduka-tanganyika.html
 
Nguruvi3, mimi kwa upande wangu nitavuta subira hadi pale wanaodaiwa kuhusika na taarifa hii ama watakiri uhusika wao au wataikataa.
 
Last edited by a moderator:
Marejeo: Kwa muda mrefu tumetahadhirisha sana kuhusu mgogoro ndani ya CDM. Mwezi wa 6 mwaka jana'sakata la Juliana Shonzo' tuliandika kwa undani kuwa nguvu yake ilikuwa na msukumo mkubwa ndani ya chama.

Tulionya mgogoro wa Kafulila kuwa kuna nguvu zaidi isiyoonekana na hivyo kuna tatizo
Mgogoro wa Masalia, tulionyesha ufa mkubwa zaidi uliopo unaohitaji ufumbuzi wa haraka.

Wiki moja iliyopita tuliandika kule duru za siasa kuhusu chanzo cha mgogoro, wahusika kwa kuwataja, na nini CDM wafanyae.
Tulionya kuwa mgogoro huo ni mkubwa unaoweza kukivuruga chama kama ilivyokuwa kwa NCCR na CUF.
Yote yaliyowahi kujadiliwa leo ni marudio tu, kinachotokea sasa ni 'movie' tuliyoiona wakati inaandaliwa tukiwa watazamaji.

Wiki iliyopita tulisema haya
1. Mgogoro unahitaji suluhu ya haraka. Mpambano wa Lema, Zitto, Mwigamba ni dalili, tatizo lilikuwa kubwa.
2. Tulionya kuwa mgogoro huu unachochowe kutoka nje wahusika wakubwa wakiwa ndani ya CDM
3. Tukashauri kikao cha haraka ili kushughulikia tatizo kwasababu litakapofumuka lenyewe itakuwa ni balaa wala si tatizo
4. Tukasema ili kuleta uwiano mzuri na utengamano lazima awepo msuluhishi nje ya uongozi na kundi la watuhumiwa

5. Tukashauri baraza la wadhamini wa CDM waliangalie tatizo na kulichukua mikononi mwao
Sababu zilikuwa kama ifuatavyo
a) Kuepuka maamuzi ya jazba au yenye namna isiyotenda haki kwasababu tayari kuna pande mbili na moja haiwezi kuwa inatuhumu, ikasima upande mwingine na kuendesha mashataka, ikageuga na kutoa hukumu
b)Maamuzi nje ya uongozi uliopo yataleta muafaka miongoni mwa wanachama waliogawanyika katika makundi kwa itikadi na mapenzi tu ya viongozi

6. Tukashauri kuwa ni muhimu ukwepo uchaguzi kabla muda tete haujawadia ili kuleta utengamano kabla ya mwaka 2015

7. CDM izingatie masuala ya kijamii katika kulishugulikia tatizo kwasababu ni kubwa na lina mizizi na washiriki wengi.

Kikao cha kamati kuu kimetoa maamuzi ya kuwavua uanachama na kutaka wajielezekatika siku 14 kwanini wasifukuzwe

Hatua hizo zinaweza kuwa za kidemokrasia, zilizofuata taratibu, sheria nakanuni.
Lakini je, zilizingatia factors nyingine zinazoweza kujitokeza ambazosi lazima ziwe za kanuni , sheria au maadili?
Je, hatua zilifuata kwa kuangalia nyakati, jamii au mazingira ya suala lenyewe?

Uwepo wa makundi ya ushindani ndani ya chama cha siasa ni jambo zuri sana.
Makundi hutoa viongozi bora kama chekecheo na ndivyo ilivyo duniani kote.
Kinachotakiwa ni kushindanisha sera, maono na mipango.
Tenamakundi hayo ni ya ushindani na wala si upinzani

CCM ilikuwa na ushindani wa ndani uliojenga chama, baada ya kuuachakilichofuata ni makundi na maana nzima ya chama tawala imepotea. Kilichobaki nikuviziana katika 'glasi za maji ya kunywa'

Mag3 hoja yako ina msingi na mantiki. Hebu tuvute subira kidogo ili tupate kuona silingi pande zote

Tutaendelea baada ya mkutano tarajiwa kesho
 
Mkuu nadhani tunatakiwa kujua kuwa migongano ndani ya chama ni jambo la kawaida, na kimisngi kama ikiwa hadled vizuri basi inaweza kujenga chama na sio kukibomoa. Nadhani tunaweza kujifunza kutokana na experience ya NCCR.

KUna watu walijazwa NCCR na kufanya kila hila kuijuhumu hadi ilipokuifa, na wale waliojazwa wakaneda TLP na Mremba na kummaliza huko huko TLP.

Kueleka 2013 ni wazi kabisa kuwa sasa hivi CDMinawekwa kwenye defence mode ili isihindwe kuishambulia CCM, na kinachotokea ndani ya chama, kama kweli ni genuine mgogoro naona ni jambo zuri, as longo as linalenga kuifanya CDM iwe na posture ya offense.

Tunatakiwa kuiangalia CDM as a an institution and its ability to deal with internal troubles, i do not think it is of any good start looking into individuals.
 
Well said Bongolander
Katika bandiko 3 nimezungumzia hili la ushindani nikasema ni jambo zuri sana katika kuimarisha demokrasia.
Ninachokiona ndani ya cdm ni upinzani na wala si ushindani. Upinzani hauwezi kutokea ndani ya chama kimoja lakini upinzani unatokea miongoni mwa vyama.

Chadema kama insitution ambayo imebeba matarajio ya sehemu ya jamii inapaswa kuoneysha utayari wa kushughulikia migogoro ndani ya chama kwanza ili kuonyesha utayari wa kushughulikia migogoro katika dola.

Kwa viashirio, maoni, maonyo n.k. haikuonekana kama insitution inayoweza kufanyia kazi habari. Ndio maana nilieleza kuwa tatizo halikuanza juzi Arusha, lilianza kuanzia wakati wa Kafulila, Juliana na Masalia kwa ujumla.
Kwanini tatizo lenye miaka zaidi ya 5 liendelee kuitafuna institution kubwa kama hiyo? Kuna utayari kwa hilo.

Ni kweli lazima tuiangalie kama institution lakini pia ikumbukwe kuwa institution inatangenezwa na watu na hakuna institution inayoishi bila watu. Ni watu wanaojenga au kubomoa na hao ndio wanaangaliwa.
CDM kama chama sioni kama kuna tatizo, lakini CDM kama uongozi naona lipo tatizo.
Je, hilo lifumbiwe macho tukitumaini kuwa institution itajirekebisha yenyewe?

Ni kweli kuwa kuna mbinu za kuihujumu kutoka kwa CCM. Hii ni baada ya CCM kukosa nguvu za hoja kama insstitution iliyotokana na watu kuacha misingi yake ya awali, kuruhusu watu kuingilia institution n.k.
Lakini pia majaribio kama ya kuwagawa watu kwa kutumia ukabila na udini yalionekana kugonga mwamba na pengine kuirudi CCM kwa namna moja au nyingine.

Kinachoonekana sasa hivi ndani ya cdm ni kuruhusu au kutoa udhaifu ambao CCM wanautumia kuimaliza.
CCM sidhani kama ina makosa kwasababu ndicho inachotaka, makosa yapo CDM kwa kuruhusu udhaifu unaowezesha CCM kutimiza matakwa yake.
 
wakuu matamko yameshatolewa, sijui mnasemaje? binafsi ntashangaa kama hawa watu hawatofukuzwa uanachama, ntarudi badae kutoa maoni yangu.
 
wakuu matamko yameshatolewa, sijui mnasemaje? binafsi ntashangaa kama hawa watu hawatofukuzwa uanachama, ntarudi badae kutoa maoni yangu.
Ahsante sana zumbemkuu kuhamisha uzi wa taarifa na kuuleta hapa.

Tumesoma taarifa hizo kwa kina. Kilichoonekana ni siasa na wala si majibu kuhusu tuhuma za usalaiti zinazowakabili.
Nadhani wamekubali kuwa wanahusika na waraka na sasa ni wakati tuuchambue kwa kina.
Mkuu Mag3 kitendawili kimeshateguliwa na sasa tunaweza kuongelea kwa ukubwa na upana wake.
 
