Elimu Ya Msingi ya Lishe

Elimu Ya Msingi ya Lishe

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
Lishe nzuri na mtindo bora wa maisha ni muhimu kwa kila binadamu. Mtindo bora wa maisha ni ule unaozingatia kanuni bora za afya. Mtindo bora wa maisha ni pamoja na kula mlo bora, mazoezi ya mwili, kuepuka matumizi ya pombe, tumbaku au sigara n.k.

Mtindobora wa maisha huuwezesha mwili kujikinga na maradhi mbalimbali hasa maradhi sugu kama vile presha, kisukari, saratani n.k. ulaji wa mlo bora kila siku ni msingi wa afya bora

Lishe ni matokeo ya hatua mbalimbali kuanzia chakula kinapoliwa, kinasagwa, kinavyo menge’nywa na hatimaye kufyonzwa (kusharabiwa) mwilini ili kujenga afya bora ya mwili. Lishe bora inatokana na kula vyakula vinavyokidhi mahitaji ya mwili kwa kiwango, ubora na usalama wa chakula husika

Utapiamlo

Utapiamlo ni hali ya afya duni itokanayo na ulaji duni usiokidhi mahitaji ya mwili au ulaji
uliopitiliza mahitaji ya mwili. Utapiamlo unaotokana na ulaji duni usiokidhi mahitaji ya
mwili huitwa lishe hafifu na utapiamplo unaotokana na ulaji uliopitiliza mahitaji ya mwili
huitwa lishe iliyokithiri. Ili kuzuia utapiamlo in muhimu kelewa sababu zinazosababisha
utapiamlo ili kukabiliana na tatizo. Sababu hizo ni pamoja na:

 Ulaji duni wa chakula unaotonakana na kula milo michache na kiasi kisichotosheleza
mahitaji ya virutubishi mwilini. Hii hujuimuisha kutokuwanyonyesha watoto
ipasavyao.

 Magonjwa ya mara kwa mara huondoa hamu ya kula, husababisha ufyonzwaji wa
duni wa virutubishi na huongeza mahitaji ya virutubishi mwilini. Magonjwa hayo ni
kama vile kuharisha, magonjwa ya mfumo wa hewa na malaria.

Aina za utapiamlo
 Unyafuzi na ukondefu
o Ukondefu na kuvimba miguu yote miwili (Utapiamlo wa muda mfupi)
o Udumavu (Utapiamlo wa muda mrefu)
o Uzito mdogo (unajumuisha udumavu na ukondefu)
 Upungufu wa vitamini na madini mbalimbali
 Uzito uliokithiri na kiribatumbo
Utapiamlo huchangia katika ongezeko la magonjwa na vifo vya watoto wenye umri chini ya
miaka mitano.
Magonjwa yatokanayo na utapiamlo ndio chanzo kikuu cha mwili kuwa na afya mb
 
Mimi ni mmojawapo wa wakufunzi wazuri wa kuwahimiza watu wale kwa afya ila leo asubuhi nimetandika chapati mbili na maharagwe bakuli zima...
Kuuishi ukweli ni changamoto haswa.
 
Lishe nzuri na mtindo bora wa maisha ni muhimu kwa kila binadamu. Mtindo bora wa maisha ni ule unaozingatia kanuni bora za afya. Mtindo bora wa maisha ni pamoja na kula mlo bora, mazoezi ya mwili, kuepuka matumizi ya pombe, tumbaku au sigara n.k.

Mtindobora wa maisha huuwezesha mwili kujikinga na maradhi mbalimbali hasa maradhi sugu kama vile presha, kisukari, saratani n.k. ulaji wa mlo bora kila siku ni msingi wa afya bora

Lishe ni matokeo ya hatua mbalimbali kuanzia chakula kinapoliwa, kinasagwa, kinavyo menge’nywa na hatimaye kufyonzwa (kusharabiwa) mwilini ili kujenga afya bora ya mwili. Lishe bora inatokana na kula vyakula vinavyokidhi mahitaji ya mwili kwa kiwango, ubora na usalama wa chakula husika

Utapiamlo

Utapiamlo ni hali ya afya duni itokanayo na ulaji duni usiokidhi mahitaji ya mwili au ulaji
uliopitiliza mahitaji ya mwili. Utapiamlo unaotokana na ulaji duni usiokidhi mahitaji ya
mwili huitwa lishe hafifu na utapiamplo unaotokana na ulaji uliopitiliza mahitaji ya mwili
huitwa lishe iliyokithiri. Ili kuzuia utapiamlo in muhimu kelewa sababu zinazosababisha
utapiamlo ili kukabiliana na tatizo. Sababu hizo ni pamoja na:

 Ulaji duni wa chakula unaotonakana na kula milo michache na kiasi kisichotosheleza
mahitaji ya virutubishi mwilini. Hii hujuimuisha kutokuwanyonyesha watoto
ipasavyao.

 Magonjwa ya mara kwa mara huondoa hamu ya kula, husababisha ufyonzwaji wa
duni wa virutubishi na huongeza mahitaji ya virutubishi mwilini. Magonjwa hayo ni
kama vile kuharisha, magonjwa ya mfumo wa hewa na malaria.

Aina za utapiamlo
 Unyafuzi na ukondefu
o Ukondefu na kuvimba miguu yote miwili (Utapiamlo wa muda mfupi)
o Udumavu (Utapiamlo wa muda mrefu)
o Uzito mdogo (unajumuisha udumavu na ukondefu)
 Upungufu wa vitamini na madini mbalimbali
 Uzito uliokithiri na kiribatumbo
Utapiamlo huchangia katika ongezeko la magonjwa na vifo vya watoto wenye umri chini ya
miaka mitano.
Magonjwa yatokanayo na utapiamlo ndio chanzo kikuu cha mwili kuwa na afya mb
kwani hamna virutubisho vinavyopatikana katika pombe? tuweke pembeni ALCOHOL
 
Back
Top Bottom