Elizabeth Bathory: Mwanamke muuaji hatari zaidi kuwahi kutokea katika historia ya dunia

Elizabeth Bathory: Mwanamke muuaji hatari zaidi kuwahi kutokea katika historia ya dunia

FM facts

Member
Joined
Mar 16, 2019
Posts
45
Reaction score
88
Elizabeth Bathory Alizaliwa Augost 7, 1560 Huko Hungary na Kufariki Augost 14, 1614 na Anatajwa Kuwa ni Mmoja Kati Wanawake Wauwaji Hatari zaidi Kuwahi Kutokea Katika Historia ya Dunia.

Alikua anafahamika Pia kwa Majina ya 'The Blood Countess'

'The Čachtice Countess' na hii ni Kutokana na Unyama wake Aliokua Akiufanya na Kwa Mujibu wa Kitabu cha Rekodi za Dunia Huyu ndie Mwanamke Muuwaji Hatari Kuwahi Kutokea Duniani.

Inaelezwa Kwamba Alipatikana na Hatia ya Kuwauwa Watoto Zaidi ya 650! Kati ya Miaka ya 1585-1609 na Alikuwa Anawauwa, Anawakamua Damu na Kuogea! (Anaoga Damu) Lengo likiwa ni Kuifanya Ngozi yake Kuwa Nyororo na Isiyozeeka.

Inaelezwa Elizabeth Alikuwa Msomi na Tajiri Aliyekua Anamiliki Mashamba makubwa sana Huko Hungary na Baada ya Mumewe Kufariki Mwaka 1604 Siri zake Kuhusu Mauwaji Zilianza Kuvuja na Inaelezwa Zaidi ya Mashahidi 300 Waliitwa Kutolea Ushahidi.

Elizabeth Alikutwa na Hatia ya Kuwauwa Mabinti wadogo wa Kati ya Miaka 10-14 Akitumia Nyumba yake Iliyokuwa Milimani Kuficha Siri hizo Vitendo alivyokuwa Akivifanya Kwa Kusaidiana na Vijakazi wake Aliwowaajiri.

Watoto Hao Alikua Akiwapata kwa Kuwaita Kufanya kazi Mashambani kwake Akiwaahidi Kuwapa Ujira Mzuri.

Alikamatwa December 30, 1609 na Kufungwa Kifungo cha Maisha Jela huku ikielezwa Chumba Alichofungiwa Hakikua na Mwanga Wowote wala Sehemu ya Kutokea!, Kilikua na Tobo Dogo tuu la Kuweza Kupitishia Sahani ya Msosi! na Alikaa Humo kwa Miaka Minne tuu Kabla ya Kufariki Augost 14, 1614.p

Inaelezwa Kwamba Usiku wa Kabla ya Kifo Elizabeth Alilalamika kwa Walinzi wa Gereza Kwamba Mkono wake Ulikua Unauma lakini Walimpuuzia, na Asubuhi Akakutwa Kafariki Dunia na Alizikwa November 25, 1614 Kando ya Kanisa la Čachtice Church huko Hungary.

Tufollow Instagram @fm_facts

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dunia duara


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hata walio mhukumu kifungo cha maisha pamoja na majaji na wote walio skiliza hiyo kesi hawapo tena duniani walisha fariki. CCM wana la kujifunza kupitia comment yangu.
 
Back
Top Bottom