Last edited by a moderator:
Ningependa kutoa baadhi ya vifupisho vilivyotumika katika waraka huo ili kuuelewa kwa undani.

Mtendaji mkuu- Dr Slaa
Kiongozi aliyepo, mpinzani wetu- Mh Mbowe
Mtendaji msaidizi- Zitto Kabwe
mida eight (mida= saa, eight nane) saa nane
kichaa wa 'ars'-Lema
MM= Zitto
MI= Kitila mkumbo
M3 =Mwigamba

Marejeo: Kwa muda mrefu tumetahadhirisha kuhusu mgogoro ndani ya CDM.
Mwezi wa 6 2012 'sakata la Juliana Shonzo' tuliandika kwa undani kuhusu nguvu aliyokuwa nayo na mshukumo mkubwa ndani ya chama.

Tulionya mgogoro wa Kafulila kuwa kuna nguvu zaidi isiyoonekana na hivyo kuna tatizo
Mgogoro wa Masalia, tulionyesha ufa mkubwa unaohitaji ufumbuzi wa haraka.

Wiki iliyopita tuliandika duru za siasa kuhusu chanzo cha mgogoro, wahusika kwa kuwataja, na nini CDM wafanye.Tulisema mgogoro ni mkubwa unaoweza kukivuruga chama kama ilivyokuwa NCCR na CUF.
Yote yaliyodiliwa leo ni marudio tu, kinachotokea ni 'movie' tuliyoiona wakati inaandaliwa tukiwa watazamaji.

Wiki iliyopita tulisema haya
1. Mgogoro unahitaji suluhu ya haraka. Mpambano wa Lema, Zitto, Mwigamba ni dalili za tatizo kubwa.
2. Mgogoro huu unachochewa kutoka nje lakini wahusika wakubwa wamo ndani ya CDM
3. kikao cha haraka ili kushughulikia tatizo kwasababu litakapofumuka lenyewe itakuwa ni balaa wala si tatizo
4. Tukasema ili kuleta uwiano mzuri na utengamano lazima awepo msuluhishi nje ya uongozi na kundi la watuhumiwa

5.Tukashauri baraza la wadhamini wa CDM waliangalie tatizo na kulichukua mikononi mwao

Sababu zilikuwa kama ifuatavyo
a) Kuepuka maamuzi ya jazba au yenye namna isiyotenda haki kwasababu tayari kuna pande mbili
b)Maamuzi nje ya uongozi uliopo yataleta muafaka miongoni mwa wanachama waliogawanyika
6.Tukashauri ni muhimu ukwepo uchaguzi kabla muda tete(2015) haujawadia ili kuleta utengamano

7. CDM izingatie masuala ya kijamii katika kulishugulikia tatizo,ni kubwa na lina mizizi na washiriki wengi na wakubwa.

Kikao cha kamati kuu kimetoa maamuzi ya kuwavua uongozi na kutaka wajieleze katika siku 14 kwanini wasitimuliwe

Hatua hizo zinaweza kuwa za kidemokrasia, zilizofuata taratibu, sheria na kanuni.
Lakini je, zilizingatia factors nyingine zinazoweza kujitokeza ambazo si lazima ziwe za kanuni , sheria au maadili.
Je, hatua zilifuata na kuangalia nyakati, jamii au mazingira ya suala lenyewe?

Uwepo wa makundi ya ushindani ndani ya chama cha siasa ni jambo zuri.
Makundi hutoa viongozi bora kama chekecheo na ndivyo ilivyo duniani kote.
Kinachotakiwa ni kushindanisha sera, maono na mipango. Tena makundi hayo ni ya USHINDANI na wala si UPINZANI.

CCM ilikuwa na ushindani wa ndani uliojenga chama, baada ya kuuacha kilichofuata ni makundi na maana nzima ya chama tawala imepotea. Kilichobaki ni kuviziana katika 'glasi za maji ya kunywa'

Kuna swali linajitokeza endapo waraka huo una tatizo lolote.
Jibu la haraka ni ndiyo. Lipo tatizo kubwa sana katika waraka huo.

Laiti matatizo tutakayoyaonyesha yasingekuwepo waraka usingekuwa na tatizo.
Tungebaki kuuita waraka wa mipango ya ushindani ambayo tumekubali ni njia halali ya kuimarisha chama.

Kwanini waraka huo una matatizo.
1. Umeandikwa ukihusisha viongozi wa chama. Zitto ni naibu katibu mkuu, mtendaji wa pili wa chama ngazi ya kitaifa.
Kitila ni mjumbe wa kamati kuu na mshauri wa chama aliyeaminiwa hata kuja na formula ya kupta wabunge wa kuteuliwa. Kitila amehusishwa sana katika shughuli za chama kwa wadhifa huo.

Mwigamba ambaye ametajwa pia katika waraka ni mwenyekiti wa mkoa wa CDM.
Mtu muhimu sana katika shughuli za chama kimkoa na kitaifa.

Hawa walikuwa na nafasi ya kuleta mabadiliko waliyokusudia bila kupandikiza mbegu za chuki, udini na uhasama.
Bila kuwagawa wanachama kwa njia za chuki badala ya sera.

Kwa kuweka tuhuma dhidi ya uongozi hadharani bila kujificha au kujiuzulu nafasi zao kama kitendo cha kutoridhika. Kuendelea na nafasi zao wakitengeneza kundi ni usaliti katika maamuzi yale yale wanayoyafanya wakiwa viongozi ndio usaliti na wala si lazima uwe wa kutumiwa na CCM.

2,. Waraka umepotosha umma au kupaka matope viongozi waanzilishi na wa sasa.
Soma hapa ''.....wakuu wetu wawili wa kwanza ambao kimsingi waliweka msingi mzuri sana wa kutong'ang'ania madaraka na badala yake kuachia mapema na kumwachia mwingine kidemokrasia bila vurugu. Hawakuwa madikteta na tunawapongeza sana''

Mbowe alichaguliwa kidemkorasia na hivyo kumsema ni dikteta ni upotoshaji.
Pili, utaratibu wa kuachiana madaraka ni vipindi viwili,kama watangulizi waifanya kwa kipindi kimoja ni matakwa yao na si kanuni au sheria za chama. Kudai Mbowe ang'ang'ania madaraka ni upotoshaji.

3. Waraka umetumia maneno makali kuonyesha vita kati ya wanachama na wala si washindani.
Mfano '' mtu mwenye uwezo kubwa kuliko tunayetaka kumtoa, Mkuu aliyepo kung'ang'ania kuendelea ni kikwazo, Kukubali kuongozwa na mtu mwenye akili ndogo, Mpinzani wetu anaporushiwa kombora,mpinzani wetu hana uwezo ABC, ...akili yake ni ya magumashi darasini na hana vipaji,... kushinda vita iliyopo mbele yetu n.k.''
Kauli hizi hazionyeshi watu waliokuwa wanajenga ushindani bali waliotaka kuleta mapinduzi nje ya demokrasia.

4. Waraka ulikusudia kuvunja misingi ya demokrasia ya chama kinachojinasibu kuwa cha kidemokrasia.
Viongozi wanachuguliwa na watu na si kundi la watu wachache tena wasiofika 10.

Hiyo hufanyika katika Vanguard party kama Politubuoro ya Urusi au communist part ya China.
soma walichokusudia ''Sisi wenyewe tunaoandaa mkakati huu hatuna hakika kama tunayemtaka yu tayari, ...nayo ni fursa muhimu kwa tunayemtaka, ...aliyepo ni lazima ang'olewe,....tukileta mtu asiyefahamika n.k.'

Lengo lilikuwa kung'oa uongozi uliopo kidemkrasia na kuweka watu wanaowataka wao na wala siyo waliowanadi wakatakiwa na wanachama. Huku ni kubinya demokrasia na lengo la waraka si zuri

5. Waraka umepingana na maneno ya chama, umethibitisha tatizo la chama na umepingana na maneno ya viongozi.
CDM siku zote imetuhumiwa kwa udini na wapinzani wao.

