Melubo Letema
JF-Expert Member
- Apr 1, 2020
- 416
- 414
Waandaaji wa mbio za Barabarani nchini Tanzania, wameaswa kuacha kutumia ne no “MARATHON” kwa kila mashindano wanazoanzisha, kwa kuwa zipo tofauti; Marathoni ni kilomita 42, wakati wanaoanzisha mbio za kilomita 21 pia wanaziita Marathon badala ya Nusu Marathoni (half marathon); kupitia ukurasa wa Shirikisho la Riadha Tanzania ; Wameandika hivi;
“……Marathon, ni Mbio Ndefu za Barabarani zenye kukimbiwa kwa umbali wa kilometa Arobaini na Mbili na pointi kama mbili (42.195 Kilometa) , mara nyingi tunafupisha kwa kuandika 42K , hivyo tupate elimu hiyo.
Half Marathon, ni mbio zenye kukimbiwa kwa urefu wa kilometa Ishirini na moja na pointi moja hivi, ( 21.0975 Kilometa) , mara nyingi tunafupisha kwa kuandika 21K, hivyo tupate Elimu Hiyo.
Mwenye rekodi ya Muda bora Tanzania wa Marathoni kwa Sasa ni Gabriel Gerald Geay, (2:03:00)….”
“……Marathon, ni Mbio Ndefu za Barabarani zenye kukimbiwa kwa umbali wa kilometa Arobaini na Mbili na pointi kama mbili (42.195 Kilometa) , mara nyingi tunafupisha kwa kuandika 42K , hivyo tupate elimu hiyo.
Half Marathon, ni mbio zenye kukimbiwa kwa urefu wa kilometa Ishirini na moja na pointi moja hivi, ( 21.0975 Kilometa) , mara nyingi tunafupisha kwa kuandika 21K, hivyo tupate Elimu Hiyo.
Mwenye rekodi ya Muda bora Tanzania wa Marathoni kwa Sasa ni Gabriel Gerald Geay, (2:03:00)….”