El Phenomenon

Gautten Potten

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2022
Posts
1,642
Reaction score
3,426

Ronaldo Luis Nazario Délima mzaliwa was Rio Dejaneiro mnamo 1976 September 18 ni Moja kiumbe hatari na gwiji la kihistoria katika Mchezo wa soka ndani na nje ya Brazil kuwahi kutokea.

Kati ya Miaka ya 1994 na 1999, Ronaldo Nazário alifunga mabao 115 katika michezo 134 kabla ya jeraha lake la kwanza la goti lililomkuta akiwa Internationale Milan.

Psv Eindhoven
Mechi 57, Goli 54, Assist 7.
Fc Barcelona
Mechi 49,Goli 47, Assist 13.
Unaweza Kuona Conversion rate yake ilivyokuwa hatari.

Alifanya matukio ya kutisha kwa mabeki na makipa akiwa na 17 Hadi 22 katika ardhi ya Spain hata Italy.

Ndiye Mchezaji pekee aliyeweza kufunga mara 88 kwa kulamba vyenga magolikipa, kuaakalisha-kuwazunguka na Kisha kufunga.

Zifuatazo ni baadhi ya kadhia walizokutana nazo makipa :
Brazil vs Ghana 2006
Kingson vs Ronaldo na ndio Goli lake la mwisho katika World Cup.
Akifunga Mabao 15 katika Michezo 19.


Mtu anapandishwa viazi na kuacha Goli wazi Serie A.


Shughuli hii ya kuwarubuni na kuwalaghai Makipa aliianza mapema Sana na katika umri mdogo mno.


Mabeki kama Paolo Maldini, Fernando Hierro, Franco Baresi, Desailly, Cafu, Roberto Carlos, Costacurta, Nesta, Cannavaro, Thuram na wengineo. Generation ya vyuma hiyo hakuna mzembe,Kolo wala kilisha hapo.

"Ni ngumu kummaki hata umpake rangi kichwani
kwa miguso yake.
Mguso wa kwanza tu ashakuacha, wa pili anakuvuruga, kisha wa tatu anakudhalilisha vibaya sana. Alikuwa kama mgeni kila nikikutana naye" - Cannavaro.

"Ulikuwa ndio wakati pekee nilipomuona Maldini akiwa na wasiwasi kibaruani kwake.
Akaniambia 'Marcel, inabidi ukae karibu yangu. Nahitaji msaada wako hapa, lazima tumuongezee Lindo huyu mtu sio wa kawaida ni
mchawi." - Marcel Deasilly

Ronaldo ni mchezaji pekee kuwahi kumtisha Paolo Maldini! na kuivuruga Safu yake ya ulinzi Hadi kupewa Jina la Elphenomenon.

Maldini
- "Nilikuwa na bahati ya kutosha kucheza dhidi ya Ronaldo. Alikuwa mtu wa ajabu na hatari Sana na mpinzani mgumu kuliko kuwahi kukumbana naye baada ya Maradona, R9 ndiye mchezaji mkubwa zaidi ambaye nimewahi kumfesi."

Pichani Maldini na Kipa wake walishaungwa tela, Billa mbinu chafu R9 alishamaliza Kazi.


Bila mbinu Chafu Paolo hakufua dafu kwa Délima.


Ni mwamba aliyepotea kwa miaka miwili baada ya kuumia goti na kurudi kuupiga Timu ya Taifa akiwa na goti Moja na kutwaa Ubingwa wa Dunia.
⠀⠀⠀⠀⠀⠀⠀⠀


Happy Birthday El Magnifico.
Ametimiza miaka 47.
Asante kwa kukonga Nyoyo zetu wakati wote uliokuwa uwanjani.
🥇🥇🥇🥇.
 
Ronaldo Bora ni yule wa Barcelona, wanaomsifia Messi au Ronadhino wakatafute clip zake akiwa Barca. Akiitwa computer, alikuwa akiingia ndani ya box anavuruga ngome mzima na kuongeza Kasi.
Michezo mibovu ya rafu ya mabeki was Italy iliyowafanya kina Marco Can basten, Ruud Guilt na Frank Ricard kutumia magoti na kustaafu mapema ndiyo ilimkumba Ronaldo de Lima na kupata majeraha ya goti.
Alipohamia Madrid mtindo wa kufanya mazoezi Mar moja ulisababisha aongezeke uzito ingawa haukupunguza Sana makali take, Ferguson anakumbuka namna alivyoadhibiwa old Trafford.
Jina la El Phenomenon alilipata alipohamia AC Milan baada ya kuanzia kuwatesa mabeki na kufunga Kila mechi kabla ya kupata majeraha mengine ya goti. Kipindi yupo Milan aliweza kupunguza uzito na kurudisha makali take.
Yeye alikuwa namba Tisa aliyekamilika ambaye alikuwa ana uwezo wa kupangua ngome na kufunga magoli wengine ni Kama George Opong Weah ukiacha namba Tisa wengi wa Sasa wanaosubiri watengenezewe Kisha wafunge.
 
Swala la uzito la Ronaldo sio swala la kujitakia bali ni ugonjwa alionao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akiwa Ac Milan kocha alikuwa Ancelloti kabla ya mechi alimwambia ronaldo umeongezeka uzito sana, Ronaldo akamwambia kuwa kama unataka nikakimbie uwanjani basi husinipange ila kama unataka nikafunge magoli nipange , iyo mechi alifunga goli mbili.
 
Akiwa Ac Milan kocha alikuwa Ancelloti kabla ya mechi alimwambia ronaldo umeongezeka uzito sana, Ronaldo akamwambia kuwa kama unataka nikakimbie uwanjani basi husinipange ila kama unataka nikafunge magoli nipange , iyo mechi alifunga goli mbili.
angesikiliza ushauri wa kocha asingevunjika miguu vile!
 

Weak Foot attacked badly.
Right side weight loaded Decision failed knocked out to sleep.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…