Hata kama si kweli leo tunaona mkakati wa kuweka viongozi kwa kutumia vigezo vya dini.
Maneno yao '' ......ni mwislam..'

Hili halionyeshi nia njema ya walioandaa waraka kwa mustakabali wa chama au taifa kwa ujumla.
Waraka umekusidia kuchoche hisia zilizokuwepo na pengine kuaminisha watu kuhusu hisia zao.Ni usaliti na hujumu

6. Waraka ulikusudia hujuma katika CDM, soma ''mkakati huu hautakiwa kujulikana...,tunahitaji watu watatu waaminifu katika ngazi ya taifa ambao tayari tuna, lazima ang'olewe'

Haya yalifanywa na watu waliokuwa wanaingia katika maamuzi makubwa ya chama kitu ambacho ni kama ushushu wa kukihujumu chama kwani kila walilofanya lililenga tofauti na kule walikofikiria

Kwa kuangalia hayo ni ngumu kuamini waraka huu ulilenga ushindani wa kisiasa. Ni wazi kabisa kulikuwa na hujuma.

Lakini, je kila kilichoelezwa kilikuwa uzushi?
Je kuna ukweli au upotoshaji?

Tunaendelea na sehemu ya tatu.......
 
Huyu M2 anastahili kuwa wa kwanza kufukuzwa, kwanza ni mwajiriwa wa chama huyu! utetezi wa Dr. Mkumbo unaeleweka ila chaguo lao yaani MM wamebugi kabisa.
 
Inaendelea

UPOTOSHAJI KUTOKA KATIKA WARAKA

1.
Waraka unasema haya ''Tunapopongeza juhudi zao hizi tunahitaji pia kuwapongeza wakuu wetu wawili wa kwanza ambao kimsingi waliweka msingi mzuri sana wa kutong'ang'ania madaraka na badala yake kuachia mapema na kumwachia mwingine kidemokrasia bila vurugu''

Kusema Mbowe kang'angania madaraka si sahihi.Katiba inasema vipindi viwili. Si lazima viwe viwili kama alivyofanya Mtei na Mkani. Hilo haifanyi ung'ang'anizi kwa yule atakateimiza vipindi viwili.
Endapo muda umepita ni suala la kufuata taratibu kwa kuzungumza ndani ya chama na si vikundi tena vikitoa kashfa na kejeli wakati watu hao wakiwa wajumbe vikao muhimu vya chama.

2.
''Mwaka 1995 chini ya mkuu wa kwanza(Mtei) tulipata wawakilishi watatu kwenye chombo chetu kikuu cha uwakilishi.
Mwaka 2000 chini ya mkuu wa pili(Makani) tukapata wawakilishi wanne pamoja na wa nyongeza mmoja na kuwa watano.
Mwaka 2005 chini ya mkuu wa tatu(Mbowe), tulipata wawakilishi watano na wa nyongeza sita jumla wakawa 11.
2010 (Mbowe) wawakilishi wakaongezeka kuwa 23 na wa nyongeza 25idadi kuwa 48 na mwingine mwaka jana wawe 49''

Waraka umewapongeza viongozi wawili wa mwanzo na kuacha ukweli kuwa idadi imezidi kuongezeka hata alipokuja mkuu wa tatu. N kweli kuwa matokeo ya serikali za mitaa hayakuwa mazuri, lakini waraka hauonyeshi ikilinganishwa na nini.
Matarajio kutokana na hamasa yanaeleza kwanini matokeo si mazuri. Kwa kutumia takwimu idadi ya viti katika serikali za mitaa imeongezeka kutoka 0 had 6%, 0 hadi 24%. Kutosema ukweli kwa kuficha takwimu ni upotoshaji.

3.''Makubaliano ya kifisadi na mtu binafsi anayeuza vifaa vya kueneza taasisi.
Hakuna kikao chochote cha juu kilichojadili ama kilichowahi hata kupewa taarifa tu kwamba sasa kuna mtu binafsi kapewa tenda ya kuuza vifaa vya taasisi na taasisi inanufaika vipi na mauzo hayo na kwa nini vifaa muhimu vya taasisi vinauzwa. Jambo hili linajulikana kwa wakuu tu''

Wakina Mkumbo na Zitto ni wajumbe wa kamati kuu. Hakuna kumbu kumbu walizoonyesha kuhusu kujadili suala hilo ndani ya vikao. Endapo kulikuwa na kufunika agenda bado walikuwa na nafasi ya kuuliza katika AOB ili iwe katika kumbu kumbu. Hawakuonyesha hilo kutokea. Walipaswa wapaze sauti zao zaidi ya watu watatu hawakufanya hivyo.
Huku ni kupotosha umma kwa kujifanya hawakuwa sehemu ya uongozi ule ule wanaoutuhumu.

4.''Uongozi wa sasa wa taasisi yetu umefanya tuonekana kwamba taasisi yetu ipo kwa ajili ya kuvuruga amani ya nchi.
Yote hii ni kwa sababu tumekuwa hatuna mbinu mpya za mapambano zinabadilikabadilika zaidi ya maandamano ya kila mara. Kwa kuzingatia utamaduni wa watanzania wa kupenda amani, kuna haja ya kufuta hii taswira na njia rahisi ni kubadilisha uongozi wa taasisi haraka iwezekanavyo''

Vyombo vya dola vimetumika katika kuvuruga mikutano ya CDM. Pale CDM walipoombwa kusitisha maandamano walifanya hivyo. Mkutano uliochukua roho za watu Arusha haukuwa maandamano bali kampeni. Ndivyo ilivyokuwa maeneo kama Iringa watu walipovamiwa ndani ya kikao. Hivyo kusema suala zima ni maandamano na ni kuvunja amani ni upotoshaji.

Hakuna kumbu kumbu Kitila Mkumbo kama mshauri wa chama chao kuelezea athari hizo za maandamano.
Zitto ameshiriki katika maandamano kama yale yaliyopita Tazara, na juzi alikuwa katika mkutano kanda ya magaharibi.
Endapo mikutano ni kuvunja amani basi Zitto alishiriki kikamilifu, kama siyo basi alifanya hivyo kwa unafiki.
Huu ni upotoshaji.

5.. Mpaka hivi sasahakuna mpango wowote wala hata mchakato wa maana kuwa connected na jumuia yakimataifa. 'Mbowe' yupo ‘too local' na hana mawasilianoyeyote ya maana na viongozi wengine katika kanda na kimataifa.
Ndio maana mkuuhuyo na mtendaji wake mkuu wamekuwa hawaonekani katika matukio makubwa yakimataifa. Hata katika kutoa maoni katika mambo makubwa ya kitaifa nakimataifa viongozi hawa hawapo. Kwa kifupi kwa sababu ya aina ya viongozitulio nao, nafasi ya taasisi yetu katika nyanja za kimataifa haipo!'

Waraka umeonyesha sehemu ambayo Mbowe alikuwa Nairobi katika uchaguzi. Tunakumbu kumbu kuwa Mbowe alifiwa na dada yake akiwa Denmark, Dr Slaa alikuwa US hivi karibuni. Slaa ametoa kauli kuhusu tatizo la Rwanda ambayo tuliipinga. Jinsi kauli ilivyowekwa kuna aina ya upotoshaji ili kujenga hoja na si kujenga hoja kwa kuepuka upotoshaji.

6.''Nikwa sababu tumegombana na kila mtu katika utawala wan chi, vikiwemo vyombovya ulinzi na usalama. Ukweli ni kwamba tutavihitaji vyombo hivi kabla nabaada ya kuingia madarakani na ni ndoto kudhani kwamba tutakabidhiwa nchi kwakugombana na kila mtu. Ni kwa sababu ya mtazamo kama huu ndio maana wakuu wetuwa sasa hawaonekani kabisa katika shughuli za kitaifa kama vile sherehe zauhuru wan chi, n.k''

Sidhani CDM inahitaji kupendwa na watawala. Kuna kauli za kina Wasira zisizoitakia mema na hata za mkuu wa nchi kuhusu kutuhumu baadhi ya viongozi kuwa wazandiki. Akina Kitila na Mkumbo wanaamini kuwa uwepo wa ukaribu na viongozi wa CCM utasaidia Chadema kuingia madarakani. Wanaamini kuwa vyombo vya dola vinaweza kufanya haki kama CDM wataacha mikutano. Wanaamini damu za watu ni kwasababu ya viongozi watatu.
Si kweli, chama tawala kinatumia vyombo vya dola na hilo linajulikana kwa kila mtu.
Upotoshaji kusema CDM inahitaji mapenzi na watu walioshindwa kusema chanzo cha bomu Arusha.

