Either Katiba Mpya au Maandamano Kwa Mwezi Mmoja

Either Katiba Mpya au Maandamano Kwa Mwezi Mmoja

IoT

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2014
Posts
1,057
Reaction score
1,402
Leo hii Report ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali 2019/2020 imewasilishwa Bungeni. Kinachoshika headline kwa sasa ni juu ya ubadhirifu/ufisadi, pamoja na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi.

Tukiangazia kwa mapana, tutagundua kuwa hata report za ukaguzi kwa miaka ya nyuma zimekuwa zikifunua ufisadi mwingi unaofanywa na Taasisi na viongozi tuliowapa dhamana ya kutumika kwa maslahi ya Taifa letu.
Pamoja na hayo yote, hakuna hatua za dhati zimechukuliwa kuondosha huo ufisadi—kwa kuwachukulia hatua hao wabadhirifu wa fedha zetu.
Wananchi pia tumekuwa tukijadili kuonyesha masikitiko yetu, baadaye tunasahau kwa muda na kukumbushwa machungu kwa mwaka unaofuata.

Ikiwa tuna nia ya dhati ya kukomesha ufisadi, pendekezo langu ni kudai Katiba mpya kwa nguvu zote au kufanya maandamano ya kuishinikiza Serikali kuchukua hatua juu ya ufisadi huu. Vinginevyo, tutaendelea kushuhudia ufisadi usio na kikomo, na kila Rais akituhumu Tawala zilizopita kwa ufisadi, lkn baada ya muda nao hutuhumiwa kwa ufisadi—a vicious cycle.

Mwisho, tusitegemee maajabu sana kwa Rais mpya.
 
Leo hii report ya ukaguzi wa hesabu za Serikali 2020/2021 imewasilishwa Bungeni. Kinachoshika headline kwa sasa ni juu ya ubadhirifu/ufisadi, pamoja na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi..
This is an oversight responsibility of the National Assembly; sio swala la taxpayer mmoja mmoja. Taxpayers wanachohitaji kufanya ni kuongea na wawakilishi wao na kuwaeleza wanachotaka kifanyike.

Haiwezekani sisi watu mmoja mmoja tukaisimamia Serikali. Kama kuna mtu anaamini hilo linawezekana, basi hakuna hata haja ya kuwa na Bunge!
 
Katiba Mpya kwa Bunge lipi?
Maamuzi mengine labda sio a Katiba Mpya kwa sasa
Bunge livunjwe period!
 
Leo hii report ya ukaguzi wa hesabu za Serikali 2020/2021 imewasilishwa Bungeni. Kinachoshika headline kwa sasa ni juu ya ubadhirifu/ufisadi, pamoja na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi...
Kabisa katiba mpya ni lazima la sivyo madudu yataendelea kuwepo.
 
Tumeshindwa kuandamana kwenye vifurushi vinavyotugusa moja kwa moja ndio tuandamane kwa katiba mpya. Rais wa sasa ndio alikuwa mwenyekiti mwenza wa bunge la katiba sijui kama anaweza kufanya uturn kama alivyofanya kwenye urais
 
Back
Top Bottom