Elon Musk anataka majaribio ya Starship yafikie 25, mwaka 2025

Elon Musk anataka majaribio ya Starship yafikie 25, mwaka 2025

incognitoTz

Senior Member
Joined
Apr 19, 2019
Posts
133
Reaction score
172
Starship siku chache kabla ya uzinduzi wake mwezi Aprili. Picha: SpaceX


Elon Musk anataka SpaceX kuongeza majaribio ya kurusha roketi ya Starship kutoka mala 5, 2024 hadi 25 kwa mwaka 2025. Hata hivyo mpango huo wa kuongeza hiyo idadi unahitaji idhini ya FAA.FAA, Federal Aviation Administration ndio yenye mamlaka ya kutoa vibali vya kurusha roketi za kibiashara.
Starship namba 24 ikiwasha injini zake sita za Raptor wakati wa jaribio fupi la Static fire mnamo Desemba 15, 2022.  picha: SpaceX

Starship ni roketi kubwa inayoweza kutumika tena (re-usable), iliyoundwa kwaajili ya safari za Mwezini na Mars. Kumekuwa na wasiwasi juu ya athari za kimazingira na kukidhi kwa vigezo vya kufanya ongezeko hilo.
Musk amekuwa na mikwaruzano ya mala kwa mala na FAA juu suala hilo, huku akiishutumu mamlaka hiyo juu ya unyanyasaji wa kiudhibiti. Hali inayoweza kubadirika kipindi hiki ambacho Elon Musk anaendakuwa sehemu serikali ya Marekani katika idara ya uwajibikaji na ufanisi huku rafiki yake wa karibu Jared Isacman akitarajiwa kuapishwa kuwa mkuu wa NASA Januari 20, 2025.

Booster ya Super Heavy ikijitenganisha na Starship kwenye safari yake ya majaribio ya Novemba 19. Picha: SpaceX


Licha ya ongezeka la idadi ya majaribio ya Starship kuwa na tija katika maendeleo uchunguzi wa anga bado vikwazo vya kimazingira na kiudhibiti vinaweza vikazuia jitihada hizo.
 
Back
Top Bottom