Waraka na kashfa ndani yake

Itaendelea

 
7. ''Tunayemataka (Zitto) ni kiongozi anayeweza kuongoza taasisi bila kujenga makundi akijali zaidi kaziya taasisi kuliko maslahi binafsi''

Zitto amehusishwa na makundi mara nyingi. Alikuwa kiongozi wa kundi Kafulila. Ametajwa katika masalia(M7) na sasa ametajwa katika waraka kukiwa na ushahidi wa kimazingira kuwa alishaanza kazi aliyopewa kwa kufuata ushauri kama waraka unavyosema.Kusema kuwa si mtu wa makundi ni upotoshaji.

8.''
Katika kuonyesha mzalendo Zitto ni kiongozi ....amekuwa ndiyemwakilishi pekee aliyeongoza katika kuibua kashfa nyingi na nzito za ubadhirifundani ya serikali hata kufikia mawaziri kadhaa kufukuzwa kazi''

Tuna ushahidi kuwa Zitto aliuza uzalendo kwa Barrick ili wamjengee shule.
Baada ya kupokea milioni 10 suala la Barrick likawa limefikia kikomo.
Kuonyesha uzalendo kwa kuibua kashfa na kuficha unyonge kwa makampuni yanayoumiza wananchi wa chini ni upotoshaji.

9.''
Uwazi: Katika taasisi zetuhizi ni muhimu sana kuepuka kufanya mambo yote wazi wazi hata kama ni mema amani haki ya mhusika ama si makosa katika jamii tuliyomo. Kuna mambo ambayo nihaki ya mtu mfano mahusiano binafsi ya kimapenzi, kuwa na marafiki wa damukutoka upande mwingine wa utawala, nk. Lakini mambo hayo ni muhimu wakatimwingine ama kwa kiwango fulani yakafanywa kwa siri kuepuka mitazamo potofu kwaunaowaongoza''

Kama wanakubali uwepo wa mambo binafsi kama mapenzi kwanini basi katika waraka huu uonyeshe kuwa Slaa ni mhuni kama jamii inavyoona. Hapa wanapotosha umma kuwa kuna mambo yana mipaka wakati waraka wao unamsumanga Slaa kwa mambo yale yale wanaosema yana mipaka. Kupotosha umma kwa hali ya juu

Lakini ukisoma hapo juu utagundua kuwa kuna elements za undugu, ufamilia na marafiki wa damu kitu wanachokiona ni sawa. Wakati huo huo wanaeneza tuhuma dhidi ya ukabila.
Hizi ni double standard tunazoita upotoshaji maana hazina ukweli bali kuwa fabricated ili kuchangaya umma.

10 ''
Mpinzaniwetu hana uwezo mkubwa wa uelewa wa mambo mbalimbali ya uchumi, jamii,utamaduni, michezo, nk. Si tuelimu yake ya darasani ni ya magumashi bali piavipaji na akili ya kuzaliwa havijaonekana katika maisha yake''

Kipaji ni uwezo kwa kutenda jambo katika hali bora kuliko sehemu kubwa ya jamii. Mzee Moris Nyunyusa alikuwa na uwezo wa kipiga ngoma kumi akiwa kipofu, hicho ni kipaji. Si lazima mtu aibue kashfa za ufisadi ili awe na kipaji.
Na wala kipaji hakitegemei elimu ingawa mwenye elimu na kipaji ana nafasi kubwa.

11.''Mpinzaniwetu ni mgumu sana katika kuchangamana na makundi yote ambapo vijana humwonakama si mwenzao kiumri na kifedha, wanawake humwona kama malaya anayependakutumia miili yao kujistarehesha wakati wazee humwona kama mtu anayedhalilishahata nafasi aliyopewa kwa kufanya uhuni waziwazi hata kuvunja ndoa si ya kwaketu bali hata za watu wengine

Ukisoma nukuu #9 hapo juu utaona wanakubali kuwa mambo ya mapenzi ni binafsi. Mbele ya safari wanazusha tuhuma zile zile walizosema ni binafsi. Hii si upotoshaji tu bali unafiki uliopinduukia.

Labda niwakubushe wana duru kuwa kumekua na malumbano mengi hapa jamii forum wengi. Wengi wakisema tuhuma dhidi ya viongozi wa CDM zinatolewa na vijana wa Lumumba.
Ni kweli kuna hilo suala lakini ukisoma waraka wa Kitila na Zitto utaona kuwa tuhuma nyingi zinatoka hapa.

Mfano hili suala la mapenzi limekuwa katika midomo sana kumbe nyuma yake wapo wajumbe wa kamati kuu ya CDM. Tuhuma kuhusu fedha zimekuwa zinatolewa kumbe nyuma yake kuna kundi la wana kamati kuu ya CDM.
Tuhuma za ubadhirifu na ufujaji wa mali zimekuwa nyingi, ukisoma waraka ni wazi zimetoka hapa.

Hatusemi tuhuma hizo hazina ukweli au ni za kweli. Duru za siasa tunaonyesha kile kinachoitafuna CDM.
Badala ya kuelekeza macho yao nje lazima wajisafishe kwanza.

Leo tunafahamu kuwa Zitto kama mwenyekiti wa PAC ameibua tuhuma kuhusu hesabu za vyama vya siasa. Wengi walidhani ni sehemu ya uzalendo.
Na kwa mujibu wa majibu yake ni kweli alichokisema.
Hata hivyo duru tunahoji kama ulikuwepo uzalendo wa pesa za umma.

Ukisoma waraka moja ya tuhuma ni hesabu kutokaguliwa. Kama ni hivyo na ni kosa hesabu kutowekwa wazi na ni kosa kutokagauliwa lakini basi tunafahmu kumbe Zitto alitumia nafasi hiyo kwa uzalendo ili akwee ngazi za chama kwa kumutuhumu mwingine.
Hizi ni siasa mufilisi sana.

Zito na Kitila kama wajumbe wa kamati kuu ya chama walikuwa na nafasi nzuri ya kueleza uozo huo ndani ya chama badala ya kutumia ofisi za PAC huku wakiwa na malengo yao. Hapa ni unafiki na upotoshaji wa umma

Itaendelea....

 
Huyu M2 anastahili kuwa wa kwanza kufukuzwa, kwanza ni mwajiriwa wa chama huyu! utetezi wa Dr. Mkumbo unaeleweka ila chaguo lao yaani MM wamebugi kabisa.
Mdau wakati tunaendelea kuufanyia kazi waraka nikuonyeshe tuhuma za akina Zitto na Kitila
''Mifumoya uteuzi wa maofisa wa makao makuu ya taasisi imevurugwa na siku hizi wakuu wataasisi hasa mtendaji mkuu anateua na kutimua ofisa anavyotaka na mara nyingibila hata kamati ya makatibu na wakurugenzi kujua

Walichokusudia ni kutaka uongozi uache ili waweke watu wao kuibua kile wanachokitaka.
Ukisoma hapo juu wanamtuhumu mtendaji kwa kufukuza watu, lakini waraka huo unahusisha watu kutoka katika ofisi zile zile wanazodai zinafukuza watu hovyo. Hii ni hasira ya watu wao kuondolewa ndio maana tunauangalia waraka kwa kina kabisa bila kumuonea mtu au kumhurumia.

Kadri tunavyosonga mbele tutaaangali upande unaotuhumiwa na 'shea' yao katika mjadala
 
Uroho wa madaraka na mali ndio unaosababisha Tanzania tuendelee katika hali ya ufukara tulio nao. Kila mtu anafikiria ya kwake tu; hata watu tuliodhani wanatutetea kama akina Zito kumbe nao wanatutetea kwa sababu ya maslahi yao binafsi.

