Bigmaaan
JF-Expert Member
- Nov 25, 2023
- 306
- 699
Habari za Jioni wakuu?
Leo nimeona niwashirikishe juu ya mchongo huu. Ni kuwa, hii ni Program maalamu ya kuwawezesha mabinti ambao hawakumaliza elimu ya Sekondari kwa sababu yoyote kujiendeleza kielimu na kifani. Elimu hii wanaipataje na kwa gharama gani?
1. Elimu hii inapatikana kwenye vyuo vyote vya Maendeleo ya wananchi (FDC) zilizopo nchi hii.
2. Kama hakumaliza Form 2, atasoma Form 1 & 2 Mwaka mmoja kisha atafanya mtihani wa Taifa. Akifaulu ataendelea Form 3 hapo hapo chuoni.
3. Kama aliishia Form 3 au Form 4[hakufanya Mtihani wa Taifa] basi atasoma Form 3 & 4 mwaka Mmoja kisha atafanya mtihani wa taifa.
4. Akiwa anasoma masomo hayo, atachagua na FANI MOJA ya itayokuwepo chuoni hapo, Mathalani Chuo cha FDC Urambo au Mbeya wanatoa fani za Umeme wa Majumbani, Ushonaji nguo, Ufundi wa Magari, Uselemala au TEHAMA atachagua moja katia ya fani hizo
5. GHARAMA ZA MASOMO. Hatolipa Ada, Chakula wala hostel [ni sharti aishi hostel za chuo], yeye atagharamika sh 54,000 kukata bima yake ya NHIF [ikiwa hana] na atalipia Uniform yake tu.
Faida kubwa ya Kozi hii ni kutafuta Cheti cha sekondari huku ukipata cheti cha fani ambacho utamuzesha kusaka michongo mingine au hata kujiajiri mwenyewe.
So, kibongo bongo tunao mabinti wenye uhitaji huu. Hebu tuwapeleke kwenye fursa hii.
Leo nimeona niwashirikishe juu ya mchongo huu. Ni kuwa, hii ni Program maalamu ya kuwawezesha mabinti ambao hawakumaliza elimu ya Sekondari kwa sababu yoyote kujiendeleza kielimu na kifani. Elimu hii wanaipataje na kwa gharama gani?
1. Elimu hii inapatikana kwenye vyuo vyote vya Maendeleo ya wananchi (FDC) zilizopo nchi hii.
2. Kama hakumaliza Form 2, atasoma Form 1 & 2 Mwaka mmoja kisha atafanya mtihani wa Taifa. Akifaulu ataendelea Form 3 hapo hapo chuoni.
3. Kama aliishia Form 3 au Form 4[hakufanya Mtihani wa Taifa] basi atasoma Form 3 & 4 mwaka Mmoja kisha atafanya mtihani wa taifa.
4. Akiwa anasoma masomo hayo, atachagua na FANI MOJA ya itayokuwepo chuoni hapo, Mathalani Chuo cha FDC Urambo au Mbeya wanatoa fani za Umeme wa Majumbani, Ushonaji nguo, Ufundi wa Magari, Uselemala au TEHAMA atachagua moja katia ya fani hizo
5. GHARAMA ZA MASOMO. Hatolipa Ada, Chakula wala hostel [ni sharti aishi hostel za chuo], yeye atagharamika sh 54,000 kukata bima yake ya NHIF [ikiwa hana] na atalipia Uniform yake tu.
Faida kubwa ya Kozi hii ni kutafuta Cheti cha sekondari huku ukipata cheti cha fani ambacho utamuzesha kusaka michongo mingine au hata kujiajiri mwenyewe.
So, kibongo bongo tunao mabinti wenye uhitaji huu. Hebu tuwapeleke kwenye fursa hii.