Durusuni Somo Hili, Kazi kwenu Mabingwa.

Junius

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2009
Posts
3,181
Reaction score
144
DURUSUNI SOMO HILI.
Durusuni somo hili, Kwanini hamdurusu?
Somo hili Kiswahili, kingereza hakihusu,
Durusuni msifeli, somo lote siyo nusu.
v
Somo kaleta Mwalimu, Pamoja na mtihani.
Wanafunzi kufahamu, imekuwa tafurani.
Wamebaki kulaumu, tatizo hawalioni.
v
Mwanena ngumu topiki, eti hamuoni ndani!
Kudurusu hamutaki, mutajuwa kitu gani?
Kufeli mukidiriki, lawama zende kwa nani?
v
Munakhiyari “twisheni”, hiyo ndo suluhu gani?
Mnakesha vikaoni, darasa mnalikhini.
Somo lipo vitabuni, sasa mwajadili nini?
v
Somo hili tangu kale, limekuwa tatanishi.
Kila kukicha kelele, vineno neno havishi.
Huyu akitaka vile, mwengine huwa mbishi.


v
Musizinge ukakasi , hebu rudini durusi.
Hakuna haja matusi, vitisho na usabasi.
Somo lenyewe rahisi, wa nini tena uasi!
v
Someni na durusuni, waiteni wadarisi.
Herufi zote piteni , musiwache sentensi.
Nahau dadavueni, semanti na sintaksi.
v
Chambueni tamathali, za semi na viambishi.
Msisahau methali, na sarufi patanishi.
Na kanuni za usuli, nomino na viambishi.
v
Nahitimisha tamati, somo nakuwachieni.
Junius ninaketi, narejea darasani.
Mabingwa na wenye viti, kazi kwenu durusuni.
v
Junius,
24/7/2009
 
wasomi wakipuuza kitabu na wakiendelea na porojo tu, somo si lazidi kuwa gumu????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…