Kitila anaonyesha ana akili sana na anajua sana kupanga maneno yake kwa makini kuliko Zitto ila nadhani naye alishindwa kujua njia nzuri ya kupamabana.

Ni kwa bahati mbaya sana kuwa watu hawa, kama ilivyokuwa kwa wafuasi wao akina Shonza (something like that) nao watahamia CCM na na kupewa ukumbi mkubwa sana wa kutangaza kuwa matatazio ya Tanzania yanatokana na CHADEMA. CCM siyo chama imara ila kina raslimali nyingi sana zitokanazo na utaratibu mbovu wa serikali yetu, halafu kinapowapata watu wenye uchu wa madaraka na tamaa kubwa kama hawa basi wanatumiwa kwa nguvu sana kuibakisha CCM madarakani. Angalia Tambwe Hiza leo sijui yuko wapi, na wapo wengi sana katika historia: Nzanzugwaku, Lamwai, Kaburu, Jidulamabambasi (something like that), na wengine wengi sana. Ni kweli kuwa wanatumia haki zao za kikatiba lakini hawazitumii haki hizo kwa manufaa ya nchi.

Migogoro ya uongozi CDM ilikuwa na njia nyingi za kuitatua kitaasisi, lakini timu hii ilipoamua kuwa confrotational basi inawezekana sana kuwa ilichangia sana kutibua kila kitu kwani ni hulka ya binadamu kutotaka kushindwa. Waraka wao ulikokuwa na observations nzuri lakini ni observations ambazo hawakuonyesha kuzichannel vizuri, kwani ningekuwa katika positions zao nisingefanya hivyo na huenda ningefanikiwa sana. CDM wamekuwa wanatumia sana public opinion kumsimamisha mgombea wao. Hakukuwa na ulazima wa kusema hatumtaki huyu tunamtaka yule, wangetumia vigezo vile vile walivyotumia kumsimamisha Slaa mwaka 2010 wangeweza kufanikiwa malengo bila kuvuruga chama chao

Hata hivyo ya ngoswe tumwachie ngoswe, ila ngoswe huyo akikata mti ukaangukia nyumba yetu inabidi tulalamike. Mgogoro huu umeirahisishia sana CCM kurudi madarakani kwa kutumia mtu yeyote watakayemsimamisha hata kama ana uchafu wa namna gani.
 
Inaendelea....

Katika waraka tumeona sehemu zenye tuhuma dhidi ya uongozi uliopo madarakani.
Tuhuma hizo ni nzito na zinapaswa kutolewa ufafanuzi.

1. Kuhusu kipengele cha uongozi kufanyiwa mbinu, je ni kweli kuhusu hilo?
Kwanini uongozi haukurekebisha ulipobaini kulikuwa na tatizo katika uchapaji.
Na kwanini kila mara kumekuwa na mang'uniko juu ya suala hili bila kupatiwa jibu la maana

2. Tuhuma za Mbowe kukopesha chama bila kumbu kumbu
Je, Mbowe anaweza kujitokeza na kuonyesha kumbu kumbu zinazohusiana na madai yake ya fedha kwa uthibitisho?

3.Je, ni utaratibu gani unaotumika katika kutoa tenda na akina nani wanahusika.
Kuna kumbu kumbu zozote za kuthibitisha kuwa tenda zinatolewa kwa kufuata taratibu zilizowekwa na chama?

4. Je, Mbowe ni kweli kuwa una mtu anaye supply vifaa vya chama ambaye hakuteuliwa na chama na kwamba wewe na wenzako wawili ndio mnaofahamu hilo

5. Dr Slaa kwanini hakuna ukaguzi wa fedha kutoka kwa CAG. Je, mwenyekiti wa POAC mh Zitto ambaye pia ni msaidiz wako ameshawahi kukueleza kuhusu hilo, kama ndio kwanini hujafanya kama ilivyotarajiwa, kama hapana ni kwanini.

6. Dr Slaa, utaratibu wa kuajiri na kufukuza ndani ya chama upoje. Nani anayeajiri na nani anayefukuza mfanyakazi.

7. Dr Slaa, ni ipi ratiba ya uchaguzi ndani ya chama ikizingatia kuwa muda wa uongozi uliopo unakaribia kufikia hatima

8. Mbowe, ni upi utaratibu wa kupata viongozi wasiochaguliwa katika chama kama katibu mkuu, katibu mkuu msaidizi

9. Katika madai ya waraka ipo sehemu inayosema kikao kiliamua kuajiri watendaji wa kanda.
Dr Slaa kuna sababu gani za msingi za kufikia miezi 5 hilo halijatendeka

10. Mbowe na Slaa, je kuna utaratibu gani zaidi ya kuchangisha pesa wa kuleta mapato ndani ya chama.


Wana duru tunauliza maswali hayo kwasababu yanaonekana kujirudia rudia katika mitandao kukiwa hakuna majibu ya kuridhisha. Tunaamini kuwa ili tuwe na 'fair trial' ni lazima tufanye 'cross examination'.

Yale tunayoyajua tutayaeleza kwa ukamilifu, yale yenye mashaka yatahitaji ufafanuzi na hii ni sehemu ya fursa hiyo ili kuondoa sintofahamu ndani ya chama.

Tunawakaribisha viongozi, wasemaji au idara za CDM kuweka uwazi.


cc @Dr W.Slaa HAMY-D sixgate Mungi Ben Saanane Ritz Tumaini Makene

Itaendelea....
 
Mkuu Kichuguu ahsante kwa hoja zako naomba nizichangie japo kidogo.
1. Mambo haya si ya ngoswe kwasababu yanagusa masilahi ya taifa kwa namna fulani. Hatupendi turudi kule kwa kikundi cha watu kukaa na kufanya watakavyo kwasababu hakuna 'watch dog'. Upinzani ni sehemu muhimu sana ya demokrasia na hilo hatuwezi kulikataa.

2. Observations zao zingekuwa na maana kama zingejikita katika mkakati wa hoja za kujenga chama chao.
Nilitegemea kama wanalaumu hakuna mkakati wa kuongeza mapato au mkakati wa kisiasa waonyeshe kwa mantiki.
Hawakuonyesha wakaishia matusi kama 'akili ndogo, wahuni wanaopora wake za watu n.k.'

Mkakati wao ulikuwa kupora madaraka kwa njia haramu wakiwa chama cha kidemokrasia.
Walikuwa tayari jengo lianguke ili waje kulijenga upya.

Walichotaka kufanya si kusaidia chama kupata viongozi bora bali viongozi waliowataka wao.
Wakati wanaandika hayo wanalaani taratibu zinazotumiwa sasa hivi.

Nakubaliana mkakati wao hauna tofauti na ule wa Juliana Shonzo. Niwahi kuandika kuwa maneno ya Kitila ya kutaka 'Akina Juliana waachwe ili wabalehe' yalikuwa na maana. Nilisema Juliana alikuwa na nguvu kubwa ambayo leo tunaijua wazi. Ingawa wanasema hawakutaka kutumia mitandao kuhujumu chama ukweli ni kuwa wametumia

Tuhuma dhidi ya Slaa na mkewe zimekuwepo katika jamvi kila siku. Tuhuma za akina Mbowe kupewa tenda, mapiki piki zimekuwepo kila siku. Tuhuma za kufukuza watu makao makuu zimekuwepo. Tuhuma za matumizi ya fedha bila mahesabu tumezisoma sana. Kila mara watu walidhani ni LB7 kwamba CCM wanachokonoa.
Yote hayo yapo katika warakaMbinu za kuwa na multiple ID ndizo zimetumika katika kuleta tuhuma kutoka ndani ya chama. Leo wanaposema hawakutaka kutumia mtando ni ulaghai, wameutumia sana wawe wakweli tu

3. Wanasema Mbowe ana akili ndogo na elimu yake ni magumashi. Nilitarajia wao wakiwa wasomi waone mambo tofauti.
Mtei hakuwahi kugombea urais kwavile alikuwa anajenga chama. Bob Makani alikuwa anaimarisha chama.
Mbowe aligombea akijua ni kutangaza chama na wala si kushinda. Dr Slaa aliingia kama mshindani.

