S.N.Jilala
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 540
- 507
ELIMU YA HISTORIA: Ni elimu muhimu sana kwetu Bindamu.
Hapa nina lengo moja tu, nalo ni elimu ya Historia na umuhimu wake kwa sisi binadamu. Hapa simaanishi kuwa kila mmoja asome somo la Historia mpaka chuo Kikuu la hasha!!. Nataka kuonyesha kwa ufupi umuhimu wa sisi binadamu kujielimisha na kujua mambo ya kihistoria.
Historia ni mafunzo yanayohusu maendeleo ya mwanadamu. Ni kupitia elimu ya historia sisi tunajua ni kwa jinsi gani mwanadamu aliweza kutawala mazingira yake,akili na uwezo wa kupambanua mambo kulingana na changamoto zilivyojitokeza. Kwa hiyo naweza kusema,elimu ya Historia ni Mama na Baba wa mambo karibu yote Duniani.
Elimu ya Historia ni elimu inayoelezea mambo ya msingi kabisa kwetu binadamu na ni lazima tuyafahamu kinaga ubaga. Kupitia elimu ya Historia tunaelewa kwa undani kabisa maswali kama;
a) Ni nani walikuwepo?
b) Sehemu gani? Na muda gani?
c) Walikutana na changamoto gani na walizitatua vipi?
d) Je njia walizotumia zilikuwa sahihi kutokana na muda ule?
Elimu ya Historia ni elimu inayotoa picha nzuri kuanzia kizazi kilichopita, cha sasa na kizazi kijacho. Mfano,vizazi vilivyopita vilikabilianaje na mambo ya kipuuzi tunayoyashadadia leo kama rushwa,ushoga,ubinafsi wa hali ya juu, lazima utakuta kuwa walipambana na hawakutaka kabisa mambo ya kipuuzi kama haya, na kizazi kilichopo basi mnayakataa wazi wazi. Vilevile,mnaweza kujifunza kuwa hawa watu walifanya hivi lakini kwa sasa tunatakiwa tuenende katika njia hii kutokana na mazingira yetu ya sasa hivi.
Elimu ya Historia ni elimu peke yake inayoweza kumfanya mtu awe mwanazuoni kweli kweli. Ni elimu pia inayowafanya watu kuwa wazalendo na wenye kudhamini Taifa lao. Elimu hii itatufanya tujue na kujiuliza mambo ya misingi kabisa, kama Taifa hili lipo kwa sababu kuna kizazi kilipigana ili kulinda heshima na utu wa mwanadamu. Mwanazuoni na Mwanahistoria maarufu Prof. Mazrui aliwahi kunena;
"Naam,hebu nirejee yale niliyowahi kusema-tunajifunza historia ili tujielewe. Lakini pia inatubidi tuisome ili tuwe na busara zaidi,ubinadamu zaidi,ili tuupunguze ujinga,na hakika tuupunguze ukatili,na mara nyingi kwa kuangalia mustakabali wetu".
Nitawapeni mifano kuntu hapa kidogo. Unaweza ukaiona midogo lakini ni ya maana sana katika elimu ya Historia na maisha ya mwanadamu kwa ujumla.
Moja,ebu uumwe na uende kituo chochote kinachotoa huduma ya afya,na ufike daktari ukupime na kutaka kukuchoma sindano au kukupa dawa ya kunywa,nini unajua kitatokea.Lazima uhoji uhalali wa kukupima na kuanza kukutibu bila ya kuhoji Historia ya ugonjwa wako!!.maana atakupta dawa ambazo zinaweza hata kukuzuru vibaya sana.
Pili, kwa mfano, huwezi kutatua tatizo la mabadiliko ya hali ya hewa bila kujua chanzo chake,ukifanya hivi ni ngumu kutatua changamoto hii.
