Eleven-year-old girl gives birth...

Eleven-year-old girl gives birth...

Nyundo_tz

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2009
Posts
640
Reaction score
20
A Bulgarian schoolgirl, aged 11, has given birth to a baby girl on her wedding day.
2832364299-eleven-year-old-girl-gives-birth-bulgaria.jpg
Eleven-year-old girl gives birth in Bulgaria



Kordeza Zhelyazkova reportedly went into labour during her marriage to the child's father, 19-year-old Jeliazko Dimitrov.
It is reported the bride-to-be was still wearing her wedding dress when she arrived at hospital and gave birth to a healthy 5.5lb baby daughter, Violeta.
Zhelyazkova, thought to be the world's youngest mother, told the News of the World that she would not play with toys anymore as she has "a new toy now".
Her husband now faces up to six years in jail for having sex with a minor.

Source: http://uk.news.yahoo.com/4/20091103/twl-eleven-year-old-girl-gives-birth-in-41f21e0.html
 
Binti wa Miaka 11 Ajifungua Mtoto Siku ya Harusi Yake</SPAN>


Binti Kordeza Zhelyazkova mwenye umri wa mwaka mmoja akiwa na mtoto wake aliyejifungua siku ya harusi yake

Binti wa miaka 11 wa nchini Bulgaria ambaye alijifungua mtoto wa kike siku ya harusi yake huku akiwa amevaa shela lake la harusi amesema hataki tena kuendelea na shule na anataka atumie muda mwingi kucheza na mtoto wake.


Kordeza Zhelyazkova mwenye umri wa miaka 11 wa nchini Bulgaria alijifungua salama wiki iliyopita mtoto wa kike mwenye uzito wa kilo 2.4 ambaye alimpa jina la Violeta lakini alitoroka hospitali na mtoto wake usiku huo huo aliojifungua mtoto wake ili awahi kumalizia sherehe za harusi yake.

Kordeza ambaye alikuwa ni mwanafunzi wa shule ya msingi, alisema kuwa alikutana na mumewe mpya mwenye umri wa miaka 19 Jeliazko Dimitrov kwenye viwanja vya michezo vya shule yake baada ya Jeliazko kumuokoa kutoka kwenye kipigo cha wahuni wa mitaani.

Kordeza anadai alianza kufanya mapenzi na Jeliazko bila kutumia kondomu na anakiri alikuwa hajui kondomu ni kitu gani wakati huo.

Kordeza alipata mimba ndani ya wiki moja baada ya kuanza kufanya mapenzi na mpenzi wake huyo.

Kordeza anasema alikuwa hajui kama ana mimba mpaka bibi yake alipoona mabadiliko ya maumbile yake, tumbo lake likizidi kuwa kubwa.

"Nilifikiria labda nimekula burger nyingi sana ndio maana tumbo langu limekuwa kubwa", alisema Kordeza.

"Sitachezea tena madoli, ninalo doli langu jipya nalipenda sana", Kordeza alinukuliwa na gazeti la News of The World la Uingereza akisema.

"Sitarudi shule tena, nimeishakuwa mama",alisema Kordeza.

Wakati huo huo kuna uwezekano wa mumewe kutupwa jela miaka sita kwa kufanya mapenzi na msichana mwenye umri chini ya miaka 14.

Umri unaoruhusiwa kisheria kuanza mapenzi nchini Bulgaria ni miaka 14.

"Ninaogopa sana... nataka nimtunze mtoto wangu na mke wangu lakini kuna uwezakano nikatupwa jela", alisema Jeliazko.

"Nimefanya makosa lakini sitaomba msamaha kwa sababu nimepata mtoto mrembo Violeta", aliongeza Jeliazko.

Mtoto Kordeza amedai hana mpango wa kuzaa mtoto mwingine tena.



Source: News Agencies
 
Back
Top Bottom