Ni Mbowe mwenye akili ndogo ndiye alikwenda kuwa recruit akina Zitto. Kwa 'akili yake ndog' alifahamu chama kinahitaji viongozi wa baadaye tena wasomi. Sijui hiyo ni akili ndogo zaidi ya ile ya kuzungumzia mahusiano binafsi ya Dr Slaa!!

4. CDM walikuwa na utaratibu mzuri wa kupata hata wagombea wao kutokana na public opinion. Sina shaka kabisa kuwa kilichotokea kwa Dr Slaa kingeweza kutokea kwa Zitto kwasababu ya public opinion.
Hili ni kosa ambalo halikhitaji hata certificate kulitambua. It was just a matter of time wangefika kule walikotaraji.

5. Tumewahi kuzungumzia sana na Mchambuzi kuwa CDM inajengwa na personality na hilo lazima walikomeshe.
Ukisoma waraka kuna sehemu wanasema 'tulete mtu maarufu tukileta siyejulikana itakuwa ni ngumu'

Mbowe alikwenda kuwaibua wasiojulinkana akina Zitto. Vipi hawa wasomi waseme wanahitaji mtu maarufu na si mtu mwenye quality za uongozi? Nani mwenye akili ndogo, yule aliyeibua vipaji au hawa wanaovizia watu maarufu?

Haya tunayoandika si maoni kutoka vichwani au hisia zetu, ni kwa mujibu wa waraka uliopo.
Wamejitahidi kupiga siasa lakini hawakujibu maswali muhimu sana yanayotokana na waraka.

Wao wamekuwa sehemu ya kuchochea mtafaruku na si kupata suluhu.
Ndio maana tunasema huo waraka una makosa na asiyeona ausome kwa uangalifu.
 
Last edited by a moderator:
MAKUNDI NDANI YA CHAMA

Wiki iliyopita tulisema chadema ina makundi yafuatayo
1. Kundi linalowania madaraka (power) ambalo sasa tunalijua ni la Kitila na Zitto
2. Kundi la Wasaliti ndani ya chama
3. kundi la CDM kama ilivyokuwa (Hili ni la akina Mbowe)
4. Kundi Neutral (Lisilofungamana na upande wowote)

Katika makundi hayo tulisema kundi la neutral linaonekana kuumizwa na migogoro. Mchambuzi akasema lipo bordeline.Leo tumeliona likiondoka katika borderline na kuchukua upande

Kundi la kuwania madaraka tulisema ndilo linachochea mitafaraku, halina subira kufika kileleni kwa mikakati yoyote.
Leo tunalijua

Kundi la CDM kama ilivyokuwa;
Hili ni la viongozi wa sasa wasiokubaliana na mabadiliko ya kijamii na kisiasa .
Linapenda consensus kuliko kufuata principles au kubadilika.
Ni kundi la wahafidhina kwa kiasi fulani.Ni kutokana na hilo kundi hili linapenda kupanga na wala si kushindana.

Kundi la wasaliti: Tukasema wapo watu ambao ni sehemu ya usaliti wakitumia na maadui wa CDM. Kwa bahati nzuri kundi hili limejinasibisha sana na 'kundi la madaraka' likiamini kuvunja nguvu za sasa ni kazi kubwa kuliko nguvu zijazo.

Tuliandika huko nyuma kuwa suluhu ya CDM ni kutafuta dawa ya kudumu na wala si kutumia asprin kutuliza maumivu. Uongozi uliopo umezembea katika suala hili kwa hofu ya kuudhi personality.

Kulikuwa na kila aina ya viashiria kuwa hali si shwari, tahadhari hazikuchukuliwa.
Leo zinachukuliwa hatua katika wakati mgumu na nyeti sana.

Uongozi umechukua hatua na kusahau factor(s) nyingine muhimu na hivyo kuwa vulnerable zaidi kwa 'maadui' wao wa nje.Ilipaswa uongozi utafute chombo neutral ili upate nguvu ya kusimamia maamuzi kwa uadilifu, uangalifu na weledi.

Endapo uongozi ulikuwa na waraka huu ambao ni ushahidi unaojitosheleza kwanini kisIundwe chombo neutral au kutumia baraza la wadhamini ili kupata suluhu. Hili lingeambatana na hatua ambazo zisingeweza kuwaacha vulnerable zaidi.

Pamoja na matatizo yaliyojiyokeza ukweli unabaki kuwa kuna kila sababu ya kufanya reform. Njia njema ya kufanya reform ni kufanya uchaguzi. Kupitia uchaguzi wa wazi na kidemokrasia CDM inaweza kupata viongozi watakaoamsha hamasa ambayo sasa imegawanyika katika political base yao.

Kwasasa hivi hakuna kitakachofanyika kama mageuzi ya haraka ya kidemokrasia hayatafanyika.
CDM ipo vulnerable kwa maadui wa nje na wa ndani wenye sentiments kutokana na viongozi wao kueneguliwa.
Hivyo wasibweteke kuwa kazi imekwisha, in fact ndio imeanza na itawavuruga kama hawatakuwa makini.
 
Last edited by a moderator:
Wanajamvi
Kuna swali nimeulizwa pembeni na pengine tuliangalie wote kwa pamoja.

Swali: Je hatua ya CDM kuwakatalia Zitto na Mkumbo kujiuzulu ilikuwa sahihi? Je haikulenga kuwadhalilisha au kukiumbua chama kama waraka huo ambao sasa umetoa habari za ndani za chama?

Jibu:
Hatua ya uongozi kuwakatalia kujiuzulu ilikuwa muafaka kabisa. Tunakumbu kumbu kuwa mgogoro umekuwa unafukuta kwa kwa muda mrefu. Tunasema wale waliokuwa wanashambulia CDM mitandaoni kwa habari za ndani ndio hawa wenye waraka. Madai yao yapo katika waraka na hata waraka umethibitisha kuwa waliamua kutumia ID feki katika shughuli zao.

Endapo wangeachiwa wajiuzulu hilo lingekuwa kosa kubwa sana.
Hakuna ambaye angeweza kutoka hadharani na kueleza kiini na sababu za kujiuzulu kwao.

Zingebaki hisia miongoni mwa watu. Kuna uwezekano mahasimu wa CDM wakachukua habari hiyo na kuifanyia spinning katika ukanda au ukabila na hilo lingeleta 'mantiki'hata kama si kweli.

Pili, viongozi waliotuhumiwa wangeweza kabisa kuendeleza mbinu zao kwa remote kwa kueleweka kama watu walioamua kuepuka majungu, ubaguzi n.k.

Hilo lingewapa nafasi ya kujijenga upya tena kwa nguvu kubwa isiyo na gharama.
Huo ndio ulikuwa mkakati wao kukimbilia kujiuzulu.

Tatu, hilo lingewaondoa katika kashfa ya Mwigamba. Ingeonekana kama Mwigamba alikuwa 'solo'

Maamuzi ya kuwakataza wasijiuzulu ni sahihi kabisa.
Maamuzi niliyo na shaka nayo hasa uelewa wa washabiki, manazi na wapenzi ni pale ambapo spinning itafanyika ili uongozi uliotoa adhabu uonekane onevu.

Kuna atakayesema kama Mbowe na Slaa ni watuhumiwa, haki ilitendekaje wakati wao ndio walioshtaki, wakaendesha mashtaka na kutoa hukumu?

Well, ndio maana tuliwaambia CDM watafute chombo neutral ili kuondoa hisia hizo.
Kwa bahati mbaya hawakufanya na hilo litabaki kama donda wakati huu wakiuguza mengine makubwa.

Nadhani hasira, jazba na kukosa mbinu kulipelekea baadhi ya maamuzi bila kuzingatia hali ya kisiasa ikiwa ni pamoja na weledi wa sehemu ya wanachama.
Na wala sikuona sababu za kufanya uteuzi kujaza nafasi ambazo hazina dharura kwa wakati huu

CDM walitakiwa wachukue muda ili kutuliza hali, kusoma mazingira na kutafuta njia mbadala itakayowaondoa katika vulnerability ambayo itaanza muda si mrefu.
 
