E FM : Sport HQ ni kipindi cha matangazo si michezo

Kumbe wengi hatupendi! nilijua mimi tu. Kiukweli matangazo yamezidi mno.kuna mda mtangazaji anaongea unashangaa tangazo limeingilia kati.matangazo yawepo ila yaje kwa utaratibu na yasiwe mengi kupitiliza
 
Sikiliza wapo radio FM kuanzia saa mbili ahsubuhi mpaka saa nne.

Kwanza Kuna wachambuzi Bora na waendeza kipindi wako vizuri sana.

Pia sikiliza U Live kwenye UFM jioni saa kumi kamili mpaka saa moja jioni jumatatu mpaka ijumaa.

Clouds walikuwa vizuri siku hizi wameharibu kabisa.
 
c nusu ni robo tatu wanaenda break kuachia matangazo ila wakirudi ni matangazo tena
 
Matangazo ndo husababisha hao watu wawape habari
 
UFM inapatikana kwa masafa ipi? Au ndo Upendo Radio?
 
Mambo yao waachie wenyewe, fanya mambo mengine...
 
Hiki kipindi ni michosho sana kubabake, yani kila dakika ni matangazo tu.

Sijui hawa mapresenter wanatuchukuliaje yani
 
Sikiliza U live, kuanzia SAA 10 alasiri hadi SAA 1 jioni, kuna wachambuzi wa maana tena wa kutukuka.

Geoffrey Mwamnyayi (Mvinyo)
Salama Ngale (super woman)
Gharib Mzinga (super G)
Omary Katanga (mlinda mlango)
Mussa Kawambwa
Ayubu Hinjo
Rashid Seif
Rashid Khamis (mzee wa Povu)
Henry Sempa
Mohamed Simba Ulanga
Mvula Jr (wonder Kid)

Etc.
 
Tatizo lako huna a,b,c's za Mass Media, PR and Advertising na ndiyo maana unazoza ( unabwata ) tu hivi.

Hayo Matangazo mengi ndiyo Faida ya Uwekezaji ya Mmiliki ambayo pia ndiyo inamuwezesha kupata Jeuri ya Kuwalipa Mamilioni ya Mishahara hao Wafanyakazi wa EFM.

Na siku zote Advertisers hawaendi kuweka Pesa yao katika Kipindi cha hovyo hovyo na ambacho hakuna Audience wa kutosha. EFM ( hasa Sports Headquarters Program ) kina Matangazo mengi kwakuwa ndiyo the leading morning Sports Show kwa Tanzania nzima na inavuta Wasikilizaji wengi hivyo kufanya Advertisers wengi kuwa na uhakika kuwa wakiweka hapo Product yao itasikika na wengi, kwa uharaka na Matunda ya Wateja wengi kuwapata.

Media nyingi za Tanzania hazina Financial Muscles za Kulipa Mishahara mikubwa au mingi hivyo wanachokifanya na kuhakikisha wanahimiza Ubunifu kwa Watangazaji wao, wanatengeneza Programs zenye mvuto Masikioni mwa Wasikilizaji na Kuajiri Watangazaji wenye Influence katika Jamii ili kuongeza Kupendwa na Kukubalika Kwake.

Hata hivyo kama Wewe utawaahidi Watangazaji wa Sports Headquarters ya EFM na Mmiliki wake Majizo kuwa waachane na hayo Matangazo yao mengi na Mishahara yao Minono utawalipa litakuwa ni Jambo jema mno ila kama nawe ni Ngumbaru ( Masikini ) tu kama Mimi GENTAMYCINE basi nakushauri uwe Mvumilivu na ukae Kimya sawa?
 
Nakazia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…