Kwangu Mimi,elimu ya Historia ni elimu inayowakuza vijana wetu kuwa WAZALENDO katika Taifa letu na jamii zetu kwa ujumla na hata Bara letu la Afrika. Na ni elimu kupitia elimu hii,tunaelewa kwa undani kabisa dhambi upumbavu wa binadamu na kujifunza kutofanya tena. Mfano, elimu ya Historia inawafanya binadamu wasiwe wabaguzi au wasiwabague watu kutokana na dini zao,rangi zao,maeneo wanakotoka.
Ni elimu inayosisitiza haki,utu,na ustashi wa jamii zetu kwa ujumla. Elimu hii inakufanya uchukie dhuruma bila kujali nani ameifanya,uchukie rushwa kutoka moyoni mwako.
Na kusema kweli elimu ya Historia lazima tuikumbatie maana inajenga watoto wetu,vijana wetu,watu wazima,ili waendelee kujua na kukumbuka umuhimu wa mambo yafuatayo;
a) Historia tujifunze uridhi wetu na faida zake zote
b) Kuwa na moyo wa upendo kwa watu wote hapa duniani,
c) Linatufanya tuwe na uwezo dhabiti wa kufikiri katika masula mbalimbali
d) Ni elimu inayoamusha hisia za kimaendeleo
e) Elimu inayotufundisha kuwa WAZALENDO wa kweli.
f) Tunajifunza jinsi ya kuheshimu MIIKO ya. Taifa letu,
g) Kuwakumbuka, kuwaenzi, na kuwaheshimu watu wote waliofia wakilinda heshima na utu wa mwanadamu katika Taifa letu,
h) Elimu inayoonyesha wapi tulikotoka,tuko wapi,na tunaelekea wapi,
i) Elimu inayotufanya tuwe viongozi imara na tusioteteleka kiurahisi.
Hitimisho
Tusipojua tunakotoka hakika hatuwezi kujua tulipo sasa na tunakoelekea kama Taifa. Kwa hiyo elimu ya Historia ni elimu ya msingi na muhimu sana katika ujenzi wa Taifa letu na Bara letu la Afrika.
Hapa nina lengo moja tu, nalo ni elimu ya Historia na umuhimu wake kwa sisi binadamu. Hapa simaanishi kuwa kila mmoja asome somo la Historia mpaka chuo Kikuu la hasha!!. Nataka kuonyesha kwa ufupi umuhimu wa sisi binadamu kujielimisha na kujua mambo ya kihistoria.
Historia ni mafunzo yanayohusu maendeleo ya mwanadamu. Ni kupitia elimu ya historia sisi tunajua ni kwa jinsi gani mwanadamu aliweza kutawala mazingira yake,akili na uwezo wa kupambanua mambo kulingana na changamoto zilivyojitokeza. Kwa hiyo naweza kusema,elimu ya Historia ni Mama na Baba wa mambo karibu yote Duniani.
Elimu ya Historia ni elimu inayoelezea mambo ya msingi kabisa kwetu binadamu na ni lazima tuyafahamu kinaga ubaga. Kupitia elimu ya Historia tunaelewa kwa undani kabisa maswali kama;
a) Ni nani walikuwepo?
b) Sehemu gani? Na muda gani?
c) Walikutana na changamoto gani na walizitatua vipi?
d) Je njia walizotumia zilikuwa sahihi kutokana na muda ule?
Elimu ya Historia ni elimu inayotoa picha nzuri kuanzia kizazi kilichopita, cha sasa na kizazi kijacho. Mfano,vizazi vilivyopita vilikabilianaje na mambo ya kipuuzi tunayoyashadadia leo kama rushwa,ushoga,ubinafsi wa hali ya juu, lazima utakuta kuwa walipambana na hawakutaka kabisa mambo ya kipuuzi kama haya, na kizazi kilichopo basi mnayakataa wazi wazi. Vilevile,mnaweza kujifunza kuwa hawa watu walifanya hivi lakini kwa sasa tunatakiwa tuenende katika njia hii kutokana na mazingira yetu ya sasa hivi.