Naam,

Sijachelewa kuingia ukumbuni,japo sijakaribishwa kwa ukamilifu lakini natia timu hivyo hivyo,

Nguruvi3,with all of my due respect hapo juuu mwanzo wakati unaianzisha hoja hii umesema wazi kabisa kwamba hapa watu tuwe huru,tueleze uhalisia wa kile kilichopo na bila woga na hofu yoyote,SHUKRANI KWA HILO..

Lakini niuleze swali,katika al mujadla huu ruksa kuchagua upande??kwani napokusoma kwa ndan sana nakuona unauma na kupulizia huku ukichagua upande wa mbowe na slaa kuutetea na kuchagua upande wa zitto na kitila KUUKANDIA,why??


Well,may be wewe tayar umeshachagua upande,ila hata hivyo sina haja,kama wewe umechagua upande ama haujachagua,mimi nasema wazi wazi kwamba mimi upande wangu ni UPANDE WA WALE WANAOPIGANIA MABADILIKO NDAN YA CHAMA BY ANY MEANS NECESSARY,MADAM WAO WANAPIGANIA MABADILIKO YATAKAYOONDOA UUNGU MTU,SIASA ZA KUOGOPANA NA DEMOKRASIA MAGHILINI NDAN YA CHAMA CHA CHADEMA,BASI MIMI NA AKILA MTANZANI MWENYE KUTAKA MABADILIKO LAZIMA ATALIAFIKI HILO (TEAM ZITTO)

Nguruvi3,si kweli kwamba ndan ya chama hiko watu hawajatumia njia za kidemokrasia kuonesha nia yao ya kutaka kupewa na fasi ya wao m kukitumikia chama hiko,siyo kweli hata kidogo,ili mtu uweze kupata picha ya kukifanya kitu flan let say kuomba ridhaa ya kuongoza,lazima kwanza uoneshe nia hiyo wazi wazi ikiwemo na kuitangaza nia hiyo na kuangalia mrejesho wa wale unaowatangazia nia hiyo ukoje,

Zitto alishaonesha nia hiyo tokea muda mrefu sana,kwa kutamka wazi wazi na kwenye viwanja halali kabisa,lakin unakumbuka kilitokea kitu gani??mara baada ya yeye kuonesha nia ya kuitumia haki nyake hiyo kikatiba na kidemokrasia basi ikawa ni zengwe mtindo mmoja,simu zilipigwa kutoka kila sehemu za watu mbali mbali kulaani kitendo kile,simu zilipigwa hadi kutoka TENGERU KWA MZEE MTEI, ziklaani kitendo hiko na kusema muda bado na zitto aache uroho na kukigawa chama..!!,kukigawa chama tena??yan kwa mtu kuonesha nia ya kutumia haki yake kidemokrasia ndan ya CHAMACHA DEMOKRASIA NA MENDELEO INAKUWA TENA LAWAMA NA KUSEMA KWAMBA ANAKIGAWA CHAMA??KIVIPI SASA??

Hapo hoja iko wazi kabisa,hoja mama dhidi ya haya yote ni kwa wahafidhina ndan ya chama hiko kutokuwa tayari kuwa challanged kwa namna yoyote ile hasa ukizingatia muda wa kufanyika kwa uchaguz umeshawadia,na wao wanahisi kwamba bado wana nafasi ya kuendela kuwatumika watanzania,inshort MBOWE & SLAA NA WAHAFIDHINA WENGINE THEY HAVE UNFINISHED BUSSNESS TOWARD 2015,SASA WANAPOONA KUNA HATI HATI YA MTU KAMA ZITTO(INTRUDER)ANATAKA KUINGIA KATI NA KUHARIBU PLAN HIYO WANA KUWA WAKALI NA KUTAFUTA KILANAMNA YA KUMJERUHI KWA KUTUMIA CHARACTER ASSISSNATION NA KUAMINISHA UMMA WA WATANZANIA KWA PROPAGANDA UCHWARA ETI KWAMBA ZITTO ANATUMIWA NA CCM PAMOJA NA USLAMA WA TAIFA,,HILO HALIPO NA WAHAFIDHINA IFIKIE HATUA KWA SASA WAUKUBALI UKWELI NA WAPISHE MABADILIKO,WAWE WAUMINI WA KWELI WA DEMOKRASIA,

Wilbroad Slaa(KAMBI YAKO),ambae kwangu mimi kwa sasa namuona kama ni kiongoz MPUUZI NA ALIEKOSA MAONO NA MWENYE UCHOVU WA KIFIKRA NI TATIZO KUBWA SANA NDAN YA CHAMA,
samahani natumia lugha kali dhidi yake lakini naweza kuthibitisha kwa nin namuita kiongoz huyo ni mpuuzi na mwenye kupaswa kupumzka,

Mara kwa mara humu jukwaani tumeona yanatokea magroup ya watu wasio fahamika ndan ya chama hiko kwamba hao ni kina nan,wana uongoz gan ndan ya chama,wanatumwa na nani na kadhalika kama Yerikcko Mdandia nasaba ya nyerere na Ben Masaa manane kuja kueleza mambo chungu tele yenye ukakasi na kumtukana zitto na watu wengine wanaonekna kwenda kinyume na mawazo yao huku WILBROAD SLAA AKITOKELEZEA NA KUJA KUWASHANGILIA WATU KAMA HAO??ZIPO TETESI AMBAZO TUNAZISKIA YA KWAMBA WATU HAO AMBAO KWA SASA HUMU JF HUONEKANA KAMA NI MATAPELI WANATUMWA NA WILBROAD SLAA.

Sasa Wilbroad Slaa naibu wake anatukanwa na kudhalilishwa mitandaoni bila ya ushahid bila ya kufuata PROTOKALI kisha yeye anatokezea kuja kushangilia je NIKISEMA WILBROAD SLAANI MPUUZI NA M.PU.MBA.VU NAKOSEA??Usichukie Nguruvi3 upumbavu na upuuzi sio tusi,RAFIKI YANGU NINAEMUHESHIMU SANA Invisible analitumia neno hilo na kusema kwamba "FICHA UPUMBAVU WAKO NA UONESHE WEREVU WAKO NA BUSARA ZAKO",,
Sasa najiuliza kwa nin Slaa hafichi u.p.umba.vu wake na kuonesha busara zake yeye kama KATIBU MKUU WA CHAMA??kwasababu haiwezekani wewe naibu wako anatukanwa kisha wewe uje ushangilie,kwani yeye zitto haumii???yeye ni binadamu na ana nyongo,Slaaalikua anadhani vipi??huo ni mfano mmoja kukuonesha kwamba kulikuwa kuna Mpango wa kufanya Character Assissnation ili lengo la wahafidhina na waungui watu ndan ya chama litimie kuelkea kwenye uchaguz huu unaokuja..


Either Kuhusu huo unaosemekana kama waraka wa siri,zitto amekanusha kuwa hausiki nao,na hata hao viongoz wa kamati k,uu hawajamvua vyeo vyake zitto kwa kuhusika na waraka huo..

Sababu walizomvua nazo uongoz ni zile zile za kunyoosheana vidole vinayvofanywa siku zote ndan ya chama hiko,

Ni vigumu sana kuonesha nia ya kutaka kuleta demokrasia ndan ya chadema kwa kuwa wao wenywe sio waumin wa hiyo demokrasia,

Chadema wanapata wapi MORAL AUTHORITY YA KUSEMA KWAMBA WAO NI WANA DEMOKRASIA ILI HALI NDAN YA KATIBA YAO KIPENGELE CHA UKOMO WA VIPINDI VYA MADARAKA HAKIPO??WANA TOFAUTI GANI SASA NA MUGABE AU MUSEVENI??UKOMO WA MADARAKA HAUPO,KISHA WATU WAKIONESHA NIA YA KUTAKA KUITUMIA HAKI YAO YA KIKATIBA HUONEKANA MAMLUKI NA WASALITI KWAN NIN??AU KWA KUWA HAWANA NUMBER ONE QUALIFICATION YA KWAMBA LAZIMA BARAKA ZITOKE TENGERU KWA MZEE MTEI??HAYA MANENO YANAWAUMIZA BAADHI YA WATU,LAKIN SASA TUFANYAJE??BORA TUSEME TUH NA KILA MTU ASIKIE,YAN MTEI AMEKUWA KAMA AYATOLLAH ALKHEMENEI??

