kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Usajili wa wachezaji wageni: Kutumia social media kusema kuwa kila mchezaji mpya unaemsajili ni Bora kuliko aliyeko kwenye position Sasa sio lugha sahihi kutumiwa na kiongozi mkubwa ndani ya Yanga. Inawezekana hiyo ndiyo falsafa sahihi ya kusajili mchezaji mpya kwenye timu lakini sio lazima kiongozi aitamke hadharani na kwenye social media kwakuwa hii inavunja moyo wachezaji walioko kwenye nafasi hiyo Sasa.
Usajili ni kama kamali unayemleta anaweza asiwe Bora uwanjani kuliko uliyenae. Ni kweli kinadharia mchezaji mpya lazima awe Bora kuliko aliyeko lakini kiongozi mkubwa kama Rais wa club hapaswi kunena hayo kwa wachezaji wake waliomsaidia kuifikisha timu hapo ilipo. Kwanini mchezaji mpya kasajiliwa na wa zamani kaachwa au kaongezewa mtu mwingine inapaswa kuwa ni Siri ya jando ya bench la ufundi na uongozi, haizungumzwi hadharani. Wacha wadau wakapime wenyewe kazi zao uwanjani badala ya wewe kubeza walioko.
Naomba mfanye vitu kitaaluma, punguzeni mihemko mnapopata nafasi ya kuongea na wanahabari. Tafakarini athari kabla ya kusema chochote kwenda hewani
Usajili ni kama kamali unayemleta anaweza asiwe Bora uwanjani kuliko uliyenae. Ni kweli kinadharia mchezaji mpya lazima awe Bora kuliko aliyeko lakini kiongozi mkubwa kama Rais wa club hapaswi kunena hayo kwa wachezaji wake waliomsaidia kuifikisha timu hapo ilipo. Kwanini mchezaji mpya kasajiliwa na wa zamani kaachwa au kaongezewa mtu mwingine inapaswa kuwa ni Siri ya jando ya bench la ufundi na uongozi, haizungumzwi hadharani. Wacha wadau wakapime wenyewe kazi zao uwanjani badala ya wewe kubeza walioko.
Naomba mfanye vitu kitaaluma, punguzeni mihemko mnapopata nafasi ya kuongea na wanahabari. Tafakarini athari kabla ya kusema chochote kwenda hewani