Ella Harper: Mwanamke aliyeitwa ‘ngamia’

Ella Harper: Mwanamke aliyeitwa ‘ngamia’

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
1611927116032.png

Ella Harper alizaliwa Januari 5, 1870 akiwa na tatizo la mifupa ambalo lilisababisha magoti yake kujipinda kwa nyuma hali iliyomlazimisha kutembea kama mnyama.

Ugonjwa wa mifupa aliokuwa nao ulikuwa unafahamika kama Congenital genu recurvatum. Ambapo kwa hali hiyo ilimfanya wamuite jina ‘The camel Girl’ au msichana ngamia.

Mwaka 1886 alijiunga na kikundi cha maonesho mbali na ulemavu wake na alikuwa akijipatia $200 kwa mwezi kama mshahara hali iliyoleta nuru katika maisha yake.

Harper alifariki Desemba 19, 1921. Hii inanesha walioendelea hawakuwa wanawafungia walemavu tangu enzi hizo, tofauti na nchi zinazoendelea ambapo mara nyingi watoto walemavu wamekuwa wakifichwa.
 
Nashauri sana walemavu wetu wasiachwe wawe ombaomba na kutumika kama kitega-uchumi (chuma ulete) kwa wenye uchu wa fedha. Hawa wanapaswa kutafutiwa kazi inayoendendana na hali zao, ili wajipatie kipato na kufurahia kuendesha maisha yao kama wengine. Hawakulemaa akili, bali sehemu tu za mwili wao.
 
Back
Top Bottom