Electronic football substitutions board: Hivi inauzwa kiasi gani mpaka timu za Tanzania zinashindwa kununua?

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2018
Posts
21,711
Reaction score
35,644
Hivi haka kadude kanauzwa pesa ngapi hadi TFF na Azam FC, Simba SC, Yanga FC wameshindwa kuvinunua.






Hadi leo wanatumia kidude kama cha sheli za kienyeji.

Nchi inamiliki Uwanja mkubwa kama wa Mkapa tunafelije hii kitu?

 
Electronic FSB kwa gharama sio yakuzishinda taasisi kama TFF au TPLB au vilabu. Kwa ligi zilizoendelea Premier League, Bundesliga, La Liga, ABSA Premier League (Afrika Kusini) huwa ni udhamini kutoka kampuni husika kuweza kutangaza biashara hasa saa (Watches/Clocks).

Tunaweza kuona PL wakiwa na udhamini mnono kutoka TAG Heur kampuni toka Uswissi, moja ya vipengele ni officials kuwa na boards mbili, timu kuingia uwanjani na boards mbili, TAG Heur kutumika katika runinga mainly vitu vinavyohusisha muda, nk.

All in all! TFF, TPLB na Vilabu watafute udhamini kutoka kwa wadau.
 
Wazo zuri, TFF wafanyiekazi msimu ujao wa ligi 2021/22 tuwe na boards za Kisasa angalau Kila Chama cha Mpira kwenye Mkoa wapate Ubao mmoja wa kuendeshea ligi zao.
 
Ukiachia udhamini kwani kama TFF kama msimamizi wa ligi anashindwaje kuvinunua hata vichache au AZAM akanunua cha kutuika CHAMAZI COMPLEX?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…