Madam wamesema kuwa hiki ni chama cha demokrasia basi waoneshe uhalisia wa hayo wanayoyasema,WATANZANIA WA SASA SIO WALE WA 2010,HILO LIFAHAMIKE WAZI,HILI SUALA LA ZITTO KABWE(TEAM YANGU) NI ZITO NA CHADEMA WASIPOKUWA MAKINI LITAWAGHARIMU MILELE,
 
Last edited by a moderator:
The Big show
Kwanza narudia kauli yangu kuwa tusimame katika ukweli na nasimama na neno hilo.Mwanzo wa bandiko nimesema tujadili waraka kama ulivyo na waraka uliopo ni wa Kitila na Zitto. Nilisita kuendelea kama alivyoshauri Mag3 ili tupate upande wa pili wa utetezi, ambao nao umewekwa hapa. Hatujadili hisia tunajadili waraka ndio maana nimekuwa nawanukuu ili kuonyesha sichomeki hisia bali najadili kile kilichopo mbele yetu.
Sababu kubwa ni kuufanyia kazi huo waraka ambao wamekiri upo na wamekiri makosa wao wenyewe.
Hakuna njia nyingine ya kuujadili waraka huo kwa namna tofauti tutaujadili kama ulivyo.

Kikubwa zaidi nimejaribu kueleza nafasi yangu kuhusu maswali tunayoulizwa.
Ndugu Torch kauliza je waraka una ubaya gani? Nimeonyesha kwa mtazamo wangu makosa ya waraka huo na katika kufanya hivyo itaonekana kuchukua upande, waraka ni wa Kitila ni makosa kumhusisha Mbowe kama mwandikaji.

Kuhusu mbinu za watu kujaribu kuleta mabadiliko, mara nyingi nimeunga mkono ushindani ndani ya chama.
Nimewahi kuandika kuwa utamaduni wa kupita uchaguzi bila mpinzani ni ujinga na sasa ufike mwisho kwa vyama vyote.

Lazima kuwe na chechecheo. The Big sjow hivi kweli chekecheo tunalolitaka ndio waraka huo tunaousoma!
Yaani sera za chama zinaandikwa na wasomi kuhusu mapenzi ya Dr Slaa, tena kuna kipengele wanakubali ni mambo binafsi.Utaona ni waraka ulio dhalili kiasi siamini aliyeandika ni Kitila, nahisi ni Juliana ! Honestly

Mbinu za kuleta mabadiliko hazifanywi kitoto namna hiyo kwa kuzua uongo na kudhalilisha watu.
Nimesoma waraka na wewe umeusoma naomba unionyeshe wapi kuna substance inayoweza kuamsha fikra zako kama mpenda mabadiliko, please the big hebu tujadiliane.

Tatu, nimeonyesha kuwa wale wanaochafua CDM mtandaoni na pengine kudhoofisha jitihada ni hawa hawa unaosema wanaka mabadiliko.Nimeorodhesha tuhuma zote ambazo zinaletwa na watu ambao wanajifanya ni CCM kumbe ni akina Kitila na Zitto ambao wamekjiri waraka ule usio na chembe ya mabadiliko.

Nimeonyesha kuwa Juliana na wenzake ambao Kitila aliwaandika makala Raia mwema kuwa 'waachwe wabalehe' walikuwa wanatumika kuvuruga chama. Rejea post za nyuma na za duru za siasa tumeweka wazi kila kitu kabla hakijatokea.Tumeweka kiti moto akina Salaa na Mbowe bila huruma lakini hili la waraka ni aibu sana.

Kama Kitila na Mkumbo hawakuridhika na mwenendo walikuwa na nafasi nyingine za kukisaidia chama.
Hawa ni watu maarufu ambao wanachama wangewahitaji kwa namna yoyote bila kuwa na kikwazo.
Wangejiuzulu nafasi zao wakiendelea na mikakati positive ya kujenga chama si waraka huu hafifu.

Hatukuwasikia hata siku moja bali walikuwa wanachochea maasi ya kuondoa viongozi kwa njia ya ufitini knyume na misingi ya kidemokrasia ya chama chao.Kampeni za CDM zimekufa kumbe ni hawa watu na nashangaa unawatetea.

Nimewauliza akina Slaa na Mbowe kuwa tuhuma dhidi yao ni nzito na zenye kufikirisha ndio maana tumewataka wajibu.
Haina maana waraka wote ni null and void, no thank you! lakini hauna substance za mabadiliko na wala hauwakilishi kundi la wasomi kama wanavyojinasibu.

Nikupe challenge mkuu, hebu nionyeshe wapi ambapo unadhani nimechukua upande kwa kuangalia waraka huo.
Nukuu zipo na maoni yangu yapo, waspi sikutenda haki.

Nimalizie kusema, hata kama jambo lililokusudiwa lilikuwa jema ukweli ni kuwa halikufanyika katika njia njema na hakukuwa na mantiki zaidi ya kiu na uchu wa madaraka. Kutoa takwimu zaupande mmoja ni majungu na hilo nabaki kulisema hivyo.

Hebu tujadiliane
 
Last edited by a moderator:
Arguably, wapo watakaodai kuwavua nyadhifa wahusika wa sakata ni maamuzi sahihi. Bado nasimama hoja uamuzi unaweza kuwa sahihi lakini njia zilizotumika hazikuwa sahihi, zinaacha loophole, ni pande mbili husika kulitakiwa kuwe na chombo kingine.

Kwa uapnde mwingine maamuzi yalikuwa ya jazba kuliko busara.

Kuwavua uongozi watu maarufu ni jambo zito na lilihitaji ‘cooling effect''

kwamba uongozi ujipe muda wa kutathmini nini cha kufanya kuhusu nafasi mbali mbali.


Kitendo cha kuteua kuziba nafasi kililenga kupeleka ujumbe kuwa nafasi ya katibu mkuu msaidizi imeshazibwa na hakuna atakachofanya kuhusu hilo.

Ni ujumbe kwa wafuasi kuwa hatua zitachukuliwa tena kali kama harakati zitaendelea.


Hii ni jazba, haikuzingatia mazingira mengine yanayoweza kuambatana au kuambatanishwa na teuzi hizo. Ilikuwa muhimu kuwa na muda wa kutafakari na kupambanua zaidi ya kukurupuka.


Kwa sasa CDM ipo katika crisis, inaonekana kuwagawa wanachama katika makundi.

Hilo si jambo jema kwa wakati walio nao .


Hakuna shughuli za chama zitakazoendelea huku kukiwa na manung'uniko na maswali ambayo hayajajibiwa.Wapo watakaoamini katika mitazamo tofauti na hilo lita paralyze shughuli za chama.


Katika nchi zenye utawala wa demokrasia na utawala bora, CDM ingeitisha uchaguzi.

Crisis iliyopo ikihusisha ofisi kuu na wajumbe wa kamati kuu ni ishara ya kutokuwa na imani na uongozi .

Mataokeo ya ‘vote of no confidence' yangeshangaza endapo lingefanyika hilo.


Kimantiki tukubali kuwa CDM ipo njia panda ili kurejesha mwamko, imani na hamasa kwa wanachama lazima uongozi ujiridhishe kuwa unakubalika au la.

Njia ya kufanya hivyo ni kupitia uchaguzi ili safu ya uongozi iingie.


Chaguzi huwa ni crisis kwa vyama vyote na inachukua muda kupona(healing).

Kunapokuwepo na looming crisis kama hii, time constrains kutokana na matukio yanayokuja ya kitaifa, CDM haina muda wa kupoteza tena.


Ni vema uongozi ukafuata taratibu za kiungozi kutafuta ridhaa wakati huu muda ukitoa nafasi. Vinginevyo ni kulundika matatizo ili yashughulikiwe siku moja, ni tatizo kubwa.


Ningewashauri viongozi waitishe uchaguzi kwasababu kimantiki kuna vote of no confidence tayari. Uongozi wa CDM utafute mandate tena au wanachama waamue vinginevyo . Kwasasa hakuna kitakachofanyika.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…