Eng. Rogatus Mativila: Ujenzi wa barabara Wasso hadi Sale (km 49) umegharamiwa na Serikali kwa 100%

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
590
Reaction score
807

Akitoa taarifa fupi ya Mradi huo Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng: Rogatus Mativila amesema Ujenzi wa barabara Wasso hadi Sale (km 49) ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha mtandao wa barabara nchini kwa kujenga Barabara Kuu na za Mikoa kwa kiwango cha lami.

Amesema kusudio la kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami ni kupunguza gharama za usafiri na usafirishaji, kupunguza muda wa usafiri na usafirishaji wa mazao na mifugo kutoka ukanda huo hasa wakazi wa Wilaya ya Ngorongoro katika mji wa Loliondo na vitongoji vyake ili kuongeza thamani ya mazao na mifugo na kukuza kipato kwa Wananchi waishio maeneo hayo, hivyo kuchochea ukuaji wa sekta ya utalii katika nchi hasa katika Hifadhi za Taifa za Serengeti na Ngorongoro.

Eng: Mativila ameeleza kuwa Mkandarasi aliyejenga sehemu ya kwanza ya Wasso - Sale ni Kampuni ya China Wu Yi Co. Ltd ya China kwa gharama ya Shilingi Bilioni 87.126, na kwamba mradi huo ulisimamiwa na TANROADS kupitia kitengo chake cha Uhandisi kiitwacho TANROADS Engineering Consulting Unit (TECU).

Aidha utekelezaji wa Mkataba wa kipande hicho cha barabara umegharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100, na mradi ulitoa jumla ya ajira 426 kwa wazawa na 21 wafanyakazi wa kigeni.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…