Ila honestly Mama SSH anaweza jambo gani ambalo mtu anaweza akamtetea nalo??!! Nchi inataka kurudishwa kwenye ukusanyaji wa mapato kupitia mifumo ya watu binafsi kama enzi za maxmalipo.
Hapo Kenya tu wanapojisifu kuwa wapo mbele kwenye masuala ya Tech na e-Government katika kipindi cha kuanzia 2015 hadi sasa tumewaacha mbali sana, hadi sasa mfumo wao wa kutoa huduma za serikali kidigitali na kukusanya mapato (eCitizen) upo chini ya Kampuni binafsi na kwa ripoti ya ukaguzi ya mwaka huu mfumo huo umeonekana kutokuwa na taarifa sahihi za yalipo mapato ya zaidi ya TZS bilioni 300 (
Auditor General raises concerns over Ksh.15.5B eCitizen revenue statements), Huku ndiko Mama SSH anataka turudi??!!
Anataka turudi kwenye kila mamlaka ya maji kuwa na mfumo wake wa bili??
Mungu amjalie maono mema huyu mama. Nnauye na January Makamba hawastahili hata kidogo kuwa kwenye wizara nyeti za nchi hii ama kusimamia masuala yenye maslahi mapana ya Taifa. Hao vijana wawili ni walafi na wana tabia ya kudhani wako na haki ya kupata jambo lolote walitakalo kwa maslahi yao binafsi.