Rajab_Omar
JF-Expert Member
- May 15, 2016
- 16,482
- 27,182
Tunapozungumzia Timu yenye mashabiki kipenzi cha mioyo ya Watanzania yenye washabiki wengi Afrika Mashariki wapatao takribani Milioni 15 Tanzania na Afrika Mashariki kwa Ujumla, Timu Bingwa wa Kihistoria zamani Wakimataifa, Timu yenye Mafanikio makubwa zaidi ndani ya Tanzania, Timu ambayo ni Mali ya Wananchi, basi hapo tunaizungumzia Timu yetu pendwa Dar Young Africans Sports Club.
Hivyo Timu kubwa zaidi kwa Ukanda huu wa Afrika Mashariki siku zote inaendeshwa kwa Ukweli na Uwazi ili sisi Wanachama mashuhuri pamoja na Wapoja na Wapenzi na Wapiga debe wa JF wafahamu kinachoendelea ndani ya Timu yetu.
Kwa leo Mimi mwanachama mashuhuri wa Yanga sihitaji Jengine Bali ni kumtaka Eng. Hersi Saidi atuambie mpaka kufikia leo Rufaa yetu dhidi ya BEN MORRISON imefikia wapi?
Utaratibu wa CAS wanapopokea Rufaa hutangaza Muda/tarehe ya kuisikiliza na kutoa hukumu! Lakini kwa hili la Morrison kwa mshangao mkubwa na hali isiyo ya kawaida Rufaa yake hata kwenye Dashboard ya CAS sehemu ya Appeals haionekani na hata ukisearch unajibiwa "No result found".
Je, hii inasadiki yaleyale maneno tuliyokuwa tunaambiwa na Watani zetu Simba kuwa "Uongozi umetudanganya sisi Wanachama na Washabiki wa Yanga kuwa Wamekata Rufaa ili kututuliza tusiwaone kuwa ni Wazembe kwenye sakata hili?"
Tafadhali Wananchi tupatiwe majibu juu ya muendelezo wa Rufaa yetu dhidi ya Morrison na kama hakuna Rufaa iliyokatwa pia tuambiwe kuwa hakuna Rufaa na sisi tutasamehe kwa maslahi ya Timu yetu pendwa ya Yanga.
DaimbaMbeleNyumaMwiko
Hivyo Timu kubwa zaidi kwa Ukanda huu wa Afrika Mashariki siku zote inaendeshwa kwa Ukweli na Uwazi ili sisi Wanachama mashuhuri pamoja na Wapoja na Wapenzi na Wapiga debe wa JF wafahamu kinachoendelea ndani ya Timu yetu.
Kwa leo Mimi mwanachama mashuhuri wa Yanga sihitaji Jengine Bali ni kumtaka Eng. Hersi Saidi atuambie mpaka kufikia leo Rufaa yetu dhidi ya BEN MORRISON imefikia wapi?
Utaratibu wa CAS wanapopokea Rufaa hutangaza Muda/tarehe ya kuisikiliza na kutoa hukumu! Lakini kwa hili la Morrison kwa mshangao mkubwa na hali isiyo ya kawaida Rufaa yake hata kwenye Dashboard ya CAS sehemu ya Appeals haionekani na hata ukisearch unajibiwa "No result found".
Je, hii inasadiki yaleyale maneno tuliyokuwa tunaambiwa na Watani zetu Simba kuwa "Uongozi umetudanganya sisi Wanachama na Washabiki wa Yanga kuwa Wamekata Rufaa ili kututuliza tusiwaone kuwa ni Wazembe kwenye sakata hili?"
Tafadhali Wananchi tupatiwe majibu juu ya muendelezo wa Rufaa yetu dhidi ya Morrison na kama hakuna Rufaa iliyokatwa pia tuambiwe kuwa hakuna Rufaa na sisi tutasamehe kwa maslahi ya Timu yetu pendwa ya Yanga.
DaimbaMbeleNyumaMwiko