Elisha Chuma : Jinsi ya kuanza safari ya kumiliki kipato chako

Elisha Chuma : Jinsi ya kuanza safari ya kumiliki kipato chako

Elisha Chuma

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
282
Reaction score
275
Matumizi ndio yanayotengeneza sura ama picha nzima ya kipato chako siku zote watu wengi wanafeli sheria ndogo ndogo kama hii ya matumizi ya pesa,hakikisha matumizi yako hayazidi kipato chako.

watu wengi wanatengeneza matumizi hadi yanapitiliza kiwango cha kipato chao na mwisho wake huishia kusema wanapata pesa lakini haionekani hiyo ni kwa sababu matumizi ya pesa yako juu hata kama ni mshahara umeshaumaliza kabla hata haujafika yaani ukipokea tayari wote unaishia kwenye madeni ya mwezi uliopita, ukijiona uko kwenye hali hiyo basi ni suala la msingi kuanza kuangalia kwa umakini matumizi yako ya mwezi,wiki ama siku ili utengeneze matumizi yenye uhalisia na yaliyondani ya kipato chako.

Ukiweza kusimamia matumizi yako yakawa chini ya kipato chako unakuwa na uwezo mkubwa wa kufanya vitu vingine vya kukuongezea kipato hata kuweka akiba inayokaa.

#Maishanihayahaya siku inamasaa yale yale 24 kwa watu wote kinachotofautisha ni matumizi ya hayo masaa kwa mtu na mtu,jitathmini kama kuna cha kubadilisha badilisha bado #wakubadilikaniwewe
uwe na Jumatatu njema...
 
Thamani ya muda.
Watanzania wengi hatujui thamani ya muda, time is money and time is a factor of production.
Muda ni kama maji ya mtoni, ukiyagusa hutoyagusa tena
 
Kwa kipato gani mkuu,maana hapo usisomeshe ili uweze kusave hela,uende kazini na baiskeli ili usave hela,usioe ili usave hela,uache kuwahudumia wazazi wako kwenye hospitali na uwapeleke kwa waganga wa kienyeji ili usave hela,kwa mtindo huo wacha tu ni we masikini,muda wangu wa kuishi utakapofika ntakwenda,na kidogo Mungu alichonijalia kuifanyia familia yangu ndicho ntakacho waachia...
 
Hakikisha matumizi yako hayazidi kipato chako.


Kwa iyo unataka kutuambia.

Kipato changu kikiwa million moja alafu na mimi natumia million kwa mwez..

Hapo ndio naanza yaona mafanikio mkuu?
 
Hakikisha matumizi yako hayazidi kipato chako.


Kwa iyo unataka kutuambia.

Kipato changu kikiwa million moja alafu na mimi natumia million kwa mwez..

Hapo ndio naanza yaona mafanikio mkuu?
WALIMU WANA KAZI SANA DUH
 
Back
Top Bottom