Elimu ya Historia ni elimu peke yake inayoweza kumfanya mtu awe mwanazuoni kweli kweli. Ni elimu pia inayowafanya watu kuwa wazalendo na wenye kudhamini Taifa lao. Elimu hii itatufanya tujue na kujiuliza mambo ya misingi kabisa, kama Taifa hili lipo kwa sababu kuna kizazi kilipigana ili kulinda heshima na utu wa mwanadamu. Mwanazuoni na Mwanahistoria maarufu Prof. Mazrui aliwahi kunena;
"Naam,hebu nirejee yale niliyowahi kusema-tunajifunza historia ili tujielewe. Lakini pia inatubidi tuisome ili tuwe na busara zaidi,ubinadamu zaidi,ili tuupunguze ujinga,na hakika tuupunguze ukatili,na mara nyingi kwa kuangalia mustakabali wetu".
Nitawapeni mifano kuntu hapa kidogo. Unaweza ukaiona midogo lakini ni ya maana sana katika elimu ya Historia na maisha ya mwanadamu kwa ujumla.
Moja,ebu uumwe na uende kituo chochote kinachotoa huduma ya afya,na ufike daktari ukupime na kutaka kukuchoma sindano au kukupa dawa ya kunywa,nini unajua kitatokea.Lazima uhoji uhalali wa kukupima na kuanza kukutibu bila ya kuhoji Historia ya ugonjwa wako!!.maana atakupta dawa ambazo zinaweza hata kukuzuru vibaya sana.
Pili, kwa mfano, huwezi kutatua tatizo la mabadiliko ya hali ya hewa bila kujua chanzo chake,ukifanya hivi ni ngumu kutatua changamoto hii.
Kwangu Mimi,elimu ya Historia ni elimu inayowakuza vijana wetu kuwa WAZALENDO katika Taifa letu na jamii zetu kwa ujumla na hata Bara letu la Afrika. Na ni elimu kupitia elimu hii,tunaelewa kwa undani kabisa dhambi upumbavu wa binadamu na kujifunza kutofanya tena. Mfano, elimu ya Historia inawafanya binadamu wasiwe wabaguzi au wasiwabague watu kutokana na dini zao,rangi zao,maeneo wanakotoka.
Ni elimu inayosisitiza haki,utu,na ustashi wa jamii zetu kwa ujumla. Elimu hii inakufanya uchukie dhuruma bila kujali nani ameifanya,uchukie rushwa kutoka moyoni mwako.
Na kusema kweli elimu ya Historia lazima tuikumbatie maana inajenga watoto wetu,vijana wetu,watu wazima,ili waendelee kujua na kukumbuka umuhimu wa mambo yafuatayo;
a) Historia tujifunze uridhi wetu na faida zake zote
b) Kuwa na moyo wa upendo kwa watu wote hapa duniani,
c) Linatufanya tuwe na uwezo dhabiti wa kufikiri katika masula mbalimbali
d) Ni elimu inayoamusha hisia za kimaendeleo
e) Elimu inayotufundisha kuwa WAZALENDO wa kweli.
f) Tunajifunza jinsi ya kuheshimu MIIKO ya. Taifa letu,
g) Kuwakumbuka, kuwaenzi, na kuwaheshimu watu wote waliofia wakilinda heshima na utu wa mwanadamu katika Taifa letu,
h) Elimu inayoonyesha wapi tulikotoka,tuko wapi,na tunaelekea wapi,
i) Elimu inayotufanya tuwe viongozi imara na tusioteteleka kiurahisi.
Hitimisho
Tusipojua tunakotoka hakika hatuwezi kujua tulipo sasa na tunakoelekea kama Taifa. Kwa hiyo elimu ya Historia ni elimu ya msingi na muhimu sana katika ujenzi wa Taifa letu na Bara letu la Afrika.