Endapo Katiba Inayopendekezwa ingepitishwa kero za Muungano zingekwisha- Kikwete

Endapo Katiba Inayopendekezwa ingepitishwa kero za Muungano zingekwisha- Kikwete

bmbalamwezi

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2015
Posts
788
Reaction score
195
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mhe. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa kama Katiba Inayopendekezwa Ingepitishwa, hakuna kipolo ambacho kingesalia kwenye kero za Muungano. Katiba hii ni nzuri sana kwa ajili ya maslahi ya Taifa. Rais Kikwete ameyasema hayo leo wakati akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa mara ya mwisho akiwa Rais. Ameipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya uongozi wa Jaji Joseph Sinde Warioba na Bunge Maalum la Katiba chini ya Mhe. Samwel Sitta. Amesema kinachosubiriwa ni Tume kuitisha Kura ya Maoni kwa ajili ya kuitimisha mchakato wa Katiba Mpya.
 
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mhe. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa kama Katiba Inayopendekezwa Ingepitishwa, hakuna kipolo ambacho kingesalia kwenye kero za Muungano. Katiba hii ni nzuri sana kwa ajili ya maslahi ya Taifa. Rais Kikwete ameyasema hayo leo wakati akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa mara ya mwisho akiwa Rais. Ameipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya uongozi wa Jaji Joseph Sinde Warioba na Bunge Maalum la Katiba chini ya Mhe. Samwel Sitta. Amesema kinachosubiriwa ni Tume kuitisha Kura ya Maoni kwa ajili ya kuitimisha mchakato wa Katiba Mpya.
Heko hili limetulia naamini kabisa endapo utpitishwa basi hakika hizi kero za Muungano zitakuwa historia mkuu Mbalamwezi, safi sana kwa hoja nzuri na makini
 
hiki ni kituko kingine cha Rais anajifanya hamnazo katiba pendekezwa haina tofauti na hii tuliyonayo kwa maana ya misingi mikuu
 
hiki ni kituko kingine cha Rais anajifanya hamnazo katiba pendekezwa haina tofauti na hii tuliyonayo kwa maana ya misingi mikuu
Wewe acha uongo wako hapa, inafananaje na hii wakati hata rangi ya Katiba yenyewe cover yake huijui? Kwanza hujaisoma ndo maana unaweka uongo wako hapa, najua umetumwa na maboss wako hao, sasa kaa ukijua kuwa Katiba Inayopendekezwa nzuri, kwanza kama unasema ile ya 77 nimsawa na hii mbona hiyo ya 1977 haikuweka TAKUKURU? Kama kweli umezisoma utagundua mapungufu ya ile ya zamani, sasa hii mpya ama Inayopendekezwa imetaja chombo cha kuuma wala rushwa yani TAKUKURU katika Ibara ya 249' kijana utoapo hoja usikurupuke na kuropoka eti hii Inayopendekezwa ni sawa na ile ya 1977, Lol! We kweli hamnazo wala huijui ya zamani wala hii Inayopendekezwa, sasa nakushauri pia ukazisome zote kwa makini then uje kuona mapungufu ya hiyo ya zamani.
 
hiki ni kituko kingine cha Rais anajifanya hamnazo katiba pendekezwa haina tofauti na hii tuliyonayo kwa maana ya misingi mikuu

tol, Ama kweli upofu sio lazima kuwa wa macho ya kawaida. Wewe ni full kipofu maana hujui hata hicho unachokizungumza. Kwa watu tuiyeisoma, ya sasa Inayopendekezwa ni bonge la Katiba ambayo inatambua Watanzania wote na mahitaji yao katika malundi yao. Tanzania itafika salama kwenye malengo yake ya 2025 kwa Katiba Inayopendekezwa ikiidhinishwa na Watanzania. Wenye figisu figisu wanalao jambo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
hiki ni kituko kingine cha Rais anajifanya hamnazo katiba pendekezwa haina tofauti na hii tuliyonayo kwa maana ya misingi mikuu
Wewe ndo miongoni mwa wale wajinga waliokosa elimu ama ulipata 0 wakati unasoma, unafaganisha hzo katiba kwanza umewahi kuzisoma? Kazisome iki uone utofauti uliopo
 
Mbona hii mada mnachangia kimipasho, zameni kwny vifungu hasa hapo kwny muungano kwa nyie mleyepata bahati ya kuisoma. Nasi tuone ubora wake.
 
Mbona hii mada mnachangia kimipasho, zameni kwny vifungu hasa hapo kwny muungano kwa nyie mleyepata bahati ya kuisoma. Nasi tuone ubora wake.
Unaonekana hata wewe hujaisoma hiyo katiba mpyaa ndo maana unaropoka, kwanza hii mpya imetaja TAKUKURU Ibara ya 249 kwa mara ya kwanza, imetaja hakiza WASANII pia kwa maraya kwanza kinyume na ile ya 77 haikutaja Takukuru wala Wasanii je huoni hapo kuna ubora wa hii mpya?
 
Unaonekana hata wewe hujaisoma hiyo katiba mpyaa ndo maana unaropoka, kwanza hii mpya imetaja TAKUKURU Ibara ya 249 kwa mara ya kwanza, imetaja hakiza WASANII pia kwa maraya kwanza kinyume na ile ya 77 haikutaja Takukuru wala Wasanii je huoni hapo kuna ubora wa hii mpya?

Hongera sana unaonekana unayajua jua hayo mambo. Tiririka mwanangu tujifunze wenzako ambao tu wavivu wa kupitia kitabu chote. Wewe tumegee megee. Si unajua kibongo bongo? Hata ambao hawajaisoma kimbele mbele kuvuruga tu! We toa somo mwanangu
 
Back
Top Bottom