Napenda kumuasa mchezaji huyu kuachana kabisa na mawazo ya kujiunga na Simba, Yanga na hata Azam kwa maendeleo yake ya kucheza soka. Badala yake ajikite kutafuta timu yoyote nje ya nchi hii hata Zambia kama walivofanya akina Samata na Ulimwengu. Asiwe na tamaa ya kufanikiwa kwa haraka kwani hata hao akina Samata na Ulimwengu walianza taratibu mpaka sasa wapo katika kiwango cha Kimataifa. Alikuwa Simba lakini wakamuona wa nini sasa wameanza kumvuruga mawazo ili aiache timu yake ya Stand United. Kuchezea timu ya taifa si lazima uwe timu za Simba na Yanga